Kumuua mtoto wako

Kumuua mtoto wako

Mungu wangu.......ningemdunda aiseee.....yani apeleke nguo kwa fundi kamwacha mwanangu sauti imekauka.......

ungemdundaaaaa!!!?? hujaona wenzio wanavyonyea ndoo sahivi ndugu kwa kuwapiga hao watu??

na ukimdunda ataendelea kukaa na mwanao ama utambadilisha??
 
Mhhh! Pole sana Mungu ashukuriwe. Nadhani hasira ulizokuwa nazo kwa huyo msaidizi wako Mungu ndio anajua.

Unapomlaza mtoto mdogo kitandani hakikisha hakuna nguo au pillows hapo karibu kwa sababu anaweza kujifuna nazo na akakosa hewa ikawa majanga.Hii imenitokea jana tu,nilitoka kwenda hosp nina sindano za masaa niliporudi sikumkuta maid,mtoto wangu wa miezi minne alikuwa kitandani kalia mpaka sauti imemkwama na alikuwa kavuta blanket yake kajifunika usoni.Karibu nizimie.
 
Kwenye swimming pools pia wazazi wasithubutu kuwaacha watoto wao bila uangalizi hata wa dakika moja, maana kufanya hivyo kunaweza kusababisha kifo kutokea na mzazi/wazazi kubaki akijilaumu/wakijilaumu kwa miaka chungu nzima.

Dakika moja kugeuka kuchukua towel inaweza kusababisha maafa makubwa. Janga lingine ni ndoo za maji, watoto wengi sana wamepoteza maisha kwa kutumbukia kwenye ndoo za maji zinazohifadhiwa majumbani kwetu.

Always tunashauriwa tujue mtoto yuko wapi na anafanya nini wakati wote. Ni muhimu sana the price to pay is too high.
 
ungemdundaaaaa!!!?? hujaona wenzio wanavyonyea ndoo sahivi ndugu kwa kuwapiga hao watu??

na ukimdunda ataendelea kukaa na mwanao ama utambadilisha??

Kwa hasira zile ningemdunda ila baada ya hasira kuisha ningemwomba msamaha........kwenye maswala ya watoto sijui nikoje.......kuna siku nshawahi kumpiga kibao mkaka kituoni.....alimweka mtoto kizembe nusu apitiwe na bus la mkoa......yani nilimzaba cha nguvu.....baadae nikamwomba msamaha afu nikamwambia kuwa makini na mtoto ukiwa barabarani......
 
ungemdundaaaaa!!!?? hujaona wenzio wanavyonyea ndoo sahivi ndugu kwa kuwapiga hao watu??

na ukimdunda ataendelea kukaa na mwanao ama utambadilisha??

Kingine hakuna mtu ambae namheshimu kama dada wa kazi....nilianza kukaa nae tangia nina mimba mpaka sasa mtoto ana miaka miwili.......sijawahi mpiga na ukweli nae anajitahidi katika maswala la mtoto......basi nami najitahidi kumpa offer mbalimbali na kukaa nae vizuri....mana kukaa nae vizuri mtoto ndo faraja yangu.....
 
Huko mbele kwa incidence kama hii mzazi lazima ufikishwe kwa pilato...
 
Kwa hasira zile ningemdunda ila baada ya hasira kuisha ningemwomba msamaha........kwenye maswala ya watoto sijui nikoje.......kuna siku nshawahi kumpiga kibao mkaka kituoni.....alimweka mtoto kizembe nusu apitiwe na bus la mkoa......yani nilimzaba cha nguvu.....baadae nikamwomba msamaha afu nikamwambia kuwa makini na mtoto ukiwa barabarani......

ni uchungu wa mwanao unakufanya hivi ama hivyo ndivyo ulivyo??
jaribu kucontrol hasira maana watu wengine hawasamehi hadi na yeye akurudishie walau "kidogo"
 
inasikitisha sana, poleni sana kwa waliofiwa, wenye watoto wadogo ni vizuri kucheck walipo kabla hujawasha gari, unamwita dada tu na kumuuliza kama yuko na mtoto akisema ndio unatoka, kama hayuko naye unahakikisha unajua mtoto alipo kabla hujawasha gari, yaani inauma sana kama mzazi.
 
Kingine hakuna mtu ambae namheshimu kama dada wa kazi....nilianza kukaa nae tangia nina mimba mpaka sasa mtoto ana miaka miwili.......sijawahi mpiga na ukweli nae anajitahidi katika maswala la mtoto......basi nami najitahidi kumpa offer mbalimbali na kukaa nae vizuri....mana kukaa nae vizuri mtoto ndo faraja yangu.....

Kweli kabisa, hebu fikiria, mtu sio ndugu yako wala ndugu wa mume wako unaondoka unamuachia mtoto wa miezi saba, ukirudi unakuta mtoto wako msafi kashiba anacheka cheka tu, usipomuheshimu kwa sababu tu unamlipa mshahara utakuwa ni mjinga wa kutupwa. Ingawa kuna wengine hata uwape nini hawaappreciate
 
Mungu wangu, sipati picha uchungu walonao hao wazazi.Aisee tunatakiwa tuwe makini sana na hawa watoto wetu.R.I.P mtoto jamani .
 
mtoto ni kitu sensitive sana, ukisikia tukio kama hili, ukiwafikiria wanao, dah ngumu sana.

ndio maana wapo wanaosema uchungu wa mwana aujuae mzazi ila wengine wanaikuza kuonyesha mwanamke aliienda leba anajua tamu na chungu ya mtoto
kunamama mmoja siku alishuhudia mtoto (sio wake) karibu agongwe na gari nikamsikia akisema "mpaka mshono wa operesheni umeuma upya" nikaelewa namna gani wanavyochukulia mtoto yoyote hivyo hata wewe sikushangai
pole sana
 
ni uchungu wa mwanao unakufanya hivi ama hivyo ndivyo ulivyo??
jaribu kucontrol hasira maana watu wengine hawasamehi hadi na yeye akurudishie walau "kidogo"

Uchungu wa mtoto yoyote yule.....sipendi nimwone mtoto yoyote anateseka kwa lolote.......
 
Kweli kabisa, hebu fikiria, mtu sio ndugu yako wala ndugu wa mume wako unaondoka unamuachia mtoto wa miezi saba, ukirudi unakuta mtoto wako msafi kashiba anacheka cheka tu, usipomuheshimu kwa sababu tu unamlipa mshahara utakuwa ni mjinga wa kutupwa. Ingawa kuna wengine hata uwape nini hawaappreciate

Sana yani unarudi mtoto ana furaha zote....kama wangu nikirudi anachukua pochi anatafuta hela anampa dada yake.......kitu chochote utasikia ya dada.......yani nawaza akisema anataka kuondoka....nitambembeleza aisee hata mshahara nita double ili asiondoke.............
 
Back
Top Bottom