Wahindi waliojenga reli sio hawa Matajiri wa Tanzania. Kama hufahamu waziri mkuu wa Sultani Karne ya 19 aliitwa Tharia topan alikua ni Ismailia toka Gujarati India, Sultan alikua Hana ukwasi kama hawa wahindi, aliwapa mazingira mazuri ya Biashara ili wahamie Znz wakati huo.
Sultani aliponunua kijiji cha uvuvi hapa Dar akawaweka hao wahindi, kina Aga khan wakaitwa ndio wakaijenga Dar, Aga khan alikua na pesa Sana yeye akafanywa ndio msimamizi wa Mali zote wakati huo.
Hawa wahindi wote walikua na Root moja wakagawanyika, Ismailia na mabohora, hawa Ismailia kiongozi wao zilienda Sana na Nyerere wakapewa vyeo vikubwa Sana serikali ya Nyerere na mpaka Leo wengi Wana vyeo nyeti na ni wasomi wakubwa. Diamond jubilee ni alama Yao kubwa na chai aliyonipa Mzee wangu ni kwamba walipofungua Hilo Jengo walidonate almasi nyingi Sana kwa Nyerere.
Upande wa pili mabohora hazikuenda na Nyerere, hawa jamaa hela zao huwa wanampelekea shehe wao Quba, kulizuka ugomvi mkubwa baina Yao na Nyerere na baadhi ya Mabohora kuwasaliti wenzao.
Pia waajemi Wana predate Waarabu na Asilimia kubwa ya wabantu hapa pwani, watu pekee ambao ni wa Mwanzo kabla ya wa Ajemi ni kushite tribes kama warangi, wairaqw etc kuna studies siku hizi zinaonesha makabila ya pwani kama wamakonde, Wazaramo etc DNA zao mpaka Asilimia 50 ni za ki Ajemi, waajemi wamekuja zaidi ya miaka 1000 iliopita na waarabu kama miaka 500 iliopita.