Kuna vitu navidhania

Raia Fulani

JF-Expert Member
Mar 12, 2009
10,883
2,765
Yah, navidhania na sidhani kama ndio havijakuwepo. Vipo. Mfano;
1. Nimetokea tu kuwaza kwa nini watu wanakufa. Napata jibu kuwa hakuna kifo cha bahati mbaya. Unaweza pia kuepuka vifo. Vifo kwa maana majaribio ya uhai wako kukutoka sio mara moja. Pengine tungeoneshwa tungeshangaa.

2. Tunaishi maisha mengi sana. Wewe kuamka na kwenda uendako na kurudi ulipotoka, haitoshi kusema ni mfumo mmoja wa maisha. Nitajaribu kutengeneza filamu huko mbeleni kuonesha hili. Mfano, umeoa na mkazaa mtoto mmoja kisha ikatokea mizengwe mkaachana. Umetoka hapo ukaoa na kuendelea na maisha. Sasa picha inaanza pale ambapo ingekuwaje mngeendelea na mwanamke wa awali. Mifano ni mingi kwa kila nyanja

3. Nawaza kwamba sisi binadamu wapo ambao katika akili zao kuna milango fulani iko wazi, na hawa wanaona beyond. Kuna muda nakaa naona kabisa kuna kitu kama pazia kwenye ufahamu wangu linapaswa kusogezwa nione mbele zaidi kuna nini. Kuna kitu nawaza ila maelezo yake ni adimu sana.

4. Mwisho, nguvu za kiumbe zipo katika viungo/viungio vya mwili. Misuli inasaidia tu
 
Kwamba binadamu hawezi kujikuta. Unapochelewa katika jambo au mahali, ndio umechelewa hivyo. Huwezi kusema nitafidia kipande nilichopoteza kwa kuharakisha jambo au kuongeza kasi.

Mfano, mpo watatu mnatembea njiani. Wakati mnatembea, ukachepuka kujisaidia. Ulipomaliza ukaanza kukimbilia wenzio walio kama mita 50 mbele. Na hatimaye unawakuta na mnaendelea na mwendo

Sasa waza uko peke yako. Ukachepuka kujisaidia na kivuli chako kinaendelea na mwendo. Unapimaliza na kutaka kukiwahi, kwa mwendo utaakaoenda ni sawa na mwendo wa kivuli. Refer to archemedes principle
 
Tena nawawaza wanaowaza kuwa akili na silika ni kitu kimoja. Au vinafanana. Havina ufanani japo vinaishi aidha pamoja, au haviishi pamoja kabisa. Mtoto anapozaliwa na kufuata titi na kuanza kunyonya, hiyo ni silika. Mbwa anapoweza kufuata mafundisho ya bwana wake, hiyo ni silika. Binadamu naye ana silika pamoja na akili, japo anapozidi kukua, silika hutitia. Wapo wengine silika zao hukua sambamba na akili. Hiyo ni mbaya. Fikiria paka kwa mfano. Anapojisaidia huhakikisha anachimba shimo kisha hujisaidia. Amimaliza hufukia na kunusa kuona kama kafukia. Umwonapo utasema, hakika huyu kiumbe ana akili. Lah, hana akili. Paka huyu huyu siku chache mbele uyamkuta anafukua unga uliouanika na kujisaidia, kisha atafunika. Wako watu wa aina hiyo. Leo utasema huyu ni mtu. Kesho utajiuliza juu ya huyo mtu baada ya kumwona kivingine... "Jana nilisemaje?"
 
Yah, navidhania na sidhani kama ndio havijakuwepo. Vipo. Mfano;
1. Nimetokea tu kuwaza kwa nini watu wanakufa. Napata jibu kuwa hakuna kifo cha bahati mbaya. Unaweza pia kuepuka vifo. Vifo kwa maana majaribio ya uhai wako kukutoka sio mara moja. Pengine tungeoneshwa tungeshangaa.

2. Tunaishi maisha mengi sana. Wewe kuamka na kwenda uendako na kurudi ulipotoka, haitoshi kusema ni mfumo mmoja wa maisha. Nitajaribu kutengeneza filamu huko mbeleni kuonesha hili. Mfano, umeoa na mkazaa mtoto mmoja kisha ikatokea mizengwe mkaachana. Umetoka hapo ukaoa na kuendelea na maisha. Sasa picha inaanza pale ambapo ingekuwaje mngeendelea na mwanamke wa awali. Mifano ni mingi kwa kila nyanja

3. Nawaza kwamba sisi binadamu wapo ambao katika akili zao kuna milango fulani iko wazi, na hawa wanaona beyond. Kuna muda nakaa naona kabisa kuna kitu kama pazia kwenye ufahamu wangu linapaswa kusogezwa nione mbele zaidi kuna nini. Kuna kitu nawaza ila maelezo yake ni adimu sana.

4. Mwisho, nguvu za kiumbe zipo katika viungo/viungio vya mwili. Misuli inasaidia tu
Stimu zimeanza kupanda sasa
 
Kadhalika mafanikio ya mtu yapo mbele yake kabisa. Shida ni kwamba tunapuuzia viashiria. Kadhalika tunajenga hofu na huruma. Huruma imeangamiza wengi.
Umri wa kufanikiwa ni kuanzia miaka 25 hivi na kuendelea hadi 60 hivi. Katikati hapo wengi sana hutoka kwenye reli, na kurudi relini ni kudra tu za Mungu, na jitihada ya ziada. Wafundisheni wanenu kusimamia sauti za ndani. zinazowaita kwenda mwelekeo fulani

Tunashindwa kuvumilia kwa muda kuonekana "wehu" na watukutu ili sauti zetu za ndani na miito ituitayo ipate kudhihirika kwa wengine
 
Back
Top Bottom