Kuna mKenya kaniuliza swali hapa naomba mnisaidie kujibu

Kuna mKenya kaniuliza swali hapa naomba mnisaidie kujibu

Username 20

JF-Expert Member
Joined
Sep 21, 2017
Posts
741
Reaction score
1,513
Baada ya kukamtwa na kurudishwa kwa baadhi ya wanaharakati wa Kenya na baadhi yao kuripotiwa kuteswa na kutupwa mipakani (Tanga na Kagera)

Kisha kauli ya Rais kuwa hatakubali chokochoko, na kuwa katiba yetu haiingiliwi na mtu, jamaa kanikomalia kuwa ni kweli nchi yoyote ile duniani ina taratibu zake na mtu hata kama akiwa ni raia wa kigeni akivunja utaratibu waliojiwekea nchi husika lazima sheria za nchi husika zifanye kazi

Sasa swali lake likawa ni kwamba hao wanaharakati wamevunja sheria gani ya nchi yetu mpaka kupata dhahama hiyo? Naomba mnisaidie kujibu nimjibu huyu mKenya
 
Ni haki ya nchi husika kuzuia raia wa kigeni asiingie nchini kwake kwasababu zozote za kiusalama hata ikiwa ni kuwatilia mashaka.

Kwahiyo kurudishwa kwao hamna sehemu sheria imevunjwa wala wao hawana haki ya kudai juu ya kuingia Tz.
 
mwambie na yeye aje tanzania halafu afanye kama walivyofanya hao wanaharakati kutoka kenya atajulishwa kwa vitendo sheria atakayoivunja au kwa lugha nyingine mwambie 'usiandikie mate wakati wino upo'.
 
Ukiwa na visa ya nchi yoyote, ambayo kwa nchi za wazungu tunalipia, bado afisa uhamiaji anao uwezo wa kukukatalia kuingia nchini mwao kama hakuridhika na maelezo yako. Hapo tayari milioni tatu nauli imetumika.

Kuwatesa ni ngumu kufahamu mantiki yake.
 
Mjibu hakuna sheria iliyovunjwa ila nchini kwetu ni kosa kutetea haki hebu tujiulize TAL amefanya kosa gani?
 
Back
Top Bottom