Mmawia
JF-Expert Member
- Aug 20, 2013
- 121,947
- 95,237
Hivyo vyoote vitafanyika maana ni kutumia rasilimali za taifa tena zitafanyika Mara 2 zaidi.Mimi naendelea kufurahia Magufuli kuitwa Fisadi, maana yake Magufuli akiitwa fisadi, basi serikari inayomfuata ifanye mambo meengi na makubwa kuliko aliyofanya Magufuli Kwa miaka yake mitano
Usambazaji umeme na bei chipa ya kuunganishia watu, ziwe Chini zaidi yake na umeme usambazwe Kwa Kasi kuliko yeye
Hospital na vituo Vya Afya, madawa na mikopo pamoja na kulipa Ada za shule msingi Hadi sekondari uongezwe kuliko yeye
Miradi kama SGR, bwawa la umeme, madaraja ya juu mfugale yawe karibu Kila jiji nchini, ndiyo, si alikuwa fisadi?? Mfanye makubwa kuliko yeye
Madege mlete angalau 50, viwanja Vya Ndege msivikarabati Tu, jengeni hata 20 hivi, stend za mabasi zienee Hadi tarafani huko
Maji vijijini, kero hii iishe na muende mbali zaidi Kwa kusambaza mabomba huko, Miradi ya maji kutoka Victoria fanyeni haraka Sana ufike Dodoma
Kwa kufanya makubwa zaidi kumshinda fisadi Magufuli kutathibitisha mkisemacho hapa, la sivyo utakuwa ni ujinga na upumbavu
Tunaye mama yetu hatuna wasiwasi