Kaa la Moto
JF-Expert Member
- Apr 24, 2008
- 7,903
- 1,053
Juzi katika kupita pita kwangu nilijikuta kwenye banda la muuza magazeti na nilikuta rundo la magazeti mengi ya kila aina. Mengine hata titles zake ndio mara ya kwanza kuziona, na mimi nilikuwa nikitafuta gazeti la mwana halisi na raia mwema ya wiki hii maana siyapati kirahisi mtandaoni.
Bahati mbaya sikuyapata. Nilikuta yamekwisha. Nilianza kumlaumu sana muuza magazeti kwa kuleta magazeti hayo kidogo. Lakini alinijibu kuwa si kweli kwamba yanakuja kidogo bali yananunuliwa kwa wingi na haraka.
Katika mazungumzo yangu huku nikimtafiti aliniambia mpaka leo hajajua kwa nini baadhi ya magazeti mengi anayouza hayanunuliwi kama baadhi ya magazeti ambayo alikiri yananunulika kwa kasi ya ajabu.
Bila kujua kwamba namtafiti alinitajia magazeti ambayo yana kasi kubwa ya kununuliwa kuwa ni MWANAHALISI, RAIA MWEMA, MWANANCHI, na TANZANIA DAIMA. aliniambia kuwa pia kwa mbali kidogo NIPASHE na MAJIRA yanajikongoja lakini mengine hayana mvuto na anayauza kwa shida sana. Kunithibitishia hilo alinionyesha rundo la magazeti ya mtanzania, rai, tazama, uhuru, daily na sunday news, habari leo na mlolongo mwingi wa magazeti ambayo aliniambia hayaendi kabisa.
Katika kuendelea kumtafiti alisema hana uhakika kwa nini hayanunuliki vizuri hayo magazeti, lakini akasema anadhani mengi ya magazeti hayo yanaonekana kutumika kumpaka matope Dr Slaa. Mie nilipomuuliza kwamba kwa kumsema ovyo Dr Slaa si basi yangeweza kununulika sana? jibu lake lilikuwa hata yeye anashangaa maana alitegemea hivyo.
Conclusion yangu ikawa hivi kumbe hata watu wameshavichoka vigazeti hivi ambavyo vinajenga negative image kwa Dr Slaa?! Na hapo kwa nini yale yasiyosema lolote mbona yananunuliwa? nika conclude kuwa watu kumbe wameshachoka na uongo na sasa wanapambanua uongo na ukweli.
Hii ni indicator kwa waandishi, wahariri na wamiliki wa vyombo vya habari kwamba mnajimaliza wenyewe kwa kutumiwa na vyama vya siasa ili mpake matope vyama vingine. Watu wanaanza kuwabaini na kuyaponda magazeti yenu. Shauri yenu, ingawa kwa sasa mnalipwa na mafisadi, hata baada ya uchaguzi watu hawatayaamini na hawatatamani kuendelea kusoma udaku wenu. Na mwisho mtajimaliza wenyewe kama uhuru na mzalendo walivyokwisha.
Kama waweza fanya utafiti wako pia katika jambo hili. Utaona ukweli wa jambo nililokutana nalo jana.
Bahati mbaya sikuyapata. Nilikuta yamekwisha. Nilianza kumlaumu sana muuza magazeti kwa kuleta magazeti hayo kidogo. Lakini alinijibu kuwa si kweli kwamba yanakuja kidogo bali yananunuliwa kwa wingi na haraka.
Katika mazungumzo yangu huku nikimtafiti aliniambia mpaka leo hajajua kwa nini baadhi ya magazeti mengi anayouza hayanunuliwi kama baadhi ya magazeti ambayo alikiri yananunulika kwa kasi ya ajabu.
Bila kujua kwamba namtafiti alinitajia magazeti ambayo yana kasi kubwa ya kununuliwa kuwa ni MWANAHALISI, RAIA MWEMA, MWANANCHI, na TANZANIA DAIMA. aliniambia kuwa pia kwa mbali kidogo NIPASHE na MAJIRA yanajikongoja lakini mengine hayana mvuto na anayauza kwa shida sana. Kunithibitishia hilo alinionyesha rundo la magazeti ya mtanzania, rai, tazama, uhuru, daily na sunday news, habari leo na mlolongo mwingi wa magazeti ambayo aliniambia hayaendi kabisa.
Katika kuendelea kumtafiti alisema hana uhakika kwa nini hayanunuliki vizuri hayo magazeti, lakini akasema anadhani mengi ya magazeti hayo yanaonekana kutumika kumpaka matope Dr Slaa. Mie nilipomuuliza kwamba kwa kumsema ovyo Dr Slaa si basi yangeweza kununulika sana? jibu lake lilikuwa hata yeye anashangaa maana alitegemea hivyo.
Conclusion yangu ikawa hivi kumbe hata watu wameshavichoka vigazeti hivi ambavyo vinajenga negative image kwa Dr Slaa?! Na hapo kwa nini yale yasiyosema lolote mbona yananunuliwa? nika conclude kuwa watu kumbe wameshachoka na uongo na sasa wanapambanua uongo na ukweli.
Hii ni indicator kwa waandishi, wahariri na wamiliki wa vyombo vya habari kwamba mnajimaliza wenyewe kwa kutumiwa na vyama vya siasa ili mpake matope vyama vingine. Watu wanaanza kuwabaini na kuyaponda magazeti yenu. Shauri yenu, ingawa kwa sasa mnalipwa na mafisadi, hata baada ya uchaguzi watu hawatayaamini na hawatatamani kuendelea kusoma udaku wenu. Na mwisho mtajimaliza wenyewe kama uhuru na mzalendo walivyokwisha.
Kama waweza fanya utafiti wako pia katika jambo hili. Utaona ukweli wa jambo nililokutana nalo jana.