Kuna Dalili ya Serikali Kufilisika

Kuna Dalili ya Serikali Kufilisika

Ni anguko kubwa sana hili, lakini huwezi kusikia Serikali hii yenye usiri mkubwa ikitia neno.
Ikifika mwisho wataongea tu, na kila mtu atajua. Nakuambia huwezi ukafucha moto, moshi utakuumbua.
 
Mwafaa! Hapa ni kazi tu!!! Acheni maneno, serikali zilizopita zilikuwa za kubebana bebana, sisi tuna'rara' nao 'mbere'
 
Tatizo Mkuu ni huyu mtu mmoja ambaye kawajaza woga watendaji wake kiasi cha kushindwa kumwambia kwamba anakoipeleka nchi siko. Hivi baraza lote la Mawaziri likiamua kumvaa huyu dikteta uchwara kwamba nchi inayumba awasikilize washauri wake na aachane na udikteta atafukuza wangapi!? Hivi wastaafu Mawaziri Wakuu na Marais wakijipanga kwenda kuongea naye Ikulu kuhusu nchi kwenda mrama atawafanya nini!?

Kwanini mtu mmoja aachiwe kuiyumbusha nchi kiasi hiki na wale walio karibu yake waamue kukaa kimya kwa kumuogopa!?
Ulikua na wazo jema,ila mihemko yako imeharibu kila kitu.
 
Ni kweli kuna pesa nyingi inatumika kwa ajili ya kumlinda Daud Bashite Mfano jana kamati ya wabunge Dodoma wamepewa pesa nyingi sana, Hosptal hazina dawa viwanda hakuna lakini pesa ya kumlinda Bashite Daudi ipo nyingi sana.
Hebu weka ushahidi vile malipo yamefanyika au ni story za kwenye vijiwe vya kahawa
 
e1c838eed5d5bc3ba55b861bbf8e5924.jpg
pesa iliyotolewa kwenye bajeti ya wizara ya kilimo ni kituko.
 
Ni wakati wa Waziri wa Fedha kujipima kama anafaa kuendelea kushika nafasi hiyo. Kuna mawili ama hajui analolifanya ama hamwambii ukweli Mkuu.
Haijawahi kutokea kwa muda wa miaka miwili tuwe na Kamishna Mkuu wa mapato watatu hiyo ni dalili tosha hali si nzuri wizara ya fedha. Kuna msemo unasema you can lie sometimes but you can not lie always. Watanzania wanataka huduma muhimu kama maji na afya sio leo tume ya faru john ambapo serikali imetumia milioni 700 ama tume ya madini ambayo mamilioni kutumika.
We are tired of these episodes.
 
Hata Kahama tatizo ni lile lile ingawa tunalipa bili zetu vizuri tu.Najiuliza tatizo ni serikali ama nani?Ina maana hizi bili za maji tunazolipa zinaenda Benki kuu?Mimi nawalaumu Kashwasa kwani wanachukua pesa,halafu wao wanakwepa kulipia umeme
Nimechukizwa sana na meneja Rugemalila yaani watu tunalipa bill effective kila tunakosa maji kisa deni LA umeme
 
Tatizo Mkuu ni huyu mtu mmoja ambaye kawajaza woga watendaji wake kiasi cha kushindwa kumwambia kwamba anakoipeleka nchi siko. Hivi baraza lote la Mawaziri likiamua kumvaa huyu dikteta uchwara kwamba nchi inayumba awasikilize washauri wake na aachane na udikteta atafukuza wangapi!? Hivi wastaafu Mawaziri Wakuu na Marais wakijipanga kwenda kuongea naye Ikulu kuhusu nchi kwenda mrama atawafanya nini!?

Kwanini mtu mmoja aachiwe kuiyumbusha nchi kiasi hiki na wale walio karibu yake waamue kukaa kimya kwa kumuogopa!?
Uzuri au tatizo ni kuwa hao unaowaita watu wa karibu yake hawaguswi kabisa na mtikisiko huu uliopo
 
Back
Top Bottom