Wajameni... Leo naomba tusaidiane kujadili jinsi tunavyowadhalilisha wapenzi wetu in the name of love and protection
Kuna rafiki yangu ana kaugonjwa kabaya sana ka kumnyang'anya mkewe simu na kukaa nazo hata siku mbili kusubiria nani atampigia mkewe... i tried to ask him kuacha tabia hiyo kwani inamweka mwanamke kwenye hisia za kudhalilishwa na kutoaminiwa na pia mke anaweza sasa akaanza kufanya siyodhani simply because jamaa ndicho alichonacho kichwani!!
Sipendi hii tabia na nina imani wengi hamuipendi
please pals, lets not do this aisee
Sijui kama nipo nje ya topic. Kuna jamaa siku moja natembea mitaa ya multichoice pale kontena nilimshuhudia akimnasa mpenziwe wa kike vibao. Mwanzo nilidhani wanafanya masikhara kuja kushtuka kumbe ni siriasi, mdada alikuwa akilia kwa kwikwi huku jamaa akimpa kofi mbili tatu hivi. Aisee iliniuma kinoma utadhani aliyepigwa ni dada yangu