Karucee
JF-Expert Member
- Mar 11, 2012
- 18,174
- 34,405
Ni kinyume na imani kuu
Haya mambo yametajwa hata kwenye vitabu vitakatifu.
Jiongeze.
Ni kinyume na imani kuu
Haya mambo yametajwa hata kwenye vitabu vitakatifu.
Jiongeze.
Imani inapokuwa mzigo...!!!
Na tumeamriwa tuyakemee kwa jina la aliye juu.... Tusiyafuge
Anakufanyia bila wewe mwenyewe kujua kwahiyo madhara yapo palepale
Yai viza ni kitu kisichofaa kimekufa kinanuka hakina uhai...yai viza hutumiwa sana na wachawi wenye roho mbaya kuharibu maisha ya mtu..ni mojawapo wapo ya uchawi mbaya kabisa kulogewa nao
Mara nyingi hunuizua maneno kama haya ....kama hili yai lisivyo na uhai ....kama hili yai lisivyo na faida...kama hili yai linavyonuka...
Kisha baada ya manuizi hayo hupasuliwa njia panda ili litawanyike pande nane za uso wa dunia ili kila utakapoenda utakalofanya lisifanikiwe na uchukiwe na kukimbiwa na kila mtu....hata ulikuwa una mafanikio kiasi gani ghafla hujikuta unaanguka na nuksi balaa na mikosi kukuandama
NB: Sifundishi uchawi bali najaribu kuelezea ubaya wa kitu fulani kama hiki ili siku ikitokea kuna mtu kakuudhi usimfanyie jambo baya kama hili bali mwachie Mungu kwakuwa yeye ndio mwamuzi wa haki
Na wewe kama kuna mtu kajaribu kukufanyia hivi Usijaribu kwenda kwa waganga wa kienyeji kwakuwa huko unaenda kutafuta balaa zaidi la viapo na maagano ambavyo unaweza kuja kushindwa kuvitengua
Mwachie Mungu kwakuwa hata juju liweje huwa lina kikomo cha kuishi na kufanya kazi expire date
mkuu, yai viza linazo kazi nyingi tu, kuna mkoa yanauzwa bei mbaya, linatumika kutegea kenge, linachemshwa halafu anawekewa kenge asivyo na akili yeye huwa ni kumeza na kulipasulia tumboni, hapo ndo huuingia mkenge.
mimi kuna watu wanapitaga kwa watu tunaoangua vifaranga na kuomba tuwauzie mayai viza kumbe ndiyo wanaenda kudungulia watu future zao... yule jamaa alinidanganya eti wanaenda kutengenezea sumu ya kuua wadudu ...
Kumuomba Mungu tu
duh basi ni hatariKamwe hawawezi kukwambia ukweli ni kama hiyo ya kenge wanaficha ukweli kuna jinsi nyingi za kumtega kenge
Facts ni nyingi unaweza kufanya sana ibada lakini ukawa na roho mbaya.....haitakusaidia