Kulikoni ndoa za siku hizi?

Kulikoni ndoa za siku hizi?

Ni hizi ndoa kuanzia 2010 ndio zinaongoza kuparaganyika
Bro kwa ufupi wengi tunapenda kwaito nazawadi tutakazo pewa siku ya harusi na kuwatambia marafiki kuwa nawewe una mke/mume basi,Haya mambo yapo mjini sana.
nilichogundua wanachanganya ndoa na harusi
 
Ndoa za sasa zipo kwa mihemko tu ya kupendeza siku ya harusi, pete yangu ya tanzanite na whitegold, nitakavyobadilisha nguo siku ya harusi kanisani shela ukumbini gauni nimeagiza dubai, bwana harusi anavyojua kuvaa na kupangilia rangi na wale marafiki zake watakavyoingia kwa mbwembwe, mtu hawazi baada ya kuachwa hotelini unakuwa mama au baba kila kitu kinawahusu tena mkijadiliana kwa pamoja siyo baba anawaza kununua kiwanja mke anawaza kuchukua mkopo wa kununua vitz ili awaambie mashostito baada ya ndoa tu akanipa gari, kumbe gari kakopa na mgogoro kwenye ndoa ukaanzia hapo kila mara mnapishana kauli kwa kuwa mwanaume ulitaka kuoa msomi siyo mke anaamua anavyotaka, uliacha kumuoa mke mwenye heshima kisa wewe unamzidi elimu hamtaendana, haya sasa umempata huyo kama wewe yeye anajua usawa tu hamsini kwa hamsini, mwanamke ni mwanamke tu itabaki kuwa hivyo mavyeo yako ukifika home yaache mlangoni tena getini kabisa ukiingia ndani wewe ni mke mtii mumeo, wengine eti wanasema usizoee kumuaga mumeo mpe taarifa tu ndoa inakufa hiyo kwenye ndoa kuna mke zaidi ya mmoja ila siyo mume zaidi ya mmoja, na wazazi nao wanachangia siku ya send off mwanangu chumba chako hakijapangishwa ukiona anakutesa rudi tu maneno gani hayo kweli akiona mwanaume kachepuka kesho kwao, wanaume mfanye kazi mlete chakula nyumbani usitegemee sana hela ya mwanamke hawajaumbwa kutoa, ndo mana bibi na mama zetu walidumu hawakupewa majukumu makubwa ndani.
 
Kwa upande wangu wahusika kuwa na yafuatayo.
1.faithful
2.Being honest to each other
3.kuchukuliana
4.true love
Tatizo haya mambo kuyapata kibongo bongo Ni ngumu kishenzi...
 
nani anataka kuishi na Malaya aje aletewe miwaya ndani!! wacha waachane tu.

na usiseme wanawake wanalipiza, sema wanaenda kutafuta furaha yao. unafikiri ni maboksi hawana hisia au wana mioyo ya chuma? aishi maisha yake kumlilia MTU ambaye hamjali? acha tu watafute furaha nao.

ukisema tu ndoa ina miaka thelathini wala hunivutii, hadi nijue ni ndoa kweli ama vepee! sio sifa kusema tu ndoa INA muda mrefu wakati wahusika hawafurahii, mnafurahia nyie watazamaji!
taratibu wewe binti acha hasira bhasi dada mzuri, siku ukipata right man hutasema hayo.
 
As if kukaa muda mrefu kwenye ndoa means anything.

Kuna ndugu yangu ndoa ina miaka 15. Lakini kutwa analalamika mume wake anavyomnyanyasa (kupigwa na kutukanwa).

Yeye furaha yake ni kuwa kakaa kwenye ndoa miaka mingi...ni role model wetu..... Hahaha.

Kuna siku waligombana na mumewe nikiwepo. Ile scenario mpaka leo nikiikumbuka huwa siamini na hunipa hofu sana.

Mdada akaniambia hapo ilikuwa kawaida tu. Inakuwaga timbwili kweli kweli, mpaka watoto hujificha...mh

Ila haya mambo naona hutegemea na mtu pia. Kuna watu wastahimilivu sana.
kabisa. watu we are wired differently. hiyo pamoja na uelewa/imani ya MTU. some people genuinely believe wanafanya ibada wakikaa matesoni!!

waje wafanye utafiti bongo za watu wanaokubali/vumilia mateso na wenye zero tolerance. our brain structures must be different.

Reina princess why your ndugu fight in front of their kids?? hawajui sio vizuri?
 
