Erythrocyte
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 117,696
- 218,216
Kitendo cha Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kumtambulisha Nusrat Hanje kama kiongozi wa Bavicha, na kwamba ule ndio uwakilishi wa vijana wa Chadema kwenye Mkutano wa Rais na Vijana huko Nyamagana Mwanza ni kumpiga changa la macho Mh Rais .BAVICHA haikuhudhuria mkutano huo na wala haikutuma mwakilishi yeyote.
Nusrat Hanje na wenzake 18 walishafukuzwa kwenye uongozi na kuvuliwa uanachama wa Chadema kwa tuhuma za USALITI, hawa wote kwa ujumla wao hawana uwezo wa kuwakilisha chadema kwenye jambo lolote.
Aliyetangaza jambo hili la uongo alilenga kumdanganya Rais ili ionekane Mkutano ule wa vijana wa CCM na Mwenyekiti wa chama chao ni mkutano wa vijana wote wa Tanzania, wakati si kweli. Napendekeza muongo huyo atumbuliwe haraka ili kunusuru mambo yasiharibike zaidi, ikiwa na ugeni wake Mwanza ameanza na uongo duni kama huu, itakuwaje akiachwa hapo mwaka mzima?
Nusrat Hanje na wenzake 18 walishafukuzwa kwenye uongozi na kuvuliwa uanachama wa Chadema kwa tuhuma za USALITI, hawa wote kwa ujumla wao hawana uwezo wa kuwakilisha chadema kwenye jambo lolote.
Aliyetangaza jambo hili la uongo alilenga kumdanganya Rais ili ionekane Mkutano ule wa vijana wa CCM na Mwenyekiti wa chama chao ni mkutano wa vijana wote wa Tanzania, wakati si kweli. Napendekeza muongo huyo atumbuliwe haraka ili kunusuru mambo yasiharibike zaidi, ikiwa na ugeni wake Mwanza ameanza na uongo duni kama huu, itakuwaje akiachwa hapo mwaka mzima?