Kununua gari au kujenga nyumba

Kununua gari au kujenga nyumba

Ushauri ni kua atafute kiwanja anunue, kisha anunue hilo gari kwa sababu viwanja vinapanda sana bei kila kukicha pia ni rahisi kuanza ujenzi kama unakiwanja. Hii inamaana utajenga kwa awamu tena kwa kudunduliza mfano msingi ukafata kozi nne, ukamalizia hadi kumi, ukafuata renta na kozi mbili, ukapaauwa kisha finishing taratitaratibu kulingana ela unayopata. nyumba huwa inajengwa hata miaka 10 ila inaisha maana kila hatua huwa inapita. Pia gari ni liability tena ni vampire ktk pesa kama haliingozi pato.
 
kunamtu aliwahi sema "gari ni mke wa pili" sijui alichomaanisha. Ni kweli kwamba gari sio anasa, kuwa na kwako pia kunafaida nyingi mno. Kama ni mfanya biashara au anamalengo ya kufanya biashara na biashara yake inahtaji gari sioni ajabu akinunua, ila kama ni mtu wa kuamka na kwenda ofsni (apaki gari) hadi jioni arudi nyumbani itakuwa uchizi kununua gari.
 
Mkuu kama upo Dar uni-pm nina kiwanja chenye nyumba (vyumba 2 na sebule)
 
Njoo nikupe Kiwanja ujenge ndugu. Chini ya million sta. Bunju. Ni pm 30 x 25
 
Ufafanuzi zaidi unahitajika. Hatujaelezwa kama hizo pesa za kununulia gari au kujengea zitapatikana kwa mkopo au akiba (savings).
 
Mimi nawashauri waanze na gari flan simple isiyokula mafuta sana. Itawasaidia sana na amini usiamini itawaongezea hata confidence na self asteem watajikuta wanabuni hata mbinu za kuongeza kipato. Mimi nilianza na gari 3 yrs ago, baadae kiwanja na nikajikuta nimejenga niko kwangu. Ukiwa na gari bana kuna furaha flani unakuwa nayo! Chukulia mmetoka kidogo wewe na wife mkakaa na washikaji pale Calabash. Mnakaa labda kimara au tabata, hapo tu mlipokaa mnawaza jinsi ya kuondoka, taxi expensive, daladala ndo hivyo tena mnafika hoi. Katoto kakipata homa ghafla usiku unakawahisha fasta hospital, mkwe kakutembelea kumchukuwa au kumpeleka kituoni siku anafika au kuondoka.......ziko faida nyingi kwa kweli ukiwa na kausafiri!
 
Nyumba ni muhimu sana hasa kwasasa wanapanga huku familia hiyo ni kubwa.
 
Habari wadau, Nina rafiki yangu wa siku nyingi alinifuata hivi karibuni kuniomba ushauri, yeye ameoa na wamebahatika kupata watoto wawili, kwa sasa anaishi nyumba ya kupanga. Ameniambia yeye na mkewe wapo katika malumbano ya kuhusu kipi waanze kukifanya kati ya kununua gari ama kununua kiwanja na kuanza ujenzi!! Kipato chao kwa mwez jumla huwa kati ya sh lak 8 hadi mil 1 na lak 2. sijui ndugu zangu mngewashauri waanze na ujenzi au gari?

hapa nilipo nawaza ikitokea amenunua leo halafu kesho yake akagonga gar nyingine vibaya sana. watakuwa kwenye hali gan
 
Habari wadau, Nina rafiki yangu wa siku nyingi alinifuata hivi karibuni kuniomba ushauri, yeye ameoa na wamebahatika kupata watoto wawili, kwa sasa anaishi nyumba ya kupanga. Ameniambia yeye na mkewe wapo katika malumbano ya kuhusu kipi waanze kukifanya kati ya kununua gari ama kununua kiwanja na kuanza ujenzi!! Kipato chao kwa mwez jumla huwa kati ya sh lak 8 hadi mil 1 na lak 2. sijui ndugu zangu mngewashauri waanze na ujenzi au gari?