.
Ishu ya feminism pia inawaharibu wanawake wengi sana. Wanawake tusijidanganye, hatuwezi kua sawa na wanaume. Ndio una elimu yako na kazi yako ata kama unaingiza kipato zaidi ya mwanaume inabidi umpe heshima yake mume wako. Mwache mwanaume awe kichwa... Usimlinganishe na wanaume wengine na husimfanye akajiona hana thamani.
what has feminism have to do na ukosefu wa heshima??

usituchafulie harakati tafadhali, kama MTU hana heshima, hajui kushauriana na watu ni character yake mwenyewe, nothing to with feminism.

na hii heshima inayoongelewa ni kitu gani?? manake nilishasoma humu mwanaume kuosha vyombo ni mke kukosa heshima!!!

au unataka mfume dume ambao mwanaume anamdharau na hamshirikishi mkewe kwenye maamuzi? ndo heshima hiyo?
 
na nimejipnaga na mipango lukuki ni namna ya moja kumalizika lingine lifuate
Hahaaaa!! Yaani bila mikakati lazima uambulie patupu, nilijifunza kitu kizuri sana kutoka kwa mama mmoja hivi, haki ile lazima niiaply nikiletewa uduwanzi
 
Mungu kwanza....
Kabla hamjafunga ndoa lazima mumshirikishe Mungu...mkioana pia Mungu ndio awe ngao na kiongozi wenu...yani Mungu ndio kila kitu.vijana wengi siku hizi Mungu kando starehe kwanza...kanisani hawaendi kipindi cha uchumba mpk ndoani .hawasali..unategemea shetani akiingia hapo watatoka salama...mimi nina mifano hai..ndoa nyingi zinazotetelreka Mungu wamemuweka kando...sio kwamba ukimuweka Mungu mbele hakuna vikwazo noo vikwazo vipo lkn Mungu anawapa njia ..mnasolve love inaendelea...kuna ndoa nilisimamia mimi na mume wangu bwana harusi anasema hajaingia kanisani muda mrefu ht miaka 10 inafika kiasi kwamba kuna vitu alishasahau kanisani vinatamkwaje na ht baadhi ya madiliko km kuitikia hajui..yn ndoa ndio imempeleka kanisani kwa mara ingine..huko aliko ndoa yke ikoje kiimani sijui....
Nna rafiki yngu ndoa imedumu only 2 years wakaachana....wao ibada kwao ilikua mwiko hawaendi kanisani wala nini .ikifika jpili ni kulala...hawana hbr na ibada si jumuia c nini...hata sasa hivi ana majaribu makubwa yanayosababishwa na kuvunjika kwa ndoa lkn wapi..anaishia tu kuandika ooh Lord help me...how then?
Ushauri wangu mtoa mada MSHIRIKISHE MUNGU KWA KILA JAMBO UWE MTU WA IBADA HATA JARIBU LIKIJA KUBWA UTALISHINDA TU..ndoa ni mpango wa Mungu si shetani. Usihofu kuoa sababu za wengine zimebuma....
Ukiwa na hofu ya Mungu utamheshimu mke hutocheat...nayeye pia akiwa na hofu na Mungu atakuheshimu hatochepuka na ataelewa nafasi yake ni ipi na mume ni ipi
 
Mie ni victim wa hvyo vitu!daah!acha tu!

Nilipenda,niliheshimu,ndugu walinipenda nilijishusha nilipambana!

Nilikua nampa kila anachokitaka kwa muda muafaka!!

Mwisho akaniambia hanihitaji akiulizwa sababu anasema basi tu nimemchoka!hana hata ubaya Ila mie sasa hivi sitaki mke!

Mungu ananiona simsingizii hata angekuepo hapa!

Mwisho nakuja Dar kuuguza narudi nakuta replacement ndani!

Nikageuza kwetu sijarudi tena nmna niliacha kila kitu!

Naanza upyaaa maisha moja kabisa!

Ndoa kwa sasa hapana kwa kweli badoooo!!!

Wacha waoane!
Duuh..hata wewe!polee..bora tuishi single tu
 
Binafsi i don't believe in marriage japo nipo kwenye ndoa ila anytime ntaiacha maana ninayokutana nayo ni makubwa na si swala la uvumilivu no mimi nimevumilia kwa miaka minne unaenda wa tano ila mtu ndo kama anakuona unajipendekeza na huna pa kwenda, nadhani kiburi cha pesa na hulka ya mtu binafsi kuwa na wanawake wengi pia vinachangia ndoa nyingi kuvunjika,mwanamke unaweza ukavumilia na kujaribu kumrekebisha ila mwanaume anakuona km unampanda kichwani na kumfatilia mambo yake so hapo ndo kuna tatizo
upuuzi wako tu jichunguze mwenyewe km hukujitongozesha kipindi cha uchumba ili hali unajua kbs malaya na ukajileta sasa unamuona hafai baada ya kukaa nae ukaona huwezi mbadilisha....tukisema mwalimu wenu kipofu mnabisha.......tulia ujue unataka nn kwa mwanaume wako wa maisha na sio ukiona mtu anapendeza anashobokewa na wanawake na ww unajichekesha chekesha...i hope darasa limekuingia vzr
 
