Kuna uhusiano gani kati ya Lowassa na TBC?

Kuna uhusiano gani kati ya Lowassa na TBC?

Wakati tukielekea katika kumbukumbu ya kifo cha kipenzi cha watanzania wengi hayati Edward Moringe Sokoine naona mheshimiwa Lowasa yumo akimwelezea marehemu alivyokuwa

1. Kuna umuhimu wa Lowasa kuwemo? Hakuna viongozi wasafi wanaoweza kumsemea huyu mpendwa wetu?
2. Hilo tangazo nani analilipia? Kama ni serikali kwa nini atumie pesa ya walipa kodi kujisafisha?

Kwangu mi naona ni sawa na kuchanganya biskuti na matofali na kuweka ndani ya boksi.

Mbona Lowassa apewe nafasi ya kumsemea kiumbe wa watu ambaye hakuwahi kufikiria watanzania wanahitaji kuibiwa?

Kwanini TBC1 wanaonekana kumpa coverage kubwa Lowassa?
Lowassa ni mbuge wa jimbo alilokuwa Sokoine, ni mtu aliyewahi kuwa waziri mkuu, cheo alichokuwa nacho Sokoinne, ni mtu pia aliye kuwepo wakati wa Sokoinne...ni miongoni mwa watu wanaostahili kuwa katika kipindi hicho.

ASANTE
 
matawi, tukimchukia kiongozi, tumchukie kwa mabaya/ufisadi wake lakini tusiwe na chuki binafsi dhidi yake. Kwa vile EL kachafuka na uchafu wa Richmonduli, sasa ndio imekuwa nongwa?!. Asifanye chochote kwavile ni mchafu hivyo atachafua?!.

Japo mimi sio mtetezi wa EL, ukimuondoa Sokoine, hatujawahi kumpata waziri mkuu mwingine yoyote anayemkaribia hata kwa mbali, lakini kati ya wote, angalau angalau ni EL tuu, sasa ulitaka nani amzungumzie Moringe?!.

Mambo ya EL siku zote nasisitiza 'Mnyonge mnyongeni, lakini haki yake mpeni'!.
EL anamkaribia mpendwa wetu Edward Moringe Sokoine kwa lipi?
EL kafanya lipi la kuweza kumlinganisha na Shujaa Sokoine?
Kunyakua maeneo ya wazi Masaki? Kushirikiana na RA kuwanyang'anya Watanzania Container Terminal bandarini? Kujengesha Shule za Kata ambazo yeye mwenyewe hapeleki watoto wake? Unajua watoto wa Shujaa Sokoine walisoma shule zipi?
EL hastahili hata kusafisha viatu vya Shujaa Sokoine.
Tafadhali msitutukane Watanzania, tuna akili timamu
 
Naomba nisijibu hoja ya mtu yeyote. Lakini nasikitika ninaposoma hoja ya mtu ambaye umri wake jf ni mkubwa, akawa anatetea EL kumusemea Sokoine eti ana haki! Sawa ana haki hiyo lakini wewe msikilizaji ambaye ndo mulengwa wa habari hiyo, unaona kuna substance au logic? Huwezi kuwasemea na kuwasifu wana demokrasia kama wewe ni wa aina ya Mubarak wa misri.

Kama mtu uliye analytical lazima ujiulize why Lowasa?

Tunachofahamu ni kwamba Lowasa bado anawinda kuwa Rais na Tatizo lake kubwa analohangaika nalo ni media. Anawinda media imusifu, imuonyeshe. Mpaka sasa hivi bado hajafanikiwa na bahati mbaya sasa, Kuna kundi potential la wapiga kura ambao bado hawamkubali na hawaikubali CCM. Si umeona yanayowapata wana CCM vyuo Vikuu! Na bado mambo yanaelekea vijijini kwenye hizo div. zero walizotengeneza. By 2015 unaweza kukadiria idadi ya graduates watakaokuwa mtaani wakipambana na hoja au udhaifu wa CCM maana nina hakika hakuna jipya litakaozuka ktk kipindi hiki.
 
bora wangempa Fred Sumaye, huyu jamaa poa sana na anaweza kuwa successor mzuri tu wa JK ambaye ametuchakachua kwa kuwalea mafisadi.
 
Nimefuatilia jinsi TBC1 ilivyofanya kazi ya kuripoti vikao vya CC na baadaye NEC Dodoma na kugundua kwamba bado TBC1 wanafanya kazi kwa maelekezo/ushabiki wa Lowassa.

Kwanza kwa Dodoma na Dar es Salaam matukio makubwa hurushwa moja kwa moja na zaidi kama yanamhusisha Rais ama tukio lenye mvuto kwa jamii. Kwa vikao vya Dodoma na baada ya NEC kuruhusu waandishi wa habari na TBC1 kurekodi badala ya kurusha live inatia shaka.

Pili baada ya kurekodi, inasikitisha sana sisi tuliokuwamo katika hiyo Press Conference tumeshangazwa na TBC kukatiza alipoishia Chiligati na kutomtoa kabisa Nape alipokua akiwataja moja kwa moja kina Lowassa, Rostam na Chenge.

TBC1 fanyeni kazi, Lowassa hasafishiki na habebeki na hata kama akifanikiwa kuwa kiongozi endeleeni na kazi bila kujali, na kama munamjali Rais ajaye (kama akipata) na kumwacha Rais aliyepo.

