Kumekucha CCM vs UKAWA

Kumekucha CCM vs UKAWA

Hivi nani aliyewafukuza bungeni?
Unajua mkifanyacho ni kama wenza waliotengana na mmoja kaenda kwao. Anakaa siku alizotegemea mwenzie lazima amrudie zinapita anarudi na kufanya kitimbi kingine kama alimuacha mtoto anamrudia na kuondoka naye. Bado anaona arejewi anarudi kudai vyombo. Bado arejewi wala ndugu hawaingilii anashitaki ustawi wa jamii. Bado arejewi antishia kunywa sumu. Bado arejewi sana anataka kuchoma nyumba moto.
Kuishi katika ndoa unataka vitimbi vya nini? Hiki chama cha watoa matamko hawana akili. Mtu wa kumtolea matamko ni nani hasa? Mh Magufuli? Kweli viroba vibaya. Hapa ni kazi tu mmelikoroga kunyweni wenyewe. Waambieni hao wakosa adabu wenu huko bungeni waache ujinga warudi wafanyekazi.
Hivi wanachotaka wafanyweje hasa? Semeni, kwani hakuna amri ya NS kuwafukuzeni. Ndio maana inakuwa ngumu viongozi wa dini na wazee wenyekuheshimika sana humu nchini kuliingilia. Nyie ndio waathirika nyinyi ndio wasababisha uathirika wenu na uwezo wa kuacha vitendo vya kujiathiri mnao wanashindwa waingie wapi kuwasaidia.
Huenda huu ujinga waliouamua huwa unauraibu kiasi kwamba mtu hushindwa kujiondoa mwenyewe. Waseme basi kuwa wamekuwa mateja wa kutoka nje ili waanzekutumia dawa ya kuondokana na huo ujinga.
Pole mkuu, naona unatetea ugali, ila in a mattee of time, ikishaingia kwenye social circle ikaeleweka mtaelewa maana yake.
Siasa ina nguvu sana hapa duniani na kwa jamii, busara ni muhimu, udongo uwah ungal maji
 
Watanzania tuombe mungu atujaalie amani na upendo na kwa uwezo wake auzime huu Moshi unaofukuta...Aaamin
 
UZURI ni kwamba WATANZANIA hatujafikia level hii ya kufanya MAIGIZO mnayotaka tufanye..afu MKAE MJUE vyama vya SIASA SI DINI ZETU wala MAKABILA YETU kiasi kwamba inaweza tenganisha umoja wetu.....NA KATIKA HILI MNAJIDANGANYA maana CDM haina ushawishi wowote kwa WATANZANIA kwa kipindi hichi ambacho WATANZANIA wote tunamuona MAGUFULI NDIO MKOMBOZI WETU.....kuthibitisha hili tuone kama mtafanikiwa mnachotaka kukifanya.....
AFU na nyie BAVICHA ebu mtuambie TOKEA huu mwaka umeanza mmeisha toa matamko mangapi juu ya SERIKALI HII na JE MAFANIKIO yenu juu ya HAYA MATAMKO ni yepi???...EBU TUPENI MREJESHO ili tuwasapoti katika hili....MAANA TUMEISHA WACHOKA NA MATAMKO YENU YA SIYO KUA NA KICHWA WALA MIGUU
Unamsemea na Nani hapo?labda familia yako tu
 
Hiyo misuguano yenu isije kutusumbua tusiokuwa na kadi,maana mmeshajiona sasa ndio wenye nchi wakati watanzania zaidi ya million 30 hawazijui hata kadi za vyama.

Usiwe na shaka sisi hii haituhusu, unadhani konda gani atakaepandisha abiria kwenye Daladala kwa kuonyeshwa kadi ya chama siasa, au mangi auze duka lake kwa kuonyeshwa kadi.

Mmachinga au bidhaa za kwa kuonyeshwa kadi, wauza maji barabarani waonyweshe kadi, baar zihudumie kwa kadi za siasa, kwa mama muuza tuhudumiwe kwa kadi.

Haiwezekani labda hao hao wanachama wenu, sisi tusiokuwa wanachama wa vyama vyenu mtupandishe mabasi ya mikoani kwa kuonyesha kadi ya cha siasa, gesti tuingie kwa kadi ya siasa, feli huduma samaki tuipate kwa kuonyesha kadi ya siasa hii haiwezekani.

