Kumbe Shetani Alikuwa Mwandishi wa Habari!, na Alichomfanya Eva Bustani ya Eden ni Uandishi wa Habari?- Je Media Tuombwe Msamaha Kuitwa Shetani au?

Pascal Mayalla

Platinum Member
Sep 22, 2008
50,498
113,601
Wanabodi

Declaration of Interest

Mimi ni Mkristu Mkatoliki, ila mara moja moja huwa nahudhuria mafundisho katika madhehebu mbalimbali, ikiwemo Lutheran, Anglican, Makanisa ya Wokovu, na kwa wachungaji mbalimbali akiwemo Nabii Mwingira, Askofu Kakobe, Mzee wa Upako, Mwamposa, Assemblies of God, na hadi mihadhara ya Kiislamu.

Angalizo za Kiimani Kwa Open Minded na Closed Minded.
Kwenye mambo ya imani, kuna watu wa aina mbili, open minded na closed minded.
Open minded ni wale waumini wanaoamini dini with an open mind, hata akitokea mtu wa imani nyingine kinyume na imani yako, you can listen and try make sense out of it. Hili ndio bandiko Lao.

Lakini kuna closed minded people ambao wakiaminishwa dini yao, wao wanaamini ni Mungu mwenyewe, hivyo hata ukiwaambia vitabu vya dini vimeandikwa na binadamu na kuhaririwa, hawawezi kuamini wanaamini ni Mungu ndio kuaandika hivyo ukileta jambo lolote ambalo wao hawalijui, watakuona kama ni una kufuru, watu hawa closed minded naombeni muishie hapa maana huko mbele mtaishia kuumia kiimani, just keep on believing what you believe.

Biblia ni kitabu kitakatifu cha dini ya Kikristu, wakati yaliyoandikwa kwenye Bibilia yanatendeka, kuna mengine ni mambo mabaya kabisa hayaandikiki, bila staha hivyo kwenye Bibilia kuna baadhi ya mambo yameandikwa lugha ya picha na tamathali za semi kwa la kuweka staha, moja ya mambo hayo ambayo yameandikwa Kwa staha ni ile dhambi ya asili, the original sin, kumaanisha sisi binadamu asili yetu ni dhambi fulani lazima itendeke ndipo kiumbe kizaliwe. Kwa sisi Wakristu Wakatoliki, dhambi hiyo ya asili huondolewa kwa sacrament ya Ubatizo na mapadri, masista, makasisi wetu na maaskofu wetu hawaruhusiwi kuitenda!.

Moja ya jambo lililoandikwa Kwa staha kubwa kwenye Bibilia ni kuhusu dhambi ya asili, "the original sin" ya Mama yetu Eva kushawishiwa na shetani, ale lile tunda walilokatazwa na Mungu wasilile.

Shetani akajigeuza nyoka, akapenya Bustanini, kuna kitu hakikusemwa kwenye Bible, lakini kupitia the powers of information powers, sisi baadhi yenu tumejaaliwa kuwa nazo, hivyo tunauwezo wa kuvijua baadhi ya vitu ambavyo vilitokea lakini haviku jandikwa ili kutunza staha!.

Shetani baada ya kujigeuza nyoka na kupenya Bustanini, si wengi wanafahamu kuwa shetani ni bingwa wa kuji disguise, na anaweza kuji disguise kuwa kiumbe chochote na hata kuji disguise as God na akaponya watu na kufanya miujiza!, na kuna mara kibao shetani ana ji disguise as God, na kufanya ishara na miujiza ili watu wamwamini na kumfuata na kumwabudu, hivyo kuna wengi wanamwabudu shetani disguised as God bila wao kujijua, wakidhani wanamwabudu Mungu wa Kweli!.

Hivyo shetani baada ya kujigeuza nyoka na kufanikiwa kupenya Bustanini, kabla hajamtokea Eva, alijigeuza, kiumbe kingine, ndipo akamtokea Eva! na Eva akashituka sana kuona kuna mtu mwingine zaidi ya Adam!, na hapo ndipo ushawishi ukaanza na katika kumshawishi Eva kula lile tunda, shetani alimshawishi sio kwa maneno tuu bali na kwa matendo practically ikiwemo kulichuma hilo tunda akalishika na kumuonyesha Eva jinsi tunda linavyomegwa na akamegea Eva na shetani na wakala kwanza tunda wao Eva na shetani na baada ya Eva kuonja utamu wa lile tunda, ndio sasa akaenda Kwa Adamu kumpelekea tunda na kumshawishi Adam kwa kumuonyesha jinsi tunda linavyomegwa na kumlazimisha Adamu kumega practically nae Adamu akamega tunda kisha, wakaishia zao usingizini, walipoamshwa ndipo wakajishtukia kuwa wako uchi baada ya kujua kazi ya vile viungo vya ule mti wa katikati na kumega tunda, na hapo ndipo ikawa wametenda dhambi ya asili, yaani the original sin!. Na adhabu yako sasa ni kufukuzwa Bustanini na Mwanamke atazaa kwa uchungu kufidia kumshawishi Adamu kumega tunda, hivyo wale wanawake wanaozaa kwa ceaserian by preference ili kukwepa maumivu ni wanatenda dhambi bila kujitambua.