Gari ni rahisi sana kununua tatizo linakuja katika kulitunza kwa wastani gharama za kuendesha gari hazipungui millioni tisa kwa mwaka ikiwemo wastani wa mafuta ya shillingi 15,000 kila siku inayofanya kuwa 450,000 kwa mwezi na kwa mwaka 5,400,000/- achilia services zenye wastani wa 100,000/- kwa mwezi barabara zetu si unazijua! hivyo kuna 3,600,000/- bado gharama za pack mjini kila siku kama 600/- kupaki jioni 1000/- au mlinzi kuosha gari 2000/- kwa siku.
lakini lililo tamu zaidi ni mitoko ya hapa na pale mama atataka kila harusi mchange ili muende kutembelea familia na mengine zaidi.
ki ukweli nilipokuwa na gari sikuweza kuanza ujenzi ila mara baada ya kupata ajali na gari kuwa haifai kabisa ujenzi ukaanza tena. hivyo achana na gari kwanza wacha watu wakucheke lakini lazima ujue nini unataka

ujenzi ni rahisi sana unaweza kuamua kununua matofari au kufyatua inategemea
tenga kila wiki 60,000 kwa tofari moja shillingi 1000/- utapata matofari 60 kwa mwezi matofari 240 kwa miezi sita 1,440 ambayo haya yanaweza kukusaidia kufikisha nyumba kiunoni.
au nunua nifuko minne kila wiki kwa shilling 60000 itaongezeka kidogo kila mfuko tofari 35 kwa mifuko minne tofari 140 kwa mwezi tofari 560 kwa miezi sita 3660 zinatosha kwa kiasi kikubwa kujenga nyumba ya kawaida.
jipange kwa mpango uleule weka hela ya ujenzi baada ya kukusanya matofari kwa miezi sita na anza ujenzi
 
Ushauri Muhimu kabisa waanze na Nyumba kwa sababu:
1/Nyumba ni mali isiyohamishika hivyo ni dhamana muhimu mahali popote pale duniani iwe Mahakamani, Benki, Biashara, Maishani, Kazini nk.

2/Thamani ya Nyumba inakwenda inaongezeka kila siku(Hata siku wakitaka kuiuza wataiuza kwa thamani kubwa zaidi).

3/Watakuwa wameondoa gharama za kupanga na usumbufu wake(Watakuwa huru sana)

4/Nyumba ni Akiba ya kudumu maishani(Wataishi wao na vizazi vyao)

5/Nyumba ni kipimo cha Heshima, Hekima, Busara na Upeo kijamii, kifamilia, kimila, kiserikali nk.

6/Nyumba ni Mtaji wa Maisha(Hawatatoa tena pesa zao kila siku au kila Mwezi kulipia gharama za kuishi kwenye hiyo nyumba zaidi wanaweza kupata kipato zaidi kama sehemu ya hiyo nyumba watapangisha)

7/Nyumba inaweza kuwaletea vitu vingine vingi kama Gari kama watafanya mahesabu vizuri(Kwa mfano wanaweza kuitumia kama dhamana katika taasisi za kipesa kukopa pesa za kununulia gari nk.)

NOTE;
Kwanini wasianze na Gari:
A/Gari inahitaji gharama kubwa sana kulihudumia(Kwa mfano Insurance, Kodi ya Mapato, Mafuta ya kila siku, Service ya kila mara, Parking ya kila siku, Trafiki, Vipuri nk)

B/Gari itakuzidishia gharama zaidi za maisha pasipo msingi.(Mfumo wako wa maisha unaweza ukabadilika ili kukidhi tu fahari ya kumiliki gari. eg.Kula, kuvaa, Makazi, matembezi, Marafiki, Ndugu, Jamaa nk.) Hili jambo nimeliona kwa watu wengi sana mijini. Kifupi Gari halipatani sana na mbana matumizi!!!

C/Thamani ya Gari mara nyingi inakwenda ikipungua tokea ile siku unalimiki.

D/Gari ni chombo kinachochakaa kwa upesi sana kadri siku zinavyokwenda au unavyolitumia(Mara nyingi magari mengi yanakuwa yameanza kuchakaa vibaya baada ya miaka mitatu tu!!)

E/Gari lina tabia ya kukugeuza kuwa Mtumwa wake(Kwa mfano Wakati wote litakuhitaji kutoa pesa zako mfukoni ili uweze kulitumia). Kifupi Gharama za Gari ziko juu zaidi wakati wa kulitumia kuliko hata wakati wa kulinunua!!

Kweli waanze na nyumba la sivyo kwa kipato chao hicho wakifikia muda wa kulipa karo ya Watoto wakati bado wanapanga watalikimbia jiji!
 