Kwa sababu mimi sina kadi na sifirii kuchukua kadi ya chama, bali nitabaki mpiga kura, mtakachoweza nikifa muisusie kuizika maiti yangu, lakini hamtaweza maana nitanuka mtanizika tu, haijalishi nitazikwa na watu wangapi maana maiti haioni fahari, hata azikwe na walimwengu wote.

Na sema hii huku kwetu imedunda ikajalibiwe kwingine. Yote kwa yote wotd mnahusika na vyama vyenu CCM na UKAWA kaa muangalie watanzania kwanza, lolote likalotokea watanzania watawalilia.
 
Mimi natangaza rasmi kuvunja uhusiano wa aina yoyote na mwana ccm, hata kama ni ndugu wa damu tusijuane kuanzia sasa.
 
Pole mkuu, naona unatetea ugali, ila in a mattee of time, ikishaingia kwenye social circle ikaeleweka mtaelewa maana yake.
Siasa ina nguvu sana hapa duniani na kwa jamii, busara ni muhimu, udongo uwah ungal maji
Hapa natoa darasa ili tupunguze wajinga. Wewe huenda umeelewa. Ndio ninavyopunguza wajinga hivyo.
 
sijali sana kuhusu matokeo ya huu uamuz,, iwe yataleta madhara au la!!......

lkn jambo moja li wazi kabisa, umoja wetu unapitia jaribio kubwa kisa tu wanasiasa wachache wanafanya maamuzi wanayoyajua wao!!

hili si jambo la kulishangilia au kubeza,, hizi mbegu sio salama kwa ustawi wa taifa letu!
 
Mke wangu tunatofautiana itikadi za vyama lakini ananipa haki yangu kama kawaida...kwa maana ushirikiano upo na amechukia sana ukawa kususa bunge na inshaallah keshokutwa namvisha kijani...

Nyie endeleeni kutoa matamko...chama kinapoteza umaarufu wake kwa kasi ya ajabu.
 
13495052_954168124681827_3057961959794714549_n.jpg
 
Upinzani haukuanza leo nchini, na miaka yote Wabunge wa upinzani na wale wa CCM wameshirikiana katika mambo mbali mbali kama Watanzania. Cha kustaajabisha ndani ya miezi minane tu ya Serikali hii ya awamu ya tano kumejengeka chuki za kutisha kati ya Wabunge wa upinzani na wale wa CCM. Wabunge wa CCM wamekuwa wakiwatusi Wabunge wa upinzani kwa matusi ya nguoni mara kwa mara bila ya kuchukuliwa hatua zozote za kinidhamu na hiyo inayoitwa kamati ya Bunge ya maadili. Kwa maneno mengine wajumbe wa kamati hiyo ya maadili wameridhia Wabunge wa upinzani kutukanwa matusi ya nguoni.

Sasa chuki inaongezeka hata kuanza kutosalimiana na chuki hii haitaishia kwa Wabunge tu bali inaweza kabisa kusambaa miongoni mwa Watanzania. Tutafakari kwa kina na kukemea huu upandikizaji wa mbegu za chuki za kutisha unaofanywa ndani na nje ya Bunge kwa kasi ya kutisha. Tukikaa kimya na kuwaacha hawa wapandikizaji wa mbegu za chuki waendelee na mradi wao basi siku za usoni nchi yetu itaingia kwenye giza nene sana kwa sababu tu wapandikizaji chuni nchini hatukuwakemea mapema na kwa nguvu zote matokeo yake mbegu zao za chuki mizizi yake itakuwa imetambaa nchi nzima.
 
MAMBO yanazidi kwenda mrama kati ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) na vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA), anaandika Dani Tibason. Msimamo uliotolewa na Baraza la Vijana wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (BAVICHA) unaakisi mwanzo mpya wa msuguano wa kisiasa nchini.

Tayari BAVICHA wametangaza msimamo wa kutoshirikiana na vijana wa CCM katika tukio la aina yoyote. Mbali na kutangaza msimamo huo pia wametangaza kuzuia mikutano yote ambayo itaandaliwa na CCM kama inavyozuiwa ya CHADEMA.