Tulidhani baada ya kuondoka Tido itakua yameisha maana Tido alimhoji Pinda na kumpa Lowassa nafasi ya kumalizia ili amfunike, lakini na sasa munaendelea kuonyesha kwamba munaandamwa na kivuli cha Lowassa. Fanyeni kazi acheni unazi wa aibu hasa kwa mafisadi.
 
Nimefuatilia jinsi TBC1 ilivyofanya kazi ya kuripoti vikao vya CC na baadaye NEC Dodoma na kugundua kwamba bado TBC1 wanafanya kazi kwa maelekezo/ushabiki wa Lowassa.
TBC bado wako 1980 . Shirika gani tovuti yake inazidiwa hatana tovuti ya udaku kama global publisher.

Hawaweki hata clip za video au za audio. Utadhani ni tovuti ya daily news. what does TBC stand for.?
 
Nimefuatilia jinsi TBC1 ilivyofanya kazi ya kuripoti vikao vya CC na baadaye NEC Dodoma na kugundua kwamba bado TBC1 wanafanya kazi kwa maelekezo/ushabiki wa Lowassa.

Kwanza kwa Dodoma na Dar es Salaam matukio makubwa hurushwa moja kwa moja na zaidi kama yanamhusisha Rais ama tukio lenye mvuto kwa jamii. Kwa vikao vya Dodoma na baada ya NEC kuruhusu waandishi wa habari na TBC1 kurekodi badala ya kurusha live inatia shaka.

Pili baada ya kurekodi, inasikitisha sana sisi tuliokuwamo katika hiyo Press Conference tumeshangazwa na TBC kukatiza alipoishia Chiligati na kutomtoa kabisa Nape alipokua akiwataja moja kwa moja kina Lowassa, Rostam na Chenge.

TBC1 fanyeni kazi, Lowassa hasafishiki na habebeki na hata kama akifanikiwa kuwa kiongozi endeleeni na kazi bila kujali, na kama munamjali Rais ajaye (kama akipata) na kumwacha Rais aliyepo.

Tulidhani baada ya kuondoka Tido itakua yameisha maana Tido alimhoji Pinda na kumpa Lowassa nafasi ya kumalizia ili amfunike, lakini na sasa munaendelea kuonyesha kwamba munaandamwa na kivuli cha Lowassa. Fanyeni kazi acheni unazi wa aibu hasa kwa mafisadi.

Yote hayo ni hisia zako tu!! Kazi ipo!
 
sokoinebc%5B1%5D.jpg
439.png



Kwenye TBC1 kipindi cha kukumbuka siku ya leo (Sokoine), Lowassa amemsifia Sokoine na kusema alikua ni mchapakazi na aliwawajibisha wote waliokua hawafanyi kazi yao. Lowassa akaongezea kuwa katika ulimwengu wa sasa ni muhimu kuwa na viongozi wenye "quality" hizo, hasa hapa nchini ambapo viongozi hawana tabia za kujiwajibisha.

Akasema hakuwa mtu wakujilimbizia mali, alikua ana ng'ombe zake wakutosha familia yake. Alifanya kazi nzito hasa ukizingatia wakati ule, alipambana na walanguzi na wala rushwa. Amelinganisha kazi hiyo na alichofanya Kikwete kule Dodoma. Ingawa katika ulimwengu wa leo ufisadi na rushwa imekuwa vigumu sana kupambana navyo, lakini bado anawasifu TAKUKURU kwa kazi kubwa na nzuri wananoifanya!

Tumefata misingi yake kwenye uchumi, hasa kwenye shuguli za wafugaji (hasa Monduli) kwenye kupata maji na madawa ya mifugo.

Alisimamia elimu, shule zimeongezeka sana kutoka kipindi cha Sokoine mpaka leo.
 
Hajazungumzia "kujiwajibisha" kama mkuu wake alivyosema kama sehemu ya kumuenzi Sokoine?
 
pls ungeweza kuzitenganisha hizo picha?
EL hatakiwi kuzungumzia utendaji wa yeyote katika nchi hii kwa sasa.
 
mmmmh mbona kashindwa kujiwajibisha yeye mwenyewe huyu laiboni?Yeye si ndie kajilimbikizia hadi kufuru?:noidea::noidea::noidea:
 
Two different persons,I had the benefit of being led by him,the best PM.
 
hivi TBC ni shirika la umma ama ni kampuni ya mtu binafsi,maana huwa siielewi kabisaaaaaa,bola hata ITV najuwa ni ya mkurugrnzi mzee mengi ila TBC hata sijui nini kinaendlea
 
Pili baada ya kurekodi, inasikitisha sana sisi tuliokuwamo katika hiyo Press Conference tumeshangazwa na TBC kukatiza alipoishia Chiligati na kutomtoa kabisa Nape alipokua akiwataja moja kwa moja kina Lowassa, Rostam na Chenge.

Sasa mzee kama ulikuwemo kwenye hiyo Press Conference ulitakiwa uturushie hali halisi ilivyokuwa badala ya kuanza kulalamika! Weka Video Clip ili tupate habari kamili please!
 
That is the only thing he can do kwani kumuiga hawezi- as one said these are the extreme oppsite sides
 
TBC1 ndio mabingwa wa kuchakachua habari kwa sasa. Wamefikia hatua ya kushindwa hata kuripoti uhalisia wa tukio kwa vile wanaichakachua habari iwe na maana wanayotaka wao badala ya uhalisia wake. Wanazidi kuporomoka.
 
Back
Top Bottom