Ushauri Muhimu kabisa waanze na Nyumba kwa sababu:
1/Nyumba ni mali isiyohamishika hivyo ni dhamana muhimu mahali popote pale duniani iwe Mahakamani, Benki, Biashara, Maishani, Kazini nk.

2/Thamani ya Nyumba inakwenda inaongezeka kila siku(Hata siku wakitaka kuiuza wataiuza kwa thamani kubwa zaidi).

3/Watakuwa wameondoa gharama za kupanga na usumbufu wake(Watakuwa huru sana)

4/Nyumba ni Akiba ya kudumu maishani(Wataishi wao na vizazi vyao)

5/Nyumba ni kipimo cha Heshima, Hekima, Busara na Upeo kijamii, kifamilia, kimila, kiserikali nk.

6/Nyumba ni Mtaji wa Maisha(Hawatatoa tena pesa zao kila siku au kila Mwezi kulipia gharama za kuishi kwenye hiyo nyumba zaidi wanaweza kupata kipato zaidi kama sehemu ya hiyo nyumba watapangisha)

7/Nyumba inaweza kuwaletea vitu vingine vingi kama Gari kama watafanya mahesabu vizuri(Kwa mfano wanaweza kuitumia kama dhamana katika taasisi za kipesa kukopa pesa za kununulia gari nk.)

NOTE;
Kwanini wasianze na Gari:
A/Gari inahitaji gharama kubwa sana kulihudumia(Kwa mfano Insurance, Kodi ya Mapato, Mafuta ya kila siku, Service ya kila mara, Parking ya kila siku, Trafiki, Vipuri nk)

B/Gari itakuzidishia gharama zaidi za maisha pasipo msingi.(Mfumo wako wa maisha unaweza ukabadilika ili kukidhi tu fahari ya kumiliki gari. eg.Kula, kuvaa, Makazi, matembezi, Marafiki, Ndugu, Jamaa nk.) Hili jambo nimeliona kwa watu wengi sana mijini. Kifupi Gari halipatani sana na mbana matumizi!!!

C/Thamani ya Gari mara nyingi inakwenda ikipungua tokea ile siku unalimiki.

D/Gari ni chombo kinachochakaa kwa upesi sana kadri siku zinavyokwenda au unavyolitumia(Mara nyingi magari mengi yanakuwa yameanza kuchakaa vibaya baada ya miaka mitatu tu!!)

E/Gari lina tabia ya kukugeuza kuwa Mtumwa wake(Kwa mfano Wakati wote litakuhitaji kutoa pesa zako mfukoni ili uweze kulitumia). Kifupi Gharama za Gari ziko juu zaidi wakati wa kulitumia kuliko hata wakati wa kulinunua!!

bonge la ushauri aisee .. ila kila nikiangalia pembeni wacha niendelee kupanga nilitafute kwanza hilo gari siku nikiishiwa kodi ntalala ndani ya gari langu....
 
Mpwa wangu unajua Kwanini inatugharimu sana kuendesha magari? Kwasababu wengi tunanunua magari ambayo yameshacboka sana kiasi kwamba maintenance costs zake zinakua kubwa sana.

Bahati mbaya sana magari mengi yaingiayo hapa kwetu ni ya mtumba...

Kwa kipato cha hawa jamaa amini amini nakuambia wataishia kununua gari kama sio second hand basi third end...

Mimi natumia Duet kwasababu ninachohitaji ni usafiri tu kwa maana ya usafiri na sio show-off najikuta siumii kuiendesha na Kila service yake hunigharimu 45;000 au 50;000.....

Hizi ni service charges za kawaida ambazo najua ni zile zisizoepukika...(kubadili engine, brake na gear box oil)

Lakini kumbuka gari lina vitu vingine vidogo vidogo visivyotabirika...
 
jamaa navyomfahamu ni mtunzaji mnzuri tu wa fedha! kwa kipato chake mi nilimshaur mwaka wa kwanza anunue suzuki carry , awe na dereva asubuhi ampeleke kazini mda unaobak dereva autumie kufanya kaz ya uchukuz wa mizigo na jioni imfuate kazini, wakati huo kuanzia mwaka wa pili atafute kiwanja aanze ujenzi taratibu huku akiwa kajiongezea kitega uchumi na usafir (suzuki carry) ! akaniambia mkewe anataka wanunue saloon car kwa ajili ya familia yao!! wakati jamaa anataka waanze tu ujenzi eti hatak kuingia risk!
 
