Kumbe Kanali wa Jeshi ni cheo kikubwa kuliko cheo cha IGP

Sio kweli umeona vibaya angakia vizuri wakati mh rais anasilimiana na wageni kwa kupeana mikono kabla hajamfikia igp siro kushoto kwa siro alikuwepo mabeyo baada ya mabeyo kumpigia saluti mh rais na rais akasogea kwa siro wakati siro anapiga saluti muda huo huo yule kanali wa jeshi alikuwa amempigia boss wake (mabeyo)saluti hivyo mkono wa kulia wa kanali ukaendana na saluti ya siro akimpigia rais hivuo ukiangalia vibaya unaweza sema ni kweli siro kampigia kanali saluti lakini sio.
Sory nilikuwepo ndo mana nakuelewesha hivyo.
Aaah...! Muongo ulikuwepo wapi?
 
We nawe sijui huelewi au unajaribu kutafuta ligi bila logic.

Sasa kama ADC alipigiwa saluti na IGP au hao wengine kwanini hakujibu kwa saluti ilihali alivaa uniforms?
Ukiona amekakamaa ujue alikua anajiweka attention pale ambapo mkuu wake (rais) anapigiwa saluti, na iko ivo kijeshi.
Ukiwa na boss wako akasalimiwa mbele yako wewe inabidi ukakamae kama ishara ya kuheshimu salamu ya kijeshi inayopokelewa na boss wako ndio maana ADC hakujibu kwa kupiga saluti maana anayesalimiwa sio yeye.

Mtu hupokea saluti kwa kukakamaa endapo hajavaa full uniforms, labda hana kofia n.k au yuko kiraia (nguo za kiraia), otherwise pale alipokuwa ADC kama alipigiwa saluti yeye lazima angejibu kwa saluti.

Au bado una morale ya ligi?
Mkuu wa magereza alipiga kwa Rais na Mpambe wa Rais video zipo angalia vizuri, na kwa kifupi alipofika kwa Kamishna wa Magereza Mpambe wa Rais ni kama alikuwa anajua lazima apewe heshima yake alijiandaa kabisa na uso wa mbuzi aliweka
 
Wewe huelewi kitu.
Toka lini Colonel akawa mkubwa kwa Mkuu wa Jeshi la Magereza?.
Yaani Kanali ambaye hana hata uwezo wa kuwasiliana moja kwa moja na Mkuu wa Majeshi awe sawa na Mkuu wa Magereza anayewasiliana moja kwa moja na Rais?.
Punguzeni bangi vijana.
Chain of command mkuu. Kanali anaweza asiwasiliane direct na CDF ingawa sina hakika kwasababu ana watu juu yake.

Mkuu wa Mkoa anawasiliana direct na Rais lakini Waziri hawezi kuwasiliana direct na Rais lazima apite kwa Waziri Mkuu. Je mkuu wa mkoa na Waziri yupi ni mkubwa??
 
Hajampigia Salute bhanaa...!! Kanali alipofika kwa Sirro aliinama kidogo tu bhasii.
sawa unachotakiwa unatoa saluti moja tu km kuna viongozi wangi wa kijeshi na unampigia mwenye cheo cha juu kabisa kwa niaba ya wenzake anaipokea.
Afisa wa Magereza hakumpigia Kanali ndio maana hakuipokea
 
Kitaalamu ni Kwamba Saluti ya kijeshi ikipigwa kwa mwanajeshi aliyekatika uniform naye atajibu kwa salute sio kwa kubana mikono.
Kama huyo Kanali hakujibu kwa kupiga Saluti ina maana hiyo salami haikuwa yake.
Lakini mbona inaonekana dhahiri kwamba alimgeukia Kanali na kumpigia??

Naomba uangalie hii video mkuu. Ili usijichose angalia kuanzia dakika ya 21 mpaka 23. Nita appreciate kama utafanya hivyo sababu nimeona atleast wewe umekuja na majibu yanayoeleweka..

 
Mkuu wa magereza alipiga kwa Rais na Mpambe wa Rais video zipo angalia vizuri, na kwa kifupi alipofika kwa Kamishna wa Magereza Mpambe wa Rais ni kama alikuwa anajua lazima apewe heshima yake alijiandaa kabisa na uso wa mbuzi aliweka
Asante mkuu.. kuna watu sijui wamelishwa nini. Wao ni kupinga tu..

