Braza Kede
JF-Expert Member
- Nov 1, 2012
- 1,679
- 3,328
Uchunguzi wangu huru umeonesha akinamama na mabinti walio wengi wamekuwa wapenzi wakuu wa kula viazi vya kukaanga vinavyochanganywa na mayai maarufu kwa jina la chips mayai.
Ukitaka kuhakikisha hili wewe ingia sehemu yoyote ya kula na uchungulie mezani vilivyoagizwa, utaona asilimia kubwa ya akinamama na mabinti ni chips mayai na wengine wanaongezea nyama choma au mishikaki na wengi wao unakuta hawapendi mboga za majani.
Lililo wazi ni kwamba watu hawa hawali chakula bora. Na kama hata huko majumbani kwao wanakula hivi basi kama taifa tuna janga kubwa kwa kizazi cha huko mbeleni maana hawa ndo mamazetu wa sasa au baadaye.
Sasa kwa ulaji huo tutakuwa na kizazi cha namna gani hapo baadae. Wizara ya Afya Tanzania angalieni jambo hili kabla hali haijawa mbaya.
Ukitaka kuhakikisha hili wewe ingia sehemu yoyote ya kula na uchungulie mezani vilivyoagizwa, utaona asilimia kubwa ya akinamama na mabinti ni chips mayai na wengine wanaongezea nyama choma au mishikaki na wengi wao unakuta hawapendi mboga za majani.
Lililo wazi ni kwamba watu hawa hawali chakula bora. Na kama hata huko majumbani kwao wanakula hivi basi kama taifa tuna janga kubwa kwa kizazi cha huko mbeleni maana hawa ndo mamazetu wa sasa au baadaye.
Sasa kwa ulaji huo tutakuwa na kizazi cha namna gani hapo baadae. Wizara ya Afya Tanzania angalieni jambo hili kabla hali haijawa mbaya.