Kuna muda unakata tamaa mpaka mwisho ila baadae unakuja kupata njia

Peril22

JF-Expert Member
Apr 15, 2020
1,422
2,313
Natumaini ni wazima wa afya ndugu zangu,

Apr 2016 zinatangazwa nafasi za jtk kwa kujitolea mjomba anauza ng'ombe mmoja kwa 600k anahonga unapata nafasi, unapangwa kikosi flan cha jkt. Unafika kikosini mnaambiwa as you where mrudi nyumbani mpaka pale itakapotangazwa tena.

Unarudi nyumbani unakutana na mradi wa madawati kwenye halmashauri yako ya wilaya unaomba kibarua unapiga kazi mpaka mwezi wa 10 bila malipo yoyote huku mkiambiwa pesa haijatoka ila mnapewa moyo kuwa pesa yenu italipwa soon. Inakubidi utafute plan B ya kuishi huku ukiendelea nakazi ya madawati.

Kama bahati waziri mwenye dhamana anatangaza wale waliosailiwa walipoti vikosini kuanzia tarehe 1/12 na mwisho wa kuriport ni tarehe 5/12 unakopa nauli tarehe moja upo kikosini. Mnapiga uzaledo kama kawa mwezi mzima mkilima kama vichaa, mnafanyiwa vipimo upya unapita fresh na kozi inaanza. Unamenyeka miezi sita migumu ila unatoboa pasi na shaka yoyote na unaapa na kuwa SM (Service Man).

Hapo ndipo kilimo kinapoanza cha kufa mtu kila siku watu wanne mnapewa heka moja mnailima na kuipanda, hayo yanakuwa ni maisha yako ya kila siku mpaka unakuwa unalala na jembe chini ya godoro saa tisa usiku upo shambani mpaka saa nane mchana unarudi kula unaenda kumwagilia bustan na unarudi na kuni. Maisha yanandelea mara inatangazwa kuna ujenzi wa ukuta wa mererani unapiganisha ili uepukane na kilimo unafanikiwa unakwenda kwenye ujenzi.

Huko ndo unakutana na balaa bora kile kilimo ulichokikimbia ila kwa uwezo wa Mungu unatoboa na ukuta unaisha wote mnaahidiwa ajira. Baada ya hapo unapelekwa ujenzi mwingine morogoro unaenda kumenyeka upya, ujenzi unaisha unahamishiwa ukonga unajenga kidogo mnapelekwa msata kwa ajiri ya kupiga kozi ya ajira (RTS).

Pale mnafanyiwa vipimo unaambiwa ni unfit na mnafukuza kama mbwa nyinyi mliokutwa unfit lakini unajitahidi kumtafuta yule daktari aliyewapima na kumuuliza tatizo lako. Anakueleza kiungwana kabisa kwamba una homa ya ini na kukupa ushauri jinsi ya kufanya ili uweze kuishi. Unaacha kuwaza ajira unaaza kulia kwa ajiri ya afya yako na uchumi wa mjomba unaukumbuka hiyo tayari ni 2019. Unarudi nyumbani mnyonge unalia kila siku, unakata tamaa ila mwisho unaamua kwenda hospitali kwa ajiri ya kuanza kupata matibabu ya gonjwa lako.

Unafika hospital unapimwa unaambiwa hauna ugonjwa huo, unawaeleza ushapima nyuma na kukutwa nao wanakupima mara kadhaa ila majibu yanakuwa vilevile. Unaondoka kwa mshangao, kesho unaenda hospitali nyingne ya private majibu ni yaleyale, unaishiwa nguvu, unaanza tena kuwaza ajira uliyoikosa kwa hila, hupati majibu kwanini ilikuwa vile unaamua kumwachia Mungu.

Mtaani kunakuwa kugumu kila unalojaribu halifanikiwi. Shirika mojawapo la umma linatangaza nafasi za kazi unajikuta una sifa walizotaja pale unatuma maombi, bahati nzuri unakuwa shortlisted kwa ajiri ya usaili. Unaenda kwenye usaili pale kwenye vipimo unamkuta daktari yuleyule wa msata, unakata tamaa ila hakuna namna unafanya vipimo majibu yanatoka hausomwi katika unfit unaendelea na usaili mpaka usaili wa mahojiano unafika mnafanya na kurudi kusubiri majibu. Baada ya muda unatumiwa email kuitwa kazini, hauamini, unafurahi sana na kumshukuru sana Mungu.

Ndugu zangu dunia hii kuna watu wenye nayo na sisi maskini tuna safari ndefu sana ya mafanikio.
 
Daa nimeanza kusoma paragraph za mwanzo nikiwa na tabasamu, bt kadri nilivyoendelea najikuta nalengwa na machoz. Vijana mpk kutoboa tunapitia mengi sna na katka hayo baadhi hutoboa na wengine huishia kwenye ufukara wa maisha.
Wapo wengine mpaka leo wapo mtaa tuliokutwa nao kwenye sakata hili tunafanya kubustiana kimbinu.
 
Mtu unatumikishwa kama mtumwa arafu unafukuzwa kama mbwa jkt ni njia moja apo ya kunyoonya watoto wa masikini na kufurahisha viongozi wa mradi. Pole sanaa kijana mimi nilikataa kwa ajiriwa kwa hizi ajira za kipumbavu eti ualimu ni wito nilifanya kazi mwezi sita tu.
 
Back
Top Bottom