Hizi ndoa hizi
Pamoja na kusoma sana humu na kusikia kuwa ndo za siku hizi majanga ila bado mimi nahitaji ndoa yakinishinda ntaondoka.
Inafikia hadi hatua mtu aliyeolewa anakwambia kabisa mwaya mdogo wangu usiolewe ndoa ngumu ingekuwa mimi wewe nazaa katoto kangu kamoja natulia.
Hapo unabaki tu kumshangaa.
Si kila mtu atapata ndoa yenye matatizo japo nyingi za siku hizi kila mtu analalamika.
Kuwa mke kuna raha yake ila usivumilie mpaka ifikie hatua unatolewa jicho eti unailinda ndoa yako.Maji yakizidi unga tafuta mbadala wa maisha yako.
Maisha yenyewe mafupi uje teseka kwasababu ya mtoto wa mwingine.
Inategemea na jinsi unavyojiweka maana ukijiheshimu mungu atakujaalia kupata mme mwema kama mimi,binafsi tangu nimebarehe nilikua na uhusiano na wasichana watatu lakini katika mazingira ya mapenzi ya kitoto na wala sijachomeka uume wangu katika papuchi zao.Mwanamke wa nne kua na uhusiano nae ni mke wangu ambaye huu ni mwaka wa saba tangu tufahamiane lakini katika maisha yetu ya ndoa sasa ni mwaka wa pili
Tangu nibarehe mkuyati wangu umeingia kwenye papuchi moja tu ambayo ni ya mke wangu chakufurahisha zaidi na mimi ndio niliyemtoa nanii yake so tunapendana sana na tabia zake hazihatarishi ndoa yetu.Mke wangu akisafiri halafi ikatokea nikapata nyege huwa napiga tu PUNYETO ili kuepesha shari maana nyumba ndogo ni laana,umasiki na mkosi.
NB;wanawake wema wapo na wanaume wema tupo
 
Ndoa za sasa zipo kwa mihemko tu ya kupendeza siku ya harusi, pete yangu ya tanzanite na whitegold, nitakavyobadilisha nguo siku ya harusi kanisani shela ukumbini gauni nimeagiza dubai, bwana harusi anavyojua kuvaa na kupangilia rangi na wale marafiki zake watakavyoingia kwa mbwembwe, mtu hawazi baada ya kuachwa hotelini unakuwa mama au baba kila kitu kinawahusu tena mkijadiliana kwa pamoja siyo baba anawaza kununua kiwanja mke anawaza kuchukua mkopo wa kununua vitz ili awaambie mashostito baada ya ndoa tu akanipa gari, kumbe gari kakopa na mgogoro kwenye ndoa ukaanzia hapo kila mara mnapishana kauli kwa kuwa mwanaume ulitaka kuoa msomi siyo mke anaamua anavyotaka, uliacha kumuoa mke mwenye heshima kisa wewe unamzidi elimu hamtaendana, haya sasa umempata huyo kama wewe yeye anajua usawa tu hamsini kwa hamsini, mwanamke ni mwanamke tu itabaki kuwa hivyo mavyeo yako ukifika home yaache mlangoni tena getini kabisa ukiingia ndani wewe ni mke mtii mumeo, wengine eti wanasema usizoee kumuaga mumeo mpe taarifa tu ndoa inakufa hiyo kwenye ndoa kuna mke zaidi ya mmoja ila siyo mume zaidi ya mmoja, na wazazi nao wanachangia siku ya send off mwanangu chumba chako hakijapangishwa ukiona anakutesa rudi tu maneno gani hayo kweli akiona mwanaume kachepuka kesho kwao, wanaume mfanye kazi mlete chakula nyumbani usitegemee sana hela ya mwanamke hawajaumbwa kutoa, ndo mana bibi na mama zetu walidumu hawakupewa majukumu makubwa ndani.
kweli kabisa, mke ni mke tu.
 
Wanawake wamekuwa wababe mnoo,anataka awe kama mama yako wa kukuzaa,na hayo wanafundishwa kwenye semina za ndoa na kitchen party.Utanifokeaje bana na kunitia makofi?
 
what has feminism have to do na ukosefu wa heshima??

usituchafulie harakati tafadhali, kama MTU hana heshima, hajui kushauriana na watu ni character yake mwenyewe, nothing to with feminism.

na hii heshima inayoongelewa ni kitu gani?? manake nilishasoma humu mwanaume kuosha vyombo ni mke kukosa heshima!!!

au unataka mfume dume ambao mwanaume anamdharau na hamshirikishi mkewe kwenye maamuzi? ndo heshima hiyo?
nyie muongee tu majukwaani lakini mwanamme haswaa hawezi kubaliana na feminism theory, mke ana nafasi yake ya pili na mme ana nafasi ya kwanza, wala haihitaji elimu kubwa kwani ELIMU YA ASILI IPO WAZI, ila tu ubishi na elimu zenu za vidato mnazitumia vibaya sana. Umetangulia kusema mwanamke akisalitiwa na mmewe eti achepuke ili kuitafuta furaha huko nje, hiyo elimu unaitoa wapi wewe kama sio mfumo jike huo yaani unasahau kuwa nyumba ya ndoa inashikwa na mwanamke, mwanaume hata akiwa kiruka njia ila mke akisimama imara familia itaendelea tu lakini sio mwanamke kuwa kicheche hapo hakuna uwezekano mkubwa wa familia kuendelea kusimama.
 
Back
Top Bottom