Kumbe mabinti ndivyo mlivyo?

Kumbe mabinti ndivyo mlivyo?

Yaani Mkuu umeshindwa kulipa mahari mpaka unataka binti ajilipie mahari? Hii ni mpya, yaani binti ajichumbie mwenyewe? Kazi boot Mkuu uliyataka mwenyewe!
 
Hapo anakumbatia fuko la nyuki,ngoja lipasuke ndani ya ndoa aanze kushambuliwa! Hata kama hajui kusoma picha haoni??? Mwambie atoke nduki akimbie mbayaaa...hapana entertain utumwa wa badae kabisa
 
Huyo jamaa kilaza!!!
Sasa wewe unauliza kama mabint ndivyo walivyo ujibiwe nini?
Yaani jamaa yako kukosa msimamo ndio uwatie doa mabint?
Ndio maana enzi zetu mahari walilipa wazazi wa mume baada ya kujiridhisha kuwa kijana wao anastahili kupewa mke!
 
Uwiiii yani binti anajua kabisa jamaa yake hayuko vizuri afu anataka makuu ivo? huyo akifika ndani si ndo atataka nguo, viatu hadi vyakula vya bei ghali? Hahaaa aliimba Jose Chamelione anataka fitu fya bei kali kama hajui eti sina mali......
Huyo si mke utakuja kuikimbia ndoa, ndoa ni kusaidiana na si kukomoana.
 
Mwambie rafiki yako ajipange ndoa yahitaji pesa nyingi.Huwezi niambia eti nikusaidie hela ya mahari hata siku moja huyo mdada yuko sawa kabisa
 
Jamaa yuko njia panda hapo awali hadi hivi sasa binti anaonesha upendo kwa jamaa ila hili ndilo linalomstua jamaaa amekubali la Pete amechukua vipimo vya kidole tiari Leo ndio nilikuwa nampeleka kwa sonata ila nimemshauri aache kwanza tumtathimini binti kwanza . Maana kama huu ni mwanzo kweli jamaa ataiona hela mwanamke ndani ya nyumba?. Anamwambia ati huko mbeleni watasaidiana ila si katika hili mh!. Kweli kuna future hapo?. Alafu anampiga jamaa ban asiombe ushauri kwa rafiki zake Bali mambo wayamalize wao wenyewe mh!. Ama anadhani friend wangu hawezi back out?.

kiukweli haitakiwi dada atoe hela sasa hivi yaani asaidie pete yake plz!sema tu asiogope mahari aimalizwagi unakubali tu italipwa majaliwa kinatolewa kilichopo., ila mwanamke kusaidia jamani ni hatar yaani kumgharamia ajickie na yeye amependwa kweli ni muhimu.ndoa ni kujiandaa jamani c kukurupuka na kumwacha mtu ulomwahidi utamuoa ni kumuumiza tu labda wazazi wakatae kuchukua kilichopo
 
Yaani Mkuu umeshindwa kulipa mahari mpaka unataka binti ajilipie mahari? Hii ni mpya, yaani binti ajichumbie mwenyewe? Kazi boot Mkuu uliyataka mwenyewe!

Si kwamba jamaa anashindwa kujilipia la hasha bado ni mwanafunzi na kazi ni ya mkataba pia binti anakibarua. Kijana kajikisanya kwa takribani miezi mitatu kafikia kiasi cha mahari ila vitu kama blanket ya bibi, vitenge, na kakoti kaomba Dada amsaidie hapo hapo jamaa kakopa pesa somewhere pesa ya kuchongesha pete ya engagement gram mbili ya dhahabu hapo awali alitaka gram tatu jamaa akagoma mbaya hivi sasa jamaa anakabiriwa na safari ya kuvuka mikoa ka nane kwenda kutoa mahari hiyo nayo ni nauli mjumbe. Mapenzi haya mh!. Hapo hapo demu hajawahi msaidia jamaa chochote akiwa chuoni ati fedha zake anasomesha Mdogo wake. Hana lolote alilowekeza maisha mwake anakuja kwa jamaa mtupu na nguo zake tuu. Hii ni sawa wajumbe?.
 
Hiiiiiivi!!! Huyu nae n mwanamke wa kuoa kwel??? Manake kwanza n mwongo,mbil ni mbinafsi,, tatu anatake akutawale bdo mapema yan ana mashart ka EMF nyooooooo ebu mwambie umeahrisha hyo ndoa had utafte iyo milion moja yao
 
Kuna wanawake wengine wanakera aisee.

Nikitulia sana namshukuru sana Mungu kwa kunipa mke ambaye hapendi na ha'support' makuu.
 
Ukweli ni kwamba hata kuku tu hana akili fupi kama ya uyo dada mwenzetu!! Mtu ambaye kweli umemzimikia huwezi mfanyia upumbavu kama huo mie naita upumbavu, so ata asijipe jasho saana, ki ukweli kwa mawazo yangu huyo dada hajampenda ko aangalie tu ustaarabu mwingine!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom