Aaa wapi aitoe wapi?. Angalau hata angekuwa bikra Mara mia . Nina rafiki mwingine anafunga ndoa mwaka huu. Kaenda vijijini kaopoa standard seven kitu kibichi na kiko bado karatasini hakijaguswa kwa laki sita tu pungufu anaongea . Tunakalia na baadhi wa mjini wenye akili kama za huyu. Pyuuu!.
Jamaa yuko njia panda hapo awali hadi hivi sasa binti anaonesha upendo kwa jamaa ila hili ndilo linalomstua jamaaa amekubali la Pete amechukua vipimo vya kidole tiari Leo ndio nilikuwa nampeleka kwa sonata ila nimemshauri aache kwanza tumtathimini binti kwanza . Maana kama huu ni mwanzo kweli jamaa ataiona hela mwanamke ndani ya nyumba?. Anamwambia ati huko mbeleni watasaidiana ila si katika hili mh!. Kweli kuna future hapo?. Alafu anampiga jamaa ban asiombe ushauri kwa rafiki zake Bali mambo wayamalize wao wenyewe mh!. Ama anadhani friend wangu hawezi back out?.
Fungukeni wajumbe jamaa apone. Maana maisha ya ndoa si lelemama hata kidogoo.
Huyo jamaa, hata kama atamchukua huyo binti waishi kwa pamoja, hiyo ndoa itakuwa ndoano na mwisho wa siku haitadumu.
ni jukumu la mwanaume kuhusika na malipo au gharama zote zinazohusiana na mahari.
wanaume tunakuwaga na kashfa sana endapo mwanamke atahusika kuchangia mahari kwa jinsi yoyote ile.
kama huyo kijana anayetaka kuoa hajajipanga basi atulie lakini sio kumsemea mbovu binti wa watu.
na wewe mleta mada mbona unatoa majibu kama ndie muoaji?
stay away from this halikuhusu kihivyo.
hah hah hii imenigusa asee.. kuna mtu anadai tuchange nusunusu atoe mahari kwetu..hapa anatishia kuniacha kwa ishuz za mshahara.. hata pete sijavishwa, ndani sijawekwa ANAPIGIA MAHESABU MSHAHARA WANGU... ooh noo noo nooo.!!! no kubwa.
huyo binti yuko sahihi asilimia mia. hasimpe huyo mwanamume hata shilingi moja
Alafu akagongwe na baboons?. Unajua nyakati zimebadilika sana ikiwa ni hivyo hata mama kununua nguo za watoto asihusike, kuchangia ada za watoto uwe mfuko wa baba ilihari mama anakazi na mshahara anapata, bill zote baba huku mwanamke akitumia fedha kutengeneza kucha na kusuka nywele. Kuna baba mmoja alikuwa analalamika mkewe anaomba mpaka pesa ya chumvi huku akiwa na kazi yake nzuri tu na pesa anapata. Hilo limama muda wote likiulizwa pesa zinakwenda wapi linanuna siku nzimaa. Hii ni sawa?. Wanawake wako wengi wengine wajane wanatafuta vijana wawalee tena kwao fedha si shidaa kabisaa. Kuna jimama moja lilipoteza funguo za nyumba kwenye kama saa nne usiku akanikuta maskani anatafuta fundi nikasema Mimi sio fundi acha aniombe nikamsaidie nikakubali Mlango ukaitika khe mama wa watu kumbe yu single acha aanze mapozi yake ya ajabu ati ananipa elfu hamsini nikamchongee ufunguo na kumi elfu usafiri wa boda boda nikamwangaliaa nikacheka kimoyo kimoyo nikajisemea mwenyewe angalijua mimi ni nani asingefanya yote hayo akaomba namba za Simu ili kesho yake anistue mapema asubuhi kwa hiyo kazi nikampa nilimfanyia kazi yake na nikarejesha fedha zote zilizobaki ati akaniambia zinifae kwa kazi niliyofanya nikakataa Kata kata nikaishia zangu mpaka Leo kimnya sijamtafuta wala nini . Alafu kije kibinti kilete shida .