Msimamo huo umetolewa leo na Julius Mwita, Katibu Mkuu wa BAVICHA wakati akizungumza na waandishi wa habari Dodoma.
Mwita amesema, kutokana na kitendo cha Serikali ya CCM kushirikiana na Jeshi la Polisi kuzuia mikutano ya Chadema kinaonesha wazi kuwa, serikali ina mpango wa kuhakikisha inaua upinzani jambo ambalo haliwezi kukubalika.

Amesema, kutokana na hali hiyo kwa sasa BAVICHA wametangaza kutoshirikiana na vijana wa CCM katika mazingira yoyote ikiwa ni pamoja na katika masomo, nyumba walizopanga, misiba na katika majamga mengine mbalimbali.

“Kutokana na kuwepo kwa vitendo vya kikatili vinavyofanywa na Serikali ya CCM vya kuzuia mikutano ya upinzani, sasa tunatangaza sisi vijana wa Bavicha hatutashirikiana na wanachama wa CCM kwa njia yoyote ya kijamii wala kimaendeleo.

“Natangaza kwa vijana wote wa CHADEMA hatutashiriki katika mazizi, hatutashiriki kusoma nao wale waliopo katika vyuo, hatutashiriki sherehe mbalimbali zinazowahusu wao wala hatutashiriki katika jambo lolote la kimaendeleo, na hii ni msimamo wetu.

“Pia tunawapongeza wabunge wetu kwa kususia shughuli zote za ambazo zinafanywa na CCM kwani kwa kufanya hivyo inaonesha kuwa sasa tumechoka na uongozi wa kiimla,” amesema Mwita.

Hata hivyo amedai, Rais John Magufuli ni muoga kuliko marais wote kwa kuwa ni rais ambaye hapendi kukosolewa na kuambiwa ukweli pale ambao amekuwa akikosea jambo ambalo anatakiwa kujitafakari na kujikosoa.

“Sasa vijana vijana tumejipanga kuhakikisha Jeshi la Polisi linazuia mikutano au mikusanyiko ambayo inafanywa na CCM na ikumbukwe kuwa, 23 Julai mwaka huu CCM watakuwa na vikao vya kumkabidhi rais Magufuli kuwa mwenyekiti wa CCM.

“Sasa tunataka Jeshi la Polisi kuzuia mkusanyiko huo na kama haitawezekana vijana wa CHADEMA na UKAWA watazui mikutano hiyo.

“Haiwezekani mikutano ya CHADEMA ikawa ndiyo inayozuiliwa wakati mikutano na mikusanyiko ya CCM inaendelea kufanyika, jambo hili kamwe haiwezi kukubalika na tunasema sasa imefika mwisho wa uvumilivu,” amesema Mwita.

Edward Simbeye, Katibu Mwenezi BAVICHA amesema, yeye ndiye mratibu wa mahafali za wanafunzi wa CHADEMA vyuo vikuu (Chaso) nchini hivyo polisi walipaswa kumkamate yeye na si kuzuia mahafali hayo.

Inanikumbusha Pemba kuna mnunuzi wa samaki ambae ni kada wa CCM kwenye mnada wa samaki alifika bei ya 170,000 kwa tenga na kufaninikiwa kushinda .Lakini mchuuzi akamwuzia mnunuzi aliefika bei ya 70,000 ambae ni kada wa CUF mwenzie.

Kada wa CCM alipohoji nae akajibiwa na yule mchuuzi wa CUF kwamba mbona na sisi tukishinda uchaguzi hatupewi madaraka
 
Inanikumbusha Pemba kuna mnunuzi wa samaki ambae ni kada wa CCM kwenye mnada wa samaki alifika bei ya 170,000 kwa tenga na kufaninikiwa kushinda .Lakini mchuuzi akamwuzia mnunuzi aliefika bei ya 70,000 ambae ni kada wa CUF mwenzie.

Kada wa CCM alipohoji nae akajibiwa na yule mchuuzi wa CUF kwamba mbona na sisi tukishinda uchaguzi hatupewi madaraka
nimeipenda hiii...
 
