Pascal Mayalla
Platinum Member
- Sep 22, 2008
- 50,467
- 113,565
Ndugu yangu Kigarama, unapoamua kuwa mkweli siku zote, ujue pia kuna price to pay, yaani kuna Vigharama utaingia. Hivyo unapoikosoa Chadema humu kwenye jf, pia ujiendae kupokea malipo ya ukosoaji huo!.Tatizo letu limelala hapo kwenye kufikiri kwenye kujiokoa kila kinachoparamiwa ni kitu salama. kuna methali ya kiswahili inayosema 'mfa maji haishi kutapatapa.
Mimi sijaona kama nao CDM wako makini kwa wanachokifanya na wala kama wanajua kwa usahihi wapi wanataka kutupeleka kama chama tawala baada ya CCM. Mfano maandiko mengi humu ndani yanaonyesha kwamba wana JF wanaamini kwamba Waislamu(Viiongozi wao?) wanaishabikia CCM kuliko CDM. Lakini sijaona karipio kali kutoka kwa viongozi wa CDM dhidi ya tabia ya sehemu kubwa ya washabiki wao kudhania CDM ni chama kilicho dhidi ya uislamu.
Viongozi wengi wa CDM (Mbowe amejitoa) wanaamin kwamba Peoples powers inamaanisha ni matumizi ya nguvu kwenye kudai "haki" na "Ukamanda" ni ukakamavu kwenye kutokutii sheria na mapambano na Polisi hata bila ya sababu za msingi. hata humu ndani ukisema CDM wamekosea utarukiwa kama kibaka aliyekamatwa akitaka kuiba simu Kariakoo.
CDM kama chama hakina Oganaizesheni ya uhakika kwenye mambo yake ya kila siku na hakuna anayeonyesha kujali.Ukiwauliza watu CDM Makao Makuu ni kiasi gani fedha chama kitatumia kwenye uchaguzi wa Igunga na chaguzi ndogo za Madiwani inawezekana hawajui kabisa kwani fedha nyingi za kuendeshea chama ama "wanakopeshwa" na Mbowe au wanapewa "msaada" na Mzee Ndesamburo.
Niliwahi kuposti hii...
[h=3]
CCM Imechokwa; CHADEMA Haijajipanga![/h]
Nilichoambulia niliambulia lakini kwa vile huu ndio ukweli wangu, kila unapotimia nitakuwa nakumbushia.