Hivyo dhambi ya asili sio sio mti sio tunda, sio neno "mega tunda" au "kula tunda la mti wa katikati" ni "tendo" la kukatazwa usifanye jambo fulani, wewe ukalifanya hivyo dhambi ya asili ni tendo la tunda kumegwa na kuliwa.

Bible haikusema dhambi ya asili ni tendo, expressly kwa uwazi kwa lengo la staha, ila bible imesema kuhusu dhambi ya asili ni tendo kwa impliedly kuwa kuna tendo fulani lazima litendwe ili mwanamke spate ujauzito ili binadamu mpya azaliwe, tendo hilo ndio dhambi ya asili, ni lazima hiyo dhambi ya asili itendwe na mwanamume na Mwanamke ndipo kiumbe kipya kiumbike!.

Shetani katika kumrubuni Eva, akamwambia wakila tunda, watakuwa na uwezo wa Kimungu wa kuumba viumbe wengine!.

Kuna binadamu mmoja tuu, Bikira Maria, yeye ndiye pekee aliye kingiwa dhambi ya asili kwa kupata mimba kwa uwezo wa Roho Mtakatifu, huku akiwa bado ni bikira bila ile dhambi ya asili kutendwa ya kumegwa kwa tunda, hivyo mtoto Yesu alizaliwa bila dhambi ya asili kutendwa!, na Bikira Maria alisikia dalili ya uchungu lakini alimzaa Yesu bila uchungu, ila baada ya kumzaa Yesu, ndoa yake iliendelea kikawaida na akapata watoto wengine kwa njia ya kawaida.

Kitendo cha kiongozi mmoja wa dini ya wokovu mwenye wafuasi wengi hapa jijini DAR kusema kilichofanyika kule bustani ya Eden ni Uandishi wa habari na kuwa Shetani ni Mwandishi wa habari, hakiwezi kuachwa kipite hivi hivi bila kupingwa.

Kwa sasa tuko katika ulimwengu kimtandao, cyber world ambapo kila mwenye access na mtandao, anakuwa ni mtoa habari na msambaza habari, kwa kuweza kupost chochote kwenye mitandao na kikawafikia watu wengi kwa haraka lakini sio wote ni waandishi wa habari. bali sasa kila mtu ni mpashanaji wa habari!.

Kitendo alichokifanya Mtumishi wa Mungu, Boniface Mwamposa kutangaza kuwa shetani alikuwa ni Mwandishi wa habari, sio kututendea haki sisi waandishi wa habari na tasnia nzima ya habari.
Kwa hisani ya mwana jf JanguKamaJangu Mtumishi Boniface Mwamposa asema "Shetani alikuwa Mwandishi wa habari"

Kitendo hiki cha kusema shetani alikuwa Mwandishi wa habari na kilichofanyika kwenye bustani ya Eden kwenye ile dhambi ya asili ni uandishi wa habari, sio kututendea haki sisi waandishi wa habari na tasnia yetu nzima ya habari. Shetani hakuwa Mwandishi wa habari, wala kitendo kile cha kumrubuni Eva sio uandishi wa habari ni ulaghai tuu katika upashanaji wa habari.

Kufuatia mabaliko ya dunia kuwa ni dunia mtaandao, cyber world sasa kila mtu anaweza kuandika chochote na kusambaza chochote au habari zozote kwenye mitandao na kuonekana kama Mwandishi wa habari, lakini sii Mwandishi wa habari.

Lengo la Mtumishi Mwamposa ni zuri kuhusu umuhimu wa sisi waandishi wa habari ni watu muhimu sana, Ila pia ni watu hatari Sana, pale kalamu zetu zikitumika vibaya zinaweza kuleta majanga makubwa, lakini shetani hakuwa Mwandishi wa habari na kilichofanyika kwenye bustani ya Eden sio uandishi wa habari!.

Kufuatia powers alizonazo Mwamposa, kitendo cha kumuita shetani ni Mwandishi wa habari, kinaweza kikapelekea sisi waandishi wa habari tukaanza kuitwa mashetani!, jee sisi waandishi wa habari, na tasnia nzima ya habari, tunakubali kuitwa mashetani, na tukanyamaza tuu au to demand an apology kutoka kwa Mwamposa kutuomba radhi waandishi kwa kumsingizia shetani kuwa alikuwa ni Mwandishi wa habari, na chanzo cha dhambi ile ya asili pale Bustanini Eden ni Mwandishi wa habari shetani?.

Paskali
 
Mimi bado nakazia hapa msamaha hamstahili kwa sasa
0b2b59c10814f241ccca4dc3f8848660.jpg
 
Kumbe Eva alianza kuonjeshwa tunda na shetani, hapa ina maana walilishana tunda Eva akalipenda akafurahia, hivyo akaenda tena kwa Adam kumlisha tunda lile lile alilolishana na shetani.

Sasa kwa hali hiyo nikisema wanawake asili yao ni kuchepuka nitakuwa nakosea?
 
Wanabodi

Biblia ni kitabu kitakatifu cha dini ya Kikristu, wakati yaliyoandikwa kwenye Bibilia yanatendeka, kuna mengine ni mambo mabaya kabisa hayaandikiki...
Huyo Mwamposa asiwaumize kichwa.. ni nabii wa mchongo jamaa anajihami muda si mwingi mambo yake yatakuwa hadharani

Ameona awandaae kisaikolojia kondoo zake.. kitendo cha kusema shetani alikuwa muandishi wa habari na makondoo yake yakaamini mjiulize ni mambo mangapi anayasema ambayo hayapo kwenye biblia na makondoo yake yakaamini!!

Inasikitisha sana.. na mbaya zaidi nabii akishakuwa fake anajipendekeza kwa serikali ili mapo yakivuja waseme ni kazi ya deep motion
 
Bora hata Anglesea shetani alikuwa CCM.

Huyu jamaa kaidhalilisha taaluma ya Mwanaharakati huru wa Mwendazake aliyedhulumiwa nyumba mheshimiwa sana na mtakatifu Cypranie Funeral
Mwendazake bado anakubutua hata baada ya kufa! Vipi mimba yake hujashusha tu?
 
Mwaposa Yupo sawa kabisa, waandishi hawa hawa ndio wamesababisha machafuko nchi nyingi tu, lakini hawa hawa ndio wanatumia karam zao kugeuza ukweli kuwa uongo kisa matumbo yao, ndio wako mstari wa mbele kuandika lolote ili kumlinda mwenye mamraka na mwenye fedha japo ukweli anaujua! Paschal kaa kimya ,shetani kuwa mwandishi wa habari hakumfanyi kila mwandishi au taaruma yte iwe ya shetani, maana shetani ypo kila sehemu.
 
Kuna waandishi wa vyombo flani vya habari, walilipwa kutoa taarifa ya watanzania waliokuwa wakionewa na wizara nyeti iliyo ajiri watanzania mamilioni, waandishi walipewa usafiri na posho na walifika eneo husika, nakuchukua ushahidi na taarifa toka kwa wananchi waliokuwa wakiilalamikia hyo wizara, lkn baadae kabla ya mda na saa yakuitoa hyo habari wte kwa pamoja wakataka kuongezwa pesa za ziada kwa kigezo kwamba, waziri husika katoa pesa mingi ili kuzima taarifa yao, wale watu walivyokoswa hela yakuongeza taarifa ilizimwa haikutangazwa mpaka leo napesa walishakula na walikataa kurudisha! Bw. Paschal ! Huo siyo USHETANI? Naomba jibu lako.
 
Japo sijasikia hayo maelezo ya Mwamposa,lakini pale bustanini kulikua na "mahojiano" kati shetani na Eva, nafikili hapo ndipo penye msingi wa hoja ya mwamposa kwamba shetani alikua mwandishi wa habari,Mwanzo 3:1,ukianza kusoma hapo shetani alianza kwa kumuhoji hawa kwa swali kwa habari ya matunda ya bustani,..nanyi waandishi si hua mnahoji watu maswali?kwa hiyo inawezekana Mwamposa akawasa sahihi kulingana na kile alichokua anataka kueleza kwa waumini wake.

