Chikolombe
Member
- Jul 23, 2020
- 36
- 69
Mimi ni kijana niliye maliza masomo yangu mwaka huu, kipindi nikiwa chuo nilikuwa najiwekea akiba kutoka kwenye boom langu ili nikimaliza basi niwe na mtaji ili nianze kufanya biashara, nimefanikisha kuwa namtaji .TZS.1000000/= tarehe 2.9.2020 nilienda wilaya ya Simanjiro (Manyara)kijiji cha Kimotoroki kufata samaki aina ya kambale nilinunua samaki 2000 waliogharimu Tzs. 900000 hapo kuanzia manunuzi hadi kuwabanika kwa moto, niliwasafirisha hadi Dodoma kwenye soko la Chang'ombe ambapo niliwasiliana na boss ambaye alisema anachukua mzigo wote ananipa pesa yangu siku hiyo hiyo.
Tulifungua samaki akahesabu akapata samaki 1385 kati ya samaki 2000 kutokana na usafiri hao wengine walivunjika hivyo hawakuhesabiwa hiyo ilikuwa tarehe 18/9/2020, kwa samaki 1835 ilitakiwa anipe TZS. 900250 ila aliomba pesa yangu atanitumia baada ya siku tatu, basi kiungwana nikakubali mimi nikaondoka nikijua pesa atanitumia, hadi sasa hajanitumia pesa na nikimtafuta simu hapokei Wala SMS hajibu, Leo nimemtafuta kapokea kaniambia niende Dodoma nikafate samaki wangu.
Baada ya kumsumbua sana kuhusu pesa yangu, naomba msaada wenu wa mawazo mimi ni mtoto wa mvuvi tena mvuvi wa hali ya chini na mama anafanya uchuuzi wa samaki ila mara nyingi matapeli kama hawa wanatufanyia hivi tukipeleka mizigo sokoni.
Tulifungua samaki akahesabu akapata samaki 1385 kati ya samaki 2000 kutokana na usafiri hao wengine walivunjika hivyo hawakuhesabiwa hiyo ilikuwa tarehe 18/9/2020, kwa samaki 1835 ilitakiwa anipe TZS. 900250 ila aliomba pesa yangu atanitumia baada ya siku tatu, basi kiungwana nikakubali mimi nikaondoka nikijua pesa atanitumia, hadi sasa hajanitumia pesa na nikimtafuta simu hapokei Wala SMS hajibu, Leo nimemtafuta kapokea kaniambia niende Dodoma nikafate samaki wangu.
Baada ya kumsumbua sana kuhusu pesa yangu, naomba msaada wenu wa mawazo mimi ni mtoto wa mvuvi tena mvuvi wa hali ya chini na mama anafanya uchuuzi wa samaki ila mara nyingi matapeli kama hawa wanatufanyia hivi tukipeleka mizigo sokoni.