Kumbe Makongoro anaongea kama baba yake?

Kumbe Makongoro anaongea kama baba yake?

Wala hajanivutia kabisa.

Namwona kama mchekeshaji (comedian) vile.
 
Nilicheka wakati jamaa wanasema tumuenzi mwalimu kwa kumuweka makongoro magogoni... kwa hiyo na mwinyi tutamuenzi.. mkapa.. kikwete... kisha tunarudi tena kwa makongoro..... dash dash mwinyi... then dash dash mkapa..... what a circle......
 
Yetu macho na masikio.
Ninachotaka mimi ni kiongozi bora bila kujali anatoka wapi na ana jina gani.

Chugio la kamati kuu ndio mpango mzima wa kumpata mgombea uraisi wa CCM.Kamati kuu ndio mwiba sio utilili wa wenye nia.Kama ingekuwa Marekani demokrasi ingechukua mkondo wake,lakini hii ni Tanzania.Sishangai ukasikia Makongoro atakuwemo kwenye finalist japo uwezo au upeo wake haueleweki vizuri kwa walio wengi
 
ila sijaona ambacho ameonngea zaidi ya pumba na ushabiki shabiki tu . badla ya kujadili hoja yeye anajadili watu. angeenda kujiuza na si kuwapiga madongo wenzake. kiukweli anaonekana ni mhuni mhuni tu hana uwezo wowote basi tu. labda ccm iamue kumbeba.... na hata angefanana na nyerere bado si sifa tunayoitaka.,kama sautu inafanana na nyerer sisi inatusaidia nini? kwan sisi tunataka mwigizaji wa sehemu ya kuongea nyerere wenye movie? aende zake huko ...mhuni mhuni tu chapombe na hajaonge hoja yoyote zaidi ya kufanya ucomedy.

hapo pekundu unaposema sisi unamaanisha wewe na nani? je umepewa haki ya kuwazungumzia wengine na nani?, jitafakari!!!!!!
 
LIKUD

Sikuhizi kaacha yale maji maupe yanayokatazwa kutumiwa?
 
Last edited by a moderator:
ila sijaona ambacho ameonngea zaidi ya pumba na ushabiki shabiki tu . badla ya kujadili hoja yeye anajadili watu. angeenda kujiuza na si kuwapiga madongo wenzake. kiukweli anaonekana ni mhuni mhuni tu hana uwezo wowote basi tu.

labda ccm iamue kumbeba.... na hata angefanana na nyerere bado si sifa tunayoitaka.,kama sautu inafanana na nyerer sisi inatusaidia nini? kwan sisi tunataka mwigizaji wa sehemu ya kuongea nyerere wenye movie? aende zake huko ...mhuni mhuni tu chapombe na hajaonge hoja yoyote zaidi ya kufanya ucomedy.

Lakini hivyo ndivyo wafanyavyo chadema,lawama nyingi kwa ccm basi.
 
Kwa jambo hili mfano wa marekani ni sahihi kabisa kwa watu wenye fikra mgando kwa watoto wa viongozi wastaafu kugombea. Je ukiwa mtoto wa mhandisi ni dhambi kurithi kazi ya mzazi kama una sifa? Tuache ukenge..hivi mwanaume gani lijari ambaye hapendi wanawake? Msitufundishe ushoga..p.

Wengine kwa jinsi wapendavyo wanawake wameiba hadi wanawake wa watu.
 
Sentensi kumi za Makongoro Nyerere kuhusu yeye na wanawake, ulevi na kutangaza nia (Sauti)..

View attachment 256683

Headlines zenye stori za Siasa zimeendelea kutawala. Makongoro Nyerere ni Mbunge anaewakilisha TZ kwenye Bunge la Afrika Mashariki, nae alikuwa nyumbani kwao Butiama, hapa nimenukuu sehemu ya kile aichokisema akiwa huko.

“Nina nia ya kutangaza nia lakini bado sijatangaza nia… kwanza tuzungumze kuhusu utaratibu wa CCM. Mkutano Mkuu utakaa tarehe 11 na 12 June ili kuisikia Rasimu ya Chama, kuithibitsha na kuipitisha… Sizuki na kuanza kuzungumza kabla ya ilani ya Uchaguzi.. Wanaoamua nani awe kiongozi sio huku kwenye Chama, ni Watanzania…“ Makongoro Nyerere.

Kwenye sentensi nyingine akasema hivi kuhusu wale wanaomzungumzia “Huyo mtoto wa Nyerere huyo ni mlevi kweli… mmewashtukia au vipi??. Huyo mtoto wa Nyerere huyo anapenda wanawake kweli.. sasa mlitaka nipende wanaume? Nawapenda kweli na mimi nashukuru MUNGU mnanipenda kweli” Makongoro Nyerere.

Makongoro Nyerere akamalizia hivi “CCM sio chama cha vibaka, ni chama cha walio wengi.. wakulima na wafanyakazi.. turudishieni chama chetu, mnaenda nacho wapi? Kufanya nacho nini? Alafu sisi mtuache wapi?”

Utamsikiliza kwa urefu zaidi kila alichokisema kwenye sauti hii (hapo chini) mtu wangu;

View attachment 256682

Chanzo: Millardayo.com

Umesikia kicheko chake?
 
Back
Top Bottom