Sema hili tukio limenikumbusha zamani sana enzi hizo najifanya eti hustler wakati nilikuwa katoto kadogo tu ambako ndo kwanza nimemaliza Form IV!!!
Hiyo siku nimepeleka mzigo, tena siku ya kwanza kama ilivyo kwa Likolombe... nikakutana na dalali ambae ni mlemavu wa miguu!!!
Jamaa alikuwa hawezi kusogea hata hatua moja bila kutumia magongo... labda asote!!
Basi bhana, nikamwachia mzigo! Huku na kule, siku ya kwanza, ya pili, ya tatu, dalali sound kibao! Alipoona mambo magumu, jamaa akala kona... akapotea kabisa sokoni!
Kila ninayemwuliza anakoishi, raia wanajifanya hawajui!!
Nilichofanya ni "kupotea" pale sokoni lakini kimsingi nilikuwa around nikimlia timing!! Sijui jamaa alikuwa anatuma wapambe waje kuangalia kama nipo au sipo, only God knows! Siku ya tatu, jamaa akatokea!!
From nowhere nikamwibukia, na kabla hajafahmu what's going on, nikayapora magongo yake na kumwambia hadi alipe pesa ndo namrudishia!!
Watu wa sokoni wajinga sana!!! Badala ya kumhurumia mwenzao, shangwe ambalo liliibuka pale halikuwa la nchi hii!!! Ungesema Tundu Lissu katangazwa rais!!!
Anyway, it's in those good old days!!
Chikolombe, hao wanaokuambia ulimwamini vp huyo jamaa inaonesha hawajawahi kuuza hata pipi ndo maana hawafahamu ulichokifanya ni kitu cha kawaida sana kwenye masoko yetu!
Sijui uliyemwachia ni mtu wa aina gani, manake kwa kawaida wanaochukua mizigo kwa staili hiyo ni madalali, ingawaje pia kunakuwa na wachuuzi ambao nao uchukua mizigo kwa mali kauli kwa kutarajia atakulipa akishauza!!
Ningeshauri rudi sokoni uangalie uhalisia lakini usimwambie kwamba unaenda! Kama ulimwachia dalali, kama mzigo hujauzika ina maana utaukuta umemdodea! Na ukikuta mazingira kama hayo, mwombe akutafutie bao fasta upige mwenyewe reja reja kabla hawajaharibika beyond selling quality!!
Usilete ujuaji wa kutaka lazima akulipe pesa yako wakati unachotakiwa kufanya hivi sasa ni kuhakikisha mtaji wako hauzami!!!
Kama ulimwavchia mchuuzi, ongea nae kama mzazi/bro ili msaidiane kuhakikisha mzigo unaisha!! Achana na simulizi za uchumi wa kati, hii nchi bado ni maskini sana!!! Huyo jamaa asipoweza kuuza huo mzigo kwa wakati basi uwezekano wa kukulipa utakuwa mdogo au utalipwa kwa mafungu kwa muda mrefu jambo ambalo ni threat kwa mtaji wako!!!
Kama mzigo bado mwingi, assuming Dom kuna masoko mengine, basi mwambie uchukue kidogo kidogo, kama vile debe moja kupeleka kwenye masoko mengine!
NARUDIA, usilete mambo ya kisomi wakati hata mkataba hamkuandikishiana... unachotakiwa kufanya hivi sasa ni kuhakikisha mzigo unauzika kwa haraka at that cost price ili kuulinda mtaji ili kuulinda mtaji!!
SHIRIKIANA na huyo mtu kuhakikisha mzigo unauzika!!!