Kuna mtu anataka kunitapeli naomba msaada

Kuna mtu anataka kunitapeli naomba msaada

Biashara hizi za sokoni mala nyingi unaweza fanya biashara na mtu ambaye humjui kwa sura ila mizigo anapokea ana uza na pesa anakutumia pia unakuta kuna mmoja ndo anamfahamu huyo mtu ndo anaweza kukuunganisha na wewe ukatuma mzigo akaupokea na akukutumia pesa yako ila utapeli upo!!! Pia kuhusu hili haki yangu nitapata tu tena yote mimi ni mtu mzima sina hofu nimetoa humu ili nipate mawazo tofauti tofauti pia hata funzo kwa wengine kama vijana wezangu n.k
Pole sana kaka.
 
Pole sana kijana...Fanya ukatoe taarifaa polisi haraka inavyowezekana..
Polisi ipi? Madalali wanakuambia mdaiwa hafungwi aje na nauli ya kurudia akiona anazungushwa atafute Uongozi wa soko awaeleze akiona hakuna msaada arudi akaanze moja Ila visimchanganye sana yeye si wa kwanza kutapeliwa, na akifanikiwa ashukuru Mungu.
 
Kuna kitu mnakoseaga, biashara be front it was too early for u to trust someone hizo siku 3 ungetafuta lodge ya bei rahisi ukapembejea hela yako! Uaminifu hakuna sikuhizi trade with caution!
 
safi sana ila pole, nadhani sasa umejifunza, next time hutapigwa kijinga ivyo
mjinga wakati wa kwenda, kurudi unakua mjanja, vuta soksi juu, pambana
 
Mimi ni kijana niliye maliza masomo yangu mwaka huu, kipindi nikiwa chuo nilikuwa najiwekea akiba kutoka kwenye boom langu ili nikimaliza basi niwe na mtaji ili nianze kufanya biashara, nimefanikisha kuwa namtaji .TZS.1000000/= tarehe 2.9.2020 nilienda wilaya ya Simanjiro (Manyara)kijiji cha Kimotoroki kufata samaki aina ya kambale nilinunua samaki 2000 walio gharimu Tzs. 900000 hapo kuanzia manunuzi hadi kuwabanika kwa moto, niliwasafirisha hadi Dodoma kwenye soko la Chang'ombe ambapo niliwasiliana na boss ambaye alisema anachukua mzigo wote ananipa pesa yangu siku hiyo hiyo.

Tulifungua samaki akahesabu akapata samaki 1385 kati ya samaki 2000 kutokna na usafiri hao wengine walivunjika hivyo hawakuhesabiwa hiyo ilikuwa tarehe 18/9/2020 , kwa samaki 1835 ilitakiwa anipe TZS. 900250 ila aliomba pesa yangu atanitumia baada ya siku tatu,basi kiungwana nikakubali mimi nikaondoka nikijua pesa ata nitumia hadi sasa hajanitumia pesa na nikimtafuta simu hapokei Wala sms hajibu, Leo nimemtafuta kapokea kaniambia niende Dodoma nikafate samaki wangu.

Baada ya kumsumbua sana kuhusu pesa yangu, naomba msaada wenu wa mawazo mimi ni mtoto wa mvuvi tena mvuvi wa hali ya chini na mama anafanya uchuuzi wa samaki ila mara nyingi matapeli kama hawa wanatufanyia hivi tukipeleka mizigo sokoni
Du... pole mkuu
Umesha kutana na kambale la utapeli.
Biashara ni mkono kwa mkono.
 
Hahahahah imagine umeshusha Fuso ya mzigo halafu baada ya siku 3 dalali analeta usenge. Hio shangazi yangu alishapigwa 16M akatoka from hero to zero. Na alikuwa mzoefu kwenye game wenzake wakapigwa 300M walifanyia biashara Zambia.

Alikuwa anazungusha mtaji wa 20M hapo bado ana marejesho ilifikia stage wanataka kuuza nyumba yake alidata almanusura tumkose. Kaka zake ndio kumpiga piga tuff akakaa sawa.

Hizo biashara za sokoni acheni tu😎 zina michezo ya hatari sana.
Kwanza biashara za kuuza jumla sokoni kama unaumwa BP, usifanye kabisa!!! Unaambiwa binafsi nililipwa pesa yangu baada ya mlemavu dalali kumpora magongo yake aliyokuwa anatumia kutembelea, sasa ikawa hawezi kwenda popote!!

Nilifanya huo uhuni baada ya kunipiga kalenda kwa siku kama 3, na alipoona nimemkalia kooni, jamaa akapotea sokoni, nami kwa kujua atakuwa anakuja kuchungulia kama nipo au hapana, nikawa najibana mahali namlia timing!

Ambacho hakujua ni kwamba chige mwenyewe ni mtoto wa Uswahilini, vurugu zote kafanya kabla hajagusa 20!!!
 
Faida ni shilingi za kitanzania 250 au nimesoma vibaya!?

Wewe ni msomi kweli!?
 
umesema anataka kukutapepli mbona kwa uzoefu inaonekana kashakutapeli.
 
(don't put all your eggs in one bucket) na usiwaamini watu ktk biashara...apo ungechukua ata laki 4 ufanye hyo biashara,nyengine (laki 2) ungewekeza Kwenye kuuza ata pipi na karanga... nyengine (laki 2) ungeiweka bank kama akiba itakayo baki ndo pocket money kilinda mfuko na tumbo.
"Put all eggs in one bucket and watch it closely"
 
Nyote nyinyi inaonesha hamjawahi kuuza hata pipi kwahiyo nyamazeni kwa sababu hakuna mnachojua!!

Alichofanya dogo kwa kiasi kikubwa ndicho kinachofanyika, kwahiyo acheni kumkejeli wakati hamjui lolote!! BIashara za aina hii zinaenda kwa "mali kauli"!
Acha hizo, mali kauli na tapeli?
 
Biashara gani ya kukopesha halafu unapata faida ya 250/=
Chifu,

Siku ukifanya biashara ya perishable goods ndipo utafahamu sio tu unaweza kukopesha na kupata faida ya Sh. 250 bali pia unaweza kukopesha kwa makubaliano ya kulipwa NUSU tu ya gharama zote ulizotumia!!

Na usisahau, amesema ni biashara ya samaki, tena wa kubanika kwa moto! And out of 2000 fishes, zaidi ya samaki 600 walikuwa wamevunjika!!!!

Sasa jiulize hata wewe mwenyewe: Je, ukienda sokoni kununua samaki wa mboga unaweza kununua samaki waliokatika?!

Ninachojaribu kusema kwa hilo swali hapo ni kwamba, samaki waliokatika wanauzwa kwa bei ya hasara kwa sababu, pamoja na kukatika, wengine miongoni mwao wanakuwa wamevurugika!!!

It's all about packaging and transportation problems!!!
 
Back
Top Bottom