Kwa kipato hicho ni bora watafute kiwanja waanze ujenzi...

Kuwa na gari ni kweli sio anasa lakini matunzo ya gari ni makubwa na mwisho wa siku wanaweza wakajikuta wanaishia kwenye nyumba za kupanga...

Ushauri wangu utabadilika kama kuna vyanzo vingine vya mapato zaidi ya hivyo ulivyotaja...

Mtani, mimi naamini katika utulivu wa akili/nafsi, yes, gari ni gharama kulitunza (Mafuta na service), ila unaweza kulinunua kwa fedha kidogo ambayo huenda ni sawa na bei ya uwanja tu (Let say 8m), halafu kwa sasa Dar viwanja vipilvyo cheap vipo nje ya jiji, let say Kibaha, na huyo bhana tufanye anafanya kazi K/Koo, na mke Gongo la mboto, fikiria gharama za usimamizi, na kwa 8M huwezi jenga nyumba ikaisha na ikawa na hadhi ya hiyo nyumba waliyo panga kwa sasa. Kama ni mimi, ningenunua gari kwanza akili yangu itulie, then najibana bana ninue kiwanja hata kama baada ya miezi sita, then na lamba kamkopo hata ka 10M naanzia ujenzi,

Mateso mara mbili hapana (Nigombee dala dala, niishi kwenye pagale)

Ni mtazamo tu
 
Kuna rafiki yangu mimi kajenga nyumba ya kawaida vyumba viwili na sebule kwa milioni 12, 13 tu.

Kimsingi hiyo sio dream house yake lakini ni kajumba kazuri na kanawatosha yeye mkewe na mwanao.

Sehemu mojawapo ya funds ili ajenge ilibidi auze gari lake...
 
Gari ni rahisi sana kununua tatizo linakuja katika kulitunza kwa wastani gharama za kuendesha gari hazipungui millioni tisa kwa mwaka ikiwemo wastani wa mafuta ya shillingi 15,000 kila siku inayofanya kuwa 450,000 kwa mwezi na kwa mwaka 5,400,000/- achilia services zenye wastani wa 100,000/- kwa mwezi barabara zetu si unazijua! hivyo kuna 3,600,000/- bado gharama za pack mjini kila siku kama 600/- kupaki jioni 1000/- au mlinzi kuosha gari 2000/- kwa siku.
lakini lililo tamu zaidi ni mitoko ya hapa na pale mama atataka kila harusi mchange ili muende kutembelea familia na mengine zaidi.
ki ukweli nilipokuwa na gari sikuweza kuanza ujenzi ila mara baada ya kupata ajali na gari kuwa haifai kabisa ujenzi ukaanza tena. hivyo achana na gari kwanza wacha watu wakucheke lakini lazima ujue nini unataka

ujenzi ni rahisi sana unaweza kuamua kununua matofari au kufyatua inategemea
tenga kila wiki 60,000 kwa tofari moja shillingi 1000/- utapata matofari 60 kwa mwezi matofari 240 kwa miezi sita 1,440 ambayo haya yanaweza kukusaidia kufikisha nyumba kiunoni.
au nunua nifuko minne kila wiki kwa shilling 60000 itaongezeka kidogo kila mfuko tofari 35 kwa mifuko minne tofari 140 kwa mwezi tofari 560 kwa miezi sita 3660 zinatosha kwa kiasi kikubwa kujenga nyumba ya kawaida.
jipange kwa mpango uleule weka hela ya ujenzi baada ya kukusanya matofari kwa miezi sita na anza ujenzi

Mkuu chiwa mfuko 1 cement tofali 35?unataka kumtafutia mwenzio majanga.
 
Jamani kuwa na usafiri sio anasa, ukiwa na Gari itakusaidia sana kwenye supervision ya ujenzi Wako. Ukiiba kapesa kidogo kazini unapitia duka la ujenzi faster unaweka kwenye Gari yako huyooooo moja kwa moja kwenye site yako. ILA sielewi Kwanini watu wana misconceptions Hii ya kuwa na Gari. Huu ni mtazamo binafsi
Nilianza kua na kiwanja halafu ikafuata gari kabla ya kujenga. Gari ilinisaidia sana wakati wa ujenzi.
 
Back
Top Bottom