Ungenisoma mstari kwa mstari ungegundua tayari swali lako lina jibu kwenye maelezo yangu!!!Kwanini alikuwa hapokei simu zake kama sio tapeli?
Ungenisoma mstari kwa mstari ungegundua tayari swali lako lina jibu kwenye maelezo yangu!!!Kwanini alikuwa hapokei simu zake kama sio tapeli?
Kama umewaamini hao ndugu zako kwa kuwa wanafanya nao biashara kwa nini usiwaite uwaelezee kilichotokea ili wakusaidie kukuchukulia pesa yako kwa huyo bwana unayemuita tapeli mara unasema unamwamini kwa vile alifanya biashara na ndugu zakoHuyu mtu anafanya biashara na watu ambao nawafahamu nakuna mmoja alitoka huko ndo akaniambia nenda ila nilikuwa nasafarisha songea
Nafikiri angekuwa anapokea simu na kutoa ushirikiano wa mwenendo mzima wa huo mzigo wala huu uzi usingekuwepo hapa.Ungenisoma mstari kwa mstari ungegundua tayari swali lako lina jibu kwenye maelezo yangu!!!
Inamaana ujasoma idadi ya walioharibika.Kuna 1385 na kuna 1835 ipi ni namba sahihi.. Unajua nyinyi wananchi mnaojiita wanyonge kumbe kweli kichwani wanyonge unafanya biashara kabla ya kujumlisha cost zingine tayari unahasara.. Biashara gani hii unapata 250,bora huyo jamaa akutapeli ili ujifunze
Sasa wewe,nakuonea huruma sana.Ushadi wa vibali na ushulu kwa sasa sina nimetafuta sana risti ya malipo ya mzigo ya serikali sijaiona pia niliamini biashara nimisha maliza hivyo kibali cha kusafirishia mzigo kilisha pita muda wake labda shaidi kipindi namuuzia alikuwepo
Utapeli hata ukiwa na phd unaweza tapeliwa kutokana na mazingira husikaDuh biashara za mazoea hizi! Unafanya biashara ya laki tisa unapata faida ya tshs 250 tu halafu ni graduate unafanya biashara ya bila mkataba na mtu kienyeji tu hivi.Mungu akusaidie!
Soma vizuri na akili yako ya mataga,Inamaana ujasoma idadi ya walioharibika.
Pole sana aisee....pole sana.chuo gani ulichosoma?,bora hata ungemshirikisha bi mkubwa angekupa uzoefu. Huu uandishi sio wa mtu aliyemaliza chuo.hapo hiyo hasara tayari,la msingi umejifunza kitu,hutarudia tena makosa,usikate tamaaa,endelea kupambana.Ushadi wa vibali na ushulu kwa sasa sina nimetafuta sana risti ya malipo ya mzigo ya serikali sijaiona pia niliamini biashara nimisha maliza hivyo kibali cha kusafirishia mzigo kilisha pita muda wake labda shaidi kipindi namuuzia alikuwepo
Wewe kweli si mfanyabiashara. Si ungekomaa nao uuuze hata kwa 350 rejareja? NA mzigo ungeisha haraka. Ungekuwa unakula samaki waliovunjika na kulala gesti isiyozidi 10,000 kwa siku.Mkuu haikuwa dhamira yangu kukopesha ila huyu nitapeli tu
duh biashara ya kuoza angefanyaje?Ila chikolombe umezingua sana kuchoma mtaji wote kwa mtu usiemfahamu, unaanzaje kukuposha tena kwa mara ya kwanza tu
Kweli Kabisa watu wa sokoni wana roho ngumu sanaWatu wa sokoni ni wauaji wanafanya biashara kwa hela yako na hasara ni juu yako.
mtafutie polisi laki mbili jokoe laki Tisa ikishindikana mtafute shehe italudi mkuuMimi ni kijana niliye maliza masomo yangu mwaka huu, kipindi nikiwa chuo nilikuwa najiwekea akiba kutoka kwenye boom langu ili nikimaliza basi niwe na mtaji ili nianze kufanya biashara, nimefanikisha kuwa namtaji .TZS.1000000/= tarehe 2.9.2020 nilienda wilaya ya simanjiro (manyara)kijiji cha kimotoroki kufata samaki aina ya kambale nili nunua samaki 2000 walio gharimu Tzs. 900000 hapo kuanzia manunuzi hadi kuwabanika kwa moto, niliwasafirisha hadi dodoma kwenye soko la chang'ombe ambapo niliwasiliana na boss ambaye alisema anachukua mzigo wote ananipa pesa yangu siku hiyo hiyo.
Tulifungua samaki akahesabu akapata samaki 1385 kati ya samaki 2000 kutokna na usafiri hao wengine walivunjika hivyo hawakuhesabiwa hiyo ilikuwa tarehe 18/9/2020 , kwa samaki 1835 ilitakiwa anipe TZS. 900250 ila aliomba pesa yangu atanitumia baada ya siku tatu,basi kiungwana nikakubali mimi nikaondoka nikijua pesa ata nitumia hadi sasa hajanitumia pesa na nikimtafuta simu hapokei Wala sms hajibu, Leo nimemtafuta kapokea kaniambia niende dodoma nikafate samaki wangu.
Baada ya kumsumbua sana kuhusu pesa yangu, naomba msaada wenu wa mawazo mimi ni mtoto wamvuvi tena mvuvi wa hali ya chini na mama anafanya uchuuzi wa samaki ila mala nyingi matapeli kama hawa wanatufanyia hivi tukipeleka mizigo sokoni