Pia kuna hoja umezungumza hapo kua wale hawa alifanya tendo la ndoa,hiyo SIO KWELI,kama ni hilo tendo Mungu aliwaruhusu ndio maana akawaambia wakazae waongezeke,maana yake walipewa ruhusa kufanya hilo tendo,Mwanza 2:1 na kuendelea....KOSA LAO ADAMU NA EVA NI KUTOKUTII walichokatazwa na Mungu na ndio maana baada ya pale walifukuzwa bustanini na ule mti wa uzima ukawekewa ulinzi ili wasije wakala tunda la mti wa uzima wakaishi milele.
 
Japo sijasikia hayo maelezo ya Mwamposa,lakini pale bustanini kulikua na "mahojiano" kati shetani na Eva, nafikili hapo ndipo penye msingi wa hoja ya mwamposa kwamba shetani alikua mwandishi wa habari,Mwanzo 3:1,ukianza kusoma hapo shetani alianza kwa kumuhoji hawa kwa swali kwa habari ya matunda ya bustani,..nanyi waandishi si hua mnahoji watu maswali?kwa hiyo inawezekana Mwamposa akawasa sahihi kulingana na kile alichokua anataka kueleza kwa waumini wake.
Pia kuna hoja umezungumza hapo kua wale hawa alifanya tendo la ndoa,hiyo SIO KWELI,kama ni hilo tendo Mungu aliwaruhusu ndio maana akawaambia wakazae waongezeke,maana yake walipewa ruhusa kufanya hilo tendo,Mwanza 2:1 na kuendelea....KOSA LAO ADAMU NA EVA NI KUTOKUTII walichokatazwa na Mungu na ndio maana baada ya pale walifukuzwa bustanini na ule mti wa uzima ukawekewa ulinzi ili wasije wakala tunda la mti wa uzima wakaishi milele.
Uko sahihi
 
Kumbe Eva alianza kuonjeshwa tunda na shetani, hapa ina maana walilishana tunda Eva akalipenda akafurahia, hivyo akaenda tena kwa Adam kumlisha tunda lile lile alilolishana na shetani.

Sasa kwa hali hiyo nikisema wanawake asili yao ni kuchepuka nitakuwa nakosea?
Hakuna maandiko yanayoelekeza hivyo, biblia inasema Tunda na Sio tendo la ndoa. Huu upotoshwaji ndo unaosababisha Kuambiwa ni Shetani😂
 
Kumbe Eva alianza kuonjeshwa tunda na shetani, hapa ina maana walilishana tunda Eva akalipenda akafurahia, hivyo akaenda tena kwa Adam kumlisha tunda lile lile alilolishana na shetani.

Sasa kwa hali hiyo nikisema wanawake asili yao ni kuchepuka nitakuwa nakosea?

Hahaha, kwa kuongezea mkuu, tunajua ndugu Shetani ana mambo ya Kishetani, hatujui kama alichepuka walifanyakipi na kipi hawakufanya.

Masuala ya kiimani kuna namna yanatoa taswira ya changamoto za mahusiano yetu ya sasa.
 
Wanabodi

Declaration of Interest
Mimi ni Mkristu Mkatoliki, ila mara moja moja huwa nahudhuria mafundisho katika madhehebu mbalimbali, ikiwemo Lutheran,
Mwandishi mwenye weledi na alie Makini ,huchunguza Jambo/ kitu kwa kina pasipo kupost.

Mwanzo 3:1-3Biblia Habari Njema (BHN)​

1. Nyoka alikuwa mwerevu kuliko wanyama wote wa porini walioumbwa na Mwenyezi-Mungu. Basi, nyoka akamwambia huyo mwanamke, “Ati Mungu alisema msile matunda ya mti wowote bustanini?”
2. Mwanamke akamjibu huyo nyoka, “Twaweza kula matunda ya mti wowote bustanini;
3. lakini Mungu alisema, ‘Msile matunda ya mti ulio katikati ya bustani, wala msiuguse, msije mkafa.’”


Kama mti wa katikati ni Tendo la ndoa,hiyo miti Mingine ni nini??
Unadhani biblia inaogopa kuongelea Tendo la ndoa? Hadi lipindishe kuandika mti??
Kiukweli Mwamposa Hajakosea!!!

Genesis 3:1-3​

New International Version​

The Fall​

3 Now the serpent(A) was more crafty than any of the wild animals the Lord God had made. He said to the woman, “Did God really say, ‘You must not eat from any tree in the garden’?(B)”
2 The woman said to the serpent, “We may eat fruit from the trees in the garden,(C) 3 but God did say, ‘You must not eat fruit from the tree that is in the middle of the garden, and you must not touch it, or you will die.’”(D)
 
Back
Top Bottom