Colonel alivyofika kwa Mkuu wa Magereza alisimama kabisa kungoja heshima yake. Na Kamishna wa Magereza akatoa saluti. Watu wanabisha hapa ingawa hata tukio hawakuliona lakini pia hata video zilizowekwa hapa hawajaangalia..
 
Utaratibu kijeshi kabla hujaongea na mkuu wako lazima umpigie saluti na ukishamaliza kuongea nae lazima umpigie saluti tena, au mkuu wako anapokaribia (kama anatembea) sehemu ulipo lazima umpigie saluti vile vile hata wewe unapomkuta njiani lazima umpigie saluti pindi unapo mkaribia.

kwa scenario hiyo mpambe wa raisi alikuwa anataka kuongea kidogo na CDF ndo maana akampigia saluti then wakaongea mawili matatu, kwa IGP, mkuu wa usalama na mkuu wa magereza, hawa wote wamempigia saluti raisi na sio mpambe wa raisi ndio maana mpambe wa raisi hakujibu salute zao, kwasababu anajua yeye ni mdogo kwa wale.


Mkuu wa magereza baada yakumaliza kushikana mikono na raisi alimpigia tena saluti kwa mara ya pili (kama kushukuru) na hapo ndipo mpambe wa raisi alikuwa karibu yake, so kama mpambe wa raisi angekua mkubwa kicheo kumzidi mkuu wa magereza angemjibu kwa kupiga saluti ila hakufanya hivyo, maana hastahili kupigiwa hiyo saluti bali hiyo saluti alipigiwa raisi baada yakumaliza kusalimiana nae.

kanali ni mdogo kicheo hata kwa kamishna wa polisi.
 
Asante mkuu.. kuna watu sijui wamelishwa nini. Wao ni kupinga tu..

Colonel alivyofika kwa Mkuu wa Magereza alisimama kabisa kungoja heshima yake. Na Kamishna wa Magereza akatoa saluti. Watu wanabisha hapa ingawa hata tukio hawakuliona lakini pia hata video zilizowekwa hapa hawajaangalia..


Si kweli mkuu, ile salute angekua kapigiwa mpambe wa raisi basi na yeye angeijibu kwa kumpigia salute pia, maana afisa yoyote anapokuwa kavaa kofia akisalimiwa/salimia lazima apige saluti.


mkuu wa magereza ni mkubwa kuliko kanali, mkuu wa magereza naweza kumfananisha na major General wa jwtz.
 
Chain of command mkuu. Kanali anaweza asiwasiliane direct na CDF ingawa sina hakika kwasababu ana watu juu yake.

Mkuu wa Mkoa anawasiliana direct na Rais lakini Waziri hawezi kuwasiliana direct na Rais lazima apite kwa Waziri Mkuu. Je mkuu wa mkoa na Waziri yupi ni mkubwa??
Chain of Command ndio inayotuonyesha nani mkubwa kati ya Mkuu wa Magereza na Colonel.
Katika Baraza la Mawaziri Chain of command inatuonyesha Waziri yupo karibu kuliko Mkuu wa Mkoa.
Katika ugh'atuaji wa Mamlaka ya Serikali,Chain of Command inatuonyesha Mkuu wa Mkoa yupo karibu na Rais ijapokuwa Waziri wa Tamisemi naye atahitajika hapo.
Tunapokuja Majeshini,Chain of Command inaonyesha Mkuu wa Magereza yuko karibu sana na Rais kuliko Kanali.
 
Si kweli mkuu, ile salute angekua kapigiwa mpambe wa raisi basi na yeye angeijibu kwa kumpigia salute pia, maana afisa yoyote anapokuwa kavaa kofia akisalimiwa/salimia lazima apige saluti.


mkuu wa magereza ni mkubwa kuliko kanali, mkuu wa magereza naweza kumfananisha na major General wa jwtz.
Mkuu huwezi kufananisha vitu ambavyo havifanani. Jeshi la Wananchi ni tofauti na Magereza, Polisi.

Kila mmoja ni mkubwa kwake. Hakuna sehemu yeyote inayoonyesha Cheo fulani jeshini ni sawa na kingine jeshi jingine.

Kama ipo iwekwe hapa tuione.
 
nilikuwa makini sana hapo mleta mada hukuona vizuri raisi alipofika kwa IGP ndo IGP akatoa saluti lakini mpambe hakutoa saluti isipokuwa rais alipokuwa kwa mkuu wa majeshi mpambe wa rais nae alitoa saluti kwa mkuu wa majeshi
Yap ndivyo ilivyokua.
 
Back
Top Bottom