Precious Diamond
JF-Expert Member
- Jun 9, 2023
- 397
- 993
Kwenye mazungumzo yaliyofanyika club house Dr. Slaa amesema kwa utaratibu anaoufahamu Rais hana mafungu makubwa kiasi hicho (milioni 150) kwaajili ya eneo moja, na fedha hizi zinawekwa katika kifungu cha Ofisi ya Rais na balaa ni kwamba fedha hizi hazikaguliki kwasababu fungu la 23 la Ikulu halikaguliwi na CAG!
Kwa maana hiyo chochote kitakachofanyika inabaki kuwa siri ya Ikulu, siri ya Rais. Jambo hili kama ni kweli Rais ametoa mfuko binafsi hatuwezi kuziingilia lakini kama ametoa kwenye mfuko wa 23 (kama sijakosea) ni lazima watanzania tulipigie kelele, hili si sahihi huu ni wizi, huu ni ubadhirifu na matumizi mabaya ya fedha za umma kwa kazi mambazo hazijaidhinishwa na bunge wala hazijawahi kuidhinishwa na bunge miaka yote tangu uhuru wetu mpaka leo, marais wamepita wengi hatujawahi kuona kitu cha namna hii.
Ni jambo la kusikitisha, tuendelee kulipigia kelele kwasababu tusipopiga kelele hii imeshapanda kuwa milioni 150, kesho itafika bilioni moja, kesho kutwa itafika bilioni 3!
Kwa maana hiyo chochote kitakachofanyika inabaki kuwa siri ya Ikulu, siri ya Rais. Jambo hili kama ni kweli Rais ametoa mfuko binafsi hatuwezi kuziingilia lakini kama ametoa kwenye mfuko wa 23 (kama sijakosea) ni lazima watanzania tulipigie kelele, hili si sahihi huu ni wizi, huu ni ubadhirifu na matumizi mabaya ya fedha za umma kwa kazi mambazo hazijaidhinishwa na bunge wala hazijawahi kuidhinishwa na bunge miaka yote tangu uhuru wetu mpaka leo, marais wamepita wengi hatujawahi kuona kitu cha namna hii.
Ni jambo la kusikitisha, tuendelee kulipigia kelele kwasababu tusipopiga kelele hii imeshapanda kuwa milioni 150, kesho itafika bilioni moja, kesho kutwa itafika bilioni 3!