Nyendo
JF-Expert Member
- Jun 4, 2017
- 1,194
- 4,115
Kuna mtu kahamia jirani nyumba ya pili, ana wiki ya 3 tu tangu ahamie ila nishajutia ujio wake kwa tabia zake, sijui katoka wapi huyu mtu jamani natamani hata kuhama nimpishe maana kumhamisha siwezi.
Ana tabia nyeusi sana, hata sijui niziitaje maana anaongea lugha ya matusi sijapa kuona huyu Mama, anaongea kwa sauti kubwa kama anatangaza na anaongea kutwa nzima Kuanzia saa 11 anaanza kuongea na watoto wake na mume wake mbaya zaidi anaongea mambo ya ovyo mwanzo mwisho mpaka saa 5 usiku akilala ndio kunakuwa shwari.
Ana waita watoto majina ya matusi na kuwatukana matusi mazito ( We kifulani chako njoo hapa, hapo kinatajwa kuingo cha siri cha mtoto chochote) ambayo hata mimi naona aibu, kwa sauti anayotumia kuongea unasikia kila kitu hadi naamua kufungulia mziki ili kukwepa matusi yake.
Hali hiyo hata kwa mumewe pia Mfano leo kamwambia mumewe hivi wewe baba M una akili timamu kweli, unaenda kununua Kvant ndogo hujui nami nataka kunywa we K......m Ny zako, kalisha hayo map...u yako hapo badala ya kurudia nyingine, mume naye kajibu tusi zito pia mbaya zaidi watoto wao wapo.
Nawaza hao watoto wao watakuwa watu wa aina gani hapo baadaye au ndio watakuwa wanatukana matusi mazito zaidi ya wazazi maana watakuwa washayazoea mno, kwanza kutwa wanasikiliza kelele za Mama yao, maadili kwao ni fumbo hakuna msamiati huo kwenye hiyo familia, sijui wameokotana wapi wazazi hawa masikini wanawapa mzigo watoto kuwabebesha matusi kutwa kucha!
Napata huruma kwa hao majirani zake wanaochangia nyumba sijui wana hali gani, mimi niko nyumba ya pili nishakereka na ndio sikai sana nyumbani kwa siku chache kama wiki nimekaa nyumbani kwa dharura nimejutia ujio wao hao wanaoshinda nao wana hali gani, hiyo ni siri yao maana mimi si mtu wa kwenda kwa watu ivyo sijui japo nadhani watakuwa wanakerwa pia maana nyumba ile kabla ya huyu jamaa na mkewe ilikuwa imegubikwa na ukimya.
Sina budi kuhama kunusuru afya maadili ya familia yangu maana kwa sasa wanashiba matusi kuanzia saa 11 aljajiri mpaka saa 5 na kero ya sauti za mtu anaongea kama kafungwa spika za matangazo ya bishara zile za machinga.
Jirani huyu anapaswa kukaa mtaa wa peke yake au akae na watu wa kariba yake na si watu waliostaarabika. Ama hakika anachosha na kukera sana.
Ana tabia nyeusi sana, hata sijui niziitaje maana anaongea lugha ya matusi sijapa kuona huyu Mama, anaongea kwa sauti kubwa kama anatangaza na anaongea kutwa nzima Kuanzia saa 11 anaanza kuongea na watoto wake na mume wake mbaya zaidi anaongea mambo ya ovyo mwanzo mwisho mpaka saa 5 usiku akilala ndio kunakuwa shwari.
Ana waita watoto majina ya matusi na kuwatukana matusi mazito ( We kifulani chako njoo hapa, hapo kinatajwa kuingo cha siri cha mtoto chochote) ambayo hata mimi naona aibu, kwa sauti anayotumia kuongea unasikia kila kitu hadi naamua kufungulia mziki ili kukwepa matusi yake.
Hali hiyo hata kwa mumewe pia Mfano leo kamwambia mumewe hivi wewe baba M una akili timamu kweli, unaenda kununua Kvant ndogo hujui nami nataka kunywa we K......m Ny zako, kalisha hayo map...u yako hapo badala ya kurudia nyingine, mume naye kajibu tusi zito pia mbaya zaidi watoto wao wapo.
Nawaza hao watoto wao watakuwa watu wa aina gani hapo baadaye au ndio watakuwa wanatukana matusi mazito zaidi ya wazazi maana watakuwa washayazoea mno, kwanza kutwa wanasikiliza kelele za Mama yao, maadili kwao ni fumbo hakuna msamiati huo kwenye hiyo familia, sijui wameokotana wapi wazazi hawa masikini wanawapa mzigo watoto kuwabebesha matusi kutwa kucha!
Napata huruma kwa hao majirani zake wanaochangia nyumba sijui wana hali gani, mimi niko nyumba ya pili nishakereka na ndio sikai sana nyumbani kwa siku chache kama wiki nimekaa nyumbani kwa dharura nimejutia ujio wao hao wanaoshinda nao wana hali gani, hiyo ni siri yao maana mimi si mtu wa kwenda kwa watu ivyo sijui japo nadhani watakuwa wanakerwa pia maana nyumba ile kabla ya huyu jamaa na mkewe ilikuwa imegubikwa na ukimya.
Sina budi kuhama kunusuru afya maadili ya familia yangu maana kwa sasa wanashiba matusi kuanzia saa 11 aljajiri mpaka saa 5 na kero ya sauti za mtu anaongea kama kafungwa spika za matangazo ya bishara zile za machinga.
Jirani huyu anapaswa kukaa mtaa wa peke yake au akae na watu wa kariba yake na si watu waliostaarabika. Ama hakika anachosha na kukera sana.