Kuna kitu hakipo sawa makanisani, ni muda wa wakristo kuamka na kuhoji

Enyi vijana mtoleeni Mungu siku za ujana wenu wakati bado mna nguvu kabla uzee haujawafika. Kuna manufaa mengi mimi binafsi nimeyapata kwenye maisha yangu.
 
Unaendaje kanisani na buku 5 mkuu? Wakati baa mnaingia na laki beba kuanzia hamsini ukiona unahoji mambo ya sadaka jua umekufa kiroho toa ulichonacho huna tulia Mungu anakuona matumiz ya sadaka hayatuhusu imarisha uhusiano wako na Mungu kwa kutoa
Ttz sio kutoa au kubeba tatizo unapanga sadaka
 
nimechangua ujenzi wa kanisa la fatima geita na kweli mpka naama nimeona kanisa zuri limesimama, hata kama jamaa wamekula ila kiukweli kazi imefanyika…

Kristu…..!!!
 
Wakati unatusifia Waislamu, sisi huku wenyewe tunatamani tungekuwa na moyo wa kutoa sadaka kama wenu.

Sisi ni changamoto watu wazito kutoa sadaka, madrasa na misikiti mingi inahitaji ukarabati na shule pia. Ila watu wetu wazito mno wa kutoa sadaka. Sadaka mpaka zitokee kwa waarabu ndio madrasa zijengwe
Ndg. Nasri; Hata ss Wakristo mwanzoni ilikuwa hivyo i.e. Tulipokea misaada ya Kifedha na Mali kutoka Ulaya lakini kadri muda ulivyokwenda ndio tuko hapa sasa.
Huenda na nyie mkawa mnapitia njia hiyo. Kwa hiyo kwa maoni yangu kinachatakiwa huko kwenu ni kutoa Elimu na Hamasa kwa watu wenu kuhusu umuhimu wa kutoa Sadaka na mwisho msisahau Kushukuru hata kwa kile kidogo kinachopatikana.
 
isingekuwa hofu ya kifo,jehanamu na kutokuzikwa na kanisa,watu wengi wangeshazipiga chini hizi dini
Mh ingekuwa hivyo basi pia wachamungu wa kweli wangekuwa wengi lakini tunaona watu wanadini ila bado wanafanya na mambo yenye kusababisha kwenda motoni.

Hilo unalizungumziaje?
 
Siku moja nimemtembelea mzee wangu nilipofika akaniambia anadaiwa elfu hamsini kanisani kwa ajili ya harambee.Akanieleza kuwa kila jumuiya imepangiwa kiasi flani cha fedha ambazo zimegawanywa kwa kila nyumba.Mzee wang anakaribia miaka 80..Na alinieleza kuwa siku ya harambee kila familia wanakuwa wanasomwa kanisani mnapita mbele kwenda kukabidhi hicho kiasi cha fedha na kama huna lazima utoe sababu za maana hapo na linakuwa deni mpaka ulilipe. Mambo yamekuwa magumu mno siku hizi.
Pole sana
 
Huu uzi walitakiwa waulete wao kupima kina cha maji na mwelekeo wa upepo, maana vipofu wameshashtuka, kuna mijitu imekula nao ikawagusa mikono
 
Ulishawahi kuona post zangu kuhusu kulilalamikia Kanisa Katoliki juu ya taratibu zake??.Mimi ni Mkristo Mkatoliki niliyekomaa kweli kweli,kisiki Cha mpingu kitoke nyuma.
Kama hujui mimi nilikuwq mnistrant mpiga chetezo ila hawa RC wamekuwa wazinguzi sana wahitaji unachanga tena na wakati sadaka ya pili ilikuwa ni kwenda kuwaona wahitaji in short hawa ma padre nao wamestuka wana familia tunalisha familia zao
 
Ukishaingia mfumo wa jumuia lazima utowe pesa ya kuwa mkatoliki kila mwezi.

Pili harambee za kipuuzi na sadaka nyingi kwenye ibada inaondoa system ya kikatoliki ambayo tulizoea ibada ya misa ya jumapili ni lisaa limoja na nusu tu na ikizidi kwa special case ni masaa mawili tu, sasa kwa huu upumbavu ulioanza ibada inakwenda mpaka masaa matatu, misa ya kwanza mnaingia saa 12 asubuhi mnatoka saa mbili na kitu.
Hiyo pesa ya kuwa mkatoliki ndo naiyona leo. Sijui itakua parokia gani hiyo. Kuhusu michango kwa uzoefu wangu mdogo nilionao. Ni hivi mfano mimi kabla sijahamia kwangu parokia mbili zote nilizowai sali zilikua hazina michango mingi kwakweli. Sasa kimbembe huku nilikojamia ndo kwanza tunajenga kanisa, aisee kuna michango jamani. Ila hii michango mimi huwa hainipi tabu kwasababu natoa nilichojaliwa .
 
Mh ingekuwa hivyo basi pia wachamungu wa kweli wangekuwa wengi lakini tunaona watu wanadini ila bado wanafanya na mambo yenye kusababisha kwenda motoni.

Hilo unalizungumziaje?
Uwepo na wachamungu wengi hakutokani na Hofu ya Kifo,Jehanum au kutokuzikwa na kanisa bali ni kutokana na watu walioamini na kuiishi Imani yao kwa vitendo. Kwa kifupi ni kwamba Kifo ni LAZIMA uwe ni mcha Mungu au asiye mcha Mungu. Jehanum ipo tu haijalishi ww ni mcha Mungu au la. La msingi ni Je, ww umejiandaa kwenda sehemu gani? i.e Matendo yako yanakuelekeza au Umechagua kwa hiari yako kwenda wapi? Mbinguni au Jehanum? Kuwa na Dini sio Tiketi Kigezo cha kwenda mbinguni. Kuzikwa na kanisa hakumfanyi mtu aende mbinguni. Kwa mantiki hiyo wapo watu (Roho zao) watakaohesabiwa Haki (watakaokwenda mbinguni) kutokana na matendo yao mema waliyotenda katika kipindi cha Uhai wao hapa Duniani na wapo watu (Roho zao) watakaohukumiwa kuingia Jehanum kutokana na matendo waliyotenda.
Kwa hiyo mtu asijifurahishe au asijiridhishe eti mm nimebatizwa nitaenda mbinguni wakati anafanya kwa makusudi matendo ya dhambi/anamuasi Mungu kwa matendo yake.
 
Kanisa katoliki lazima lijitathimini, kila siku maswali yanaibuka dhidi yake.

Kuna kitu hakiko sawa.
 
Back
Top Bottom