Bravo247
Senior Member
- Sep 14, 2013
- 108
- 229
Nimejifunza ni bora lawama kuliko fedheha.
Ndugu yangu alikuwa na mahusiano mazuri sana na mimi tuliweza kuwasiliana na kutembeleana mara kwa mara, lakini mambo yalibadilika baada ya yeye kupata matatizo fulani na kuomba nimuazime kiasi fulani cha pesa (kikubwa tu), nikamsihi nami niko vibaya basi ajitahidi arejeshe kwa wakati kama alivyoahidi.
Cha ajabu muda ulivyokuwa unakaribia nilimkumbusha na akakejeli hiyo pesa ataitafuta ndani ya siku tatu karibu na deadline. Nilikaa kimya nikiwaza kama aliona ni kiasi ni cha kutafuta kwa siku tatu kwanini alikuja kuazima?
Siku ikawadia nkamkumbusha naomba ile fund maajabu jamaa akasema jioni, mara nimpe siku kadhaa. Ikawa week na sasa miezi. Nashindwa kuwasiliana naye maana meseji hajibu simu hapokei.
Nilichojifunza ni heri kutokumkopesha ndugu upate lawama kuliko kumkopesha na kuua undugu.
Ndugu yangu alikuwa na mahusiano mazuri sana na mimi tuliweza kuwasiliana na kutembeleana mara kwa mara, lakini mambo yalibadilika baada ya yeye kupata matatizo fulani na kuomba nimuazime kiasi fulani cha pesa (kikubwa tu), nikamsihi nami niko vibaya basi ajitahidi arejeshe kwa wakati kama alivyoahidi.
Cha ajabu muda ulivyokuwa unakaribia nilimkumbusha na akakejeli hiyo pesa ataitafuta ndani ya siku tatu karibu na deadline. Nilikaa kimya nikiwaza kama aliona ni kiasi ni cha kutafuta kwa siku tatu kwanini alikuja kuazima?
Siku ikawadia nkamkumbusha naomba ile fund maajabu jamaa akasema jioni, mara nimpe siku kadhaa. Ikawa week na sasa miezi. Nashindwa kuwasiliana naye maana meseji hajibu simu hapokei.
Nilichojifunza ni heri kutokumkopesha ndugu upate lawama kuliko kumkopesha na kuua undugu.