Mbuyu huanza kama mchicha. Huku tunakoelekea na ugumu huu wa maisha usishangae kupata support kubwa ya watu. Mpaka sasa bado Magufuli hajafanya kile watanzania walichotarajia zaidi ya hadithi ya majipu. Sasa hivi ukimsifia Magu huoni watu wengi wakisupport kama ilivyokuwa miezi mitatu ya mwanzo, sasa hivi ni kama watu wamepoteana wanangoja tu mawazo mbadala ili rasmi wamtoe maanani. Kama ugali mezani unakuja kwa shida hata utoe ahadi gani itakuwa ngumu kuungwa mkono, sana sana wananchi wataingiwa tu na hofu dhidi ya dola ila sio kukufurahia. Fanya utafiti wa kutosha, wanaosifia wamebaki wanaccm tena kwa unafiki lakini kwa ugumu huu wa maisha hata hiyo pumzi ya kusifia inaanza kukata.
Umeongea kama nilivyokuwa nawaza......True story
 
Haya ndio matokeo ya kuwa na mfalme anayeongoza nchi kwa chuki.
Mimi nnauhakika Tanzania ikipata janga kubwa, huko CCM hakuna wa kuwaunganisha wananchi.
Hii awamu hakuna busara ya uongozi!
 
Huo ndio msimamo wa bavicha, upende husipende na watu tupo tayari kujiunga na ushauri wao, we nani hadi unawasemea watanzania?
Na hao Bavicha nani ata wawasemee watanzania au siku hizi vijikundi vya siasa vina power ya kuwasemea watanzania? kuwa kimawazo wewe dogo.
 
UZURI ni kwamba WATANZANIA hatujafikia level hii ya kufanya MAIGIZO mnayotaka tufanye..afu MKAE MJUE vyama vya SIASA SI DINI ZETU wala MAKABILA YETU kiasi kwamba inaweza tenganisha umoja wetu.....NA KATIKA HILI MNAJIDANGANYA maana CDM haina ushawishi wowote kwa WATANZANIA kwa kipindi hichi ambacho WATANZANIA wote tunamuona MAGUFULI NDIO MKOMBOZI WETU.....kuthibitisha hili tuone kama mtafanikiwa mnachotaka kukifanya.....
AFU na nyie BAVICHA ebu mtuambie TOKEA huu mwaka umeanza mmeisha toa matamko mangapi juu ya SERIKALI HII na JE MAFANIKIO yenu juu ya HAYA MATAMKO ni yepi???...EBU TUPENI MREJESHO ili tuwasapoti katika hili....MAANA TUMEISHA WACHOKA NA MATAMKO YENU YA SIYO KUA NA KICHWA WALA MIGUU

Huku Kwetu Kuna MwanaCCM mmoja alikuwa ni mwathirika wa UKIMWI kwa muda Mrefu na alikuwa akifuata dawa za kuongeza siku za kuishi makao makuu ya Wilaya ambapo kutoka kijijini kwetu hadi wilayani(Hospitali ya wilaya) nauli ya BUS ni Tsh 10,000/= kwenda na kurudi.

Sasa baada ya kumalizika uchaguzi kukatokea utengano wa kiwango cha juu sana, na kwa vile jamaa alikuwa anachangiwa nauli na marafiki zake ambao ni wana CDM wakakata huo mrija na ndugu yetu huyo akawa ameshindwa kuendelea na dozi kwa kukosa nauli ya kwenda kuchukua dawa, Jamaa AFYA yake ikawa mbaya sana na kupelekea kufariki.

Bad enough baada ya kufariki watu waligoma kumzika pale kijijini kwa sababu hakuwa na eneo la ardhi yoyote, ilibidi wananzengo watoe taarifa police ndo waliokuja kuuchukua mwili wake na kwenda kuuzika wanakojua wao.

Jamani hili Tamko cyo la kupuuzia hata kidogo kwa sababu baadhi ya watu hasa wana CCM ndo wahanga wakubwa sana wa hili tamko.Kwa MTU asiyejua kinachoendelea sehemu nyingi hapa Tz hasa vijijini anaweza akasema ccm inapendwa lkn ukijitambulisha kuwa wewe ni mwanachama au mshabiki tu wa ccm, watu wanakuona kama vile ni shetani flani hivi.

CCM hili tamko ni baya sana kwa usitawi wa watu wenu I mean wanachama wenu kuweni makini.
 
Back
Top Bottom