Kumuua mtoto wako

Kumuua mtoto wako

Power to the People

JF-Expert Member
Joined
Jul 11, 2007
Posts
1,198
Reaction score
900
Jana, mume wa rafiki yangu amemuua mtoto wake bila kukusudia akiwa anageuza gari lake atoke kweda kazini. Sipati picha maumivu walio nayo wazazi hasa baba wa mtoto kwa kusababisha kifo cha mwanaye. Nina hakika siwezi kuufikiria wala kuelezea uchungu walio nao sasa hivi.

Ajali nyingi za watoto hutokea nyumbani kwa sababu muda mwingi watoto hawa huwa nyumbani. Sisi kama wazazi tuna jukumu kubwa sana kuhakikisha nyumba zetu ni salama kwa ajili ya watoto wetu. Hebu chunguza nyumba yako, kama iko salama ili kujiepusha na machungu yatokanayo na kusababisha kifo cha watoto wetu wa kuwazaa. Angalia jikoni, bafuni, nje ya nyumba, unahifadhi vipi ndoo za maji, unahifadhi vipi vifaa na kemikali za usafi, drawers zina stoppers au hufunguka mpaka mwisho, socket za umeme zimekaa vizuri au zimelegea. Mambo ya kuangalia ni mengi sana.

Tukumbushane hapa mikakati ya kuchukua kuwaepusha watoto wetu na ajali na vifo vinavyoweza kuzuilika.
 
Mhhhhh! Hii inatisha sana, pole zao nyingi sana. Inabidi wazazi kuwa waangalifu mno na magari majumbani kwao maana ajali kama hizi zinatokea sana majumbani.
 
Kuna mambo ni kumwomba Mungu, yasikutokee. Will be indelible self blame for there whole life...

Kama unavyoshauri risk assessment and hazard identification ni muhimu sana kwa kila unachokusudia kufanya.

R.I.P little kid. Pole kwa wazazi.
 
Unapomuogesha mtoto mdogo kwa mfano kwenye beseni au bathtub usithubutu kumuacha mwenyewe hata dakika chache maana anaweza akaanguka na maji ya kwenye beseni/bathtub kama ni mengi yanaweza kusababisha kifo chake.
 
Unapomuogesha mtoto mdogo kwa mfano kwenye beseni au bathtub usithubutu kumuacha mwenyewe hata dakika chache maana anaweza akaanguka na maji ya kwenye beseni/bathtub kama ni mengi yanaweza kusababisha kifo chake.

Dakika moja kugeuka kuchukua towel inaweza kusababisha maafa makubwa. Janga lingine ni ndoo za maji, watoto wengi sana wamepoteza maisha kwa kutumbukia kwenye ndoo za maji zinazohifadhiwa majumbani kwetu.

Always tunashauriwa tujue mtoto yuko wapi na anafanya nini wakati wote. Ni muhimu sana the price to pay is too high.
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Ni kuomba Mungu tu hizo ni ajali siku ikishafika huwezi kuiepuka,mimi mke wa jirani yangu aliwahi kumkanyaga kichwa mwanae wakati anenda kazini asubuhi,ameagana nae ndani vizuri ghafla mtoto akawa ametoweka,kumbe kakimbilia nyuma ya gari kajificha karibu kabisa na tairi la nyuma,mama anarudisha gari nyuma kamponda kichwa mwanae na mchezo ukaishia hapo.
 
Unapomlaza mtoto mdogo kitandani hakikisha hakuna nguo au pillows hapo karibu kwa sababu anaweza kujifuna nazo na akakosa hewa ikawa majanga.Hii imenitokea jana tu,nilitoka kwenda hosp nina sindano za masaa niliporudi sikumkuta maid,mtoto wangu wa miezi minne alikuwa kitandani kalia mpaka sauti imemkwama na alikuwa kavuta blanket yake kajifunika usoni.Karibu nizimie.
 
Unapomlaza mtoto mdogo kitandani hakikisha hakuna nguo au pillows hapo karibu kwa sababu anaweza kujifuna nazo na akakosa hewa ikawa majanga.Hii imenitokea jana tu,nilitoka kwenda hosp nina sindano za masaa niliporudi sikumkuta maid,mtoto wangu wa miezi minne alikuwa kitandani kalia mpaka sauti imemkwama na alikuwa kavuta blanket yake kajifunika usoni.Karibu nizimie.

Pole sana, na hawa watoto wetu wa kuachwa na nannies ni Mungu tu anawalinda, ukimuuuliza alienda wapi atakuambia kununua phone card na hapo kaondoka madakika ya kutosha.
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Pole sana, na hawa watoto wetu wa kuachwa na nannies ni Mungu tu anawalinda, ukimuuuliza alienda wapi atakuambia kununua phone card na hapo kaondoka madakika ya kutosha.

asante,alikuja after like 30 minutes akasema alipeleka nguo take kwa fundi,just imagine.yaani Ni shiiida
 
usidhubutu kumuacha mtoto na mshumaa ukiwa unawaka

usimuache mwanao ndani ya gari wakati bila uangalizi wa mtu mzima tena mwenye akili timamu
 
Unapomlaza mtoto mdogo kitandani hakikisha hakuna nguo au pillows hapo karibu kwa sababu anaweza kujifuna nazo na akakosa hewa ikawa majanga.Hii imenitokea jana tu,nilitoka kwenda hosp nina sindano za masaa niliporudi sikumkuta maid,mtoto wangu wa miezi minne alikuwa kitandani kalia mpaka sauti imemkwama na alikuwa kavuta blanket yake kajifunika usoni.Karibu nizimie.

My dear usimfunike blanket mtoto au chochote badala ya shuka tena ambalo limechomekwa vizuri asijekuvuta yaani usiwache chochote katika crib yake kama kuna baridi nvalishe nguo ambayo itamfanya awe warm.....

Kisses kwa baby.....
 
asante,alikuja after like 30 minutes akasema alipeleka nguo take kwa fundi,just imagine.yaani Ni shiiida

Mungu wangu.......ningemdunda aiseee.....yani apeleke nguo kwa fundi kamwacha mwanangu sauti imekauka.......
 
Pole kwa wafiwa......mpaka mtoto afikie hatua ya kujitambua ni neema tu ya Mungu.......na wazazi tujitahidi kuwa makini......bora umweke mtoto mgongoni wakati unaendelea na shughuli zako ndogondogo......
 
Back
Top Bottom