Dah! Kuna kaukweli fulani lakini hapanani anataka kuishi na Malaya aje aletewe miwaya ndani!! wacha waachane tu.
na usiseme wanawake wanalipiza, sema wanaenda kutafuta furaha yao. unafikiri ni maboksi hawana hisia au wana mioyo ya chuma? aishi maisha yake kumlilia MTU ambaye hamjali? acha tu watafute furaha nao.
ukisema tu ndoa ina miaka thelathini wala hunivutii, hadi nijue ni ndoa kweli ama vepee! sio sifa kusema tu ndoa INA muda mrefu wakati wahusika hawafurahii, mnafurahia nyie watazamaji!
Hahaha umenichekeshaBinafisi nikweli ndoa za zamani zili dumu nikisema mazingira ya kipindi iko yali luhusu,unakuta mwanamke tangu aolewe anashikwa kiuno na mmewe pekee ila nambie saivi hali ilivo.kwa wanaume sasa ndio usiseme.Kipindi iki ndoa zina changamoto kupita kiasi.
Kiukweli tuache kufalijiana ndoa za kweli ndio zinaishia.
Wanao sema ndoa raha waulize wamepitia matatizo mangapi bado wakaiona ndoa ni raha.
Kwa ufupi naamini miaka ijayo mtu mwenye akili timamu(ukiacha hawa wanao funga ndoa kuepuka dhambi ya zinaa) atakae kua kwenye ndoa atashangaza sana.
![]()
![]()
![]()
![]()
![]()
![]()
Ushauri mzuri sana huu. AsanteNdoa ni tendo la kiimani hivyo wanandoa inawapasa kumtanguliza Mungu mbele ili aweze kuilinda ndoa yao. Vijana wa siku hizi wakimaliza kuoana hawamuhusishi tena Mungu wao,, Hawaendi Misikitini wala Makanisani. Hawasali pamaoja! Sala ndio nguzo pekee ya ndoa! Muwekeni Mungu wenu mbele nanyi mtaishi miaka mingi kwa raha daima!
Pia vijana waache kuhusisha maisha ya ndoa na mambo ya social networks.. Social networks ndio chanzo kikubwa cha kuvuruga ndoa nyingi! Wana ndoa wanapotaka kuiga mambo ya watu wengine wanayoyaona kwenye social network ndio tatizo linapoanzia hapo. Mdada anaona mwenzake kila siku katolewa outing na mumewe naye anataka mumewe amfanyie vivyo hivyo bila kujali mpangilio wao wa kimaisha yeye na mwenza wake!
Ushauri mzuri dada asante. Vijana tuuzingatieUliyoyasema yote ni kweli. Mi nadhani tatizo kubwa watu wanakimbilia ndoa labda kwasababu wanaona wenzao wameoa/kuolewa au wamehimizwa na familia au kupenda sifa tu hasa kwa wadada au pia kuona umri umeenda. Nimesoma vitabu vichache vya ndoa na kufahamu kua sababu pekee ya kumfanya mtu aingie kwenye ndoa ni utayari wa kuingia kwenye ndoa na si vinginevyo.
Hamna ndoa iliyokosa changamoto, ata kama hao watu walipendana kiasi gani... Uvumilivu ndo unafanya ndoa nyingi zidumu.
Pia upendo usiwe kigezo pekee cha kuingia kwenye ndoa. Upendo huzaliwa, hukua na pia hufa. Wengi pale upendo unapoyumba ndo wanagundua mapungufu yao. Mtu anatakiwa aoe/aolewe na mtu anayeendana na mipango yako ya maisha, sio mmoja ana mpango wa kwenda kuishi mbeya na mwingine anataka abaki Dar... Yote haya ni ya kuyasuluhisha ndani ya uchumba.
Ishu ya feminism pia inawaharibu wanawake wengi sana. Wanawake tusijidanganye, hatuwezi kua sawa na wanaume. Ndio una elimu yako na kazi yako ata kama unaingiza kipato zaidi ya mwanaume inabidi umpe heshima yake mume wako. Mwache mwanaume awe kichwa... Usimlinganishe na wanaume wengine na husimfanye akajiona hana thamani. Kama tunavyopenda kusifiwa, wanaume nao wanapenda hivyo. Ukimaliza tendo na mwenza wako msifie kwa kazi aliyofanya ata kama unajua siku hiyo kachemsha... Kesho yake ataongeza juhudi.
Kwa wanaume walio kwenye ndoa,,, ukimshindwa huyo ulienaye una uhakika gani huyo unaetaka kumchukua atakua tofauti?
Lakini ungefafanua kidogo dadashida ni tamaa na umimi.
uko kwenye ndoa bado unataman nje(kwa wote) Afu matumiz ndan hutoi( kwa wote) chakochako.Lakini ungefafanua kidogo dada
Dah! Hadi sumu? Kuna mtu aliwahi kuniambia kuna wanandoa wanaombeana hadi vifo ili wawe huru .Wanandoa hasa wanawake hawataki kujikubali wanapenda maonyesho anataka awe juu zaidi ya wanawake wote vitu ambavyo havimsaidii moja kwa moja social netwek ndo inawaharibu imefikia mahali me nimepiga marufuku insta na fb ili kunusuru ndoa maana ilishakuwa ICU imekata kauli kauli.ndoa ya miaka 9 nilikuwa naivunja ndani ya siku moja!
Mwanamke anakwambia ona kina fulani wanavyoishi vizuri sijui mara hivi,huwezi kujua ndoa za watu ndani wanaishi vipi ni sisi wa nje ndo tunafurahia maisha ya ndoa ya watu wengine ila wao hawana raha ndani inafikia wanataka kuwekeana hata sumu
As if kukaa muda mrefu kwenye ndoa means anything.nani anataka kuishi na Malaya aje aletewe miwaya ndani!! wacha waachane tu.
na usiseme wanawake wanalipiza, sema wanaenda kutafuta furaha yao. unafikiri ni maboksi hawana hisia au wana mioyo ya chuma? aishi maisha yake kumlilia MTU ambaye hamjali? acha tu watafute furaha nao.
ukisema tu ndoa ina miaka thelathini wala hunivutii, hadi nijue ni ndoa kweli ama vepee! sio sifa kusema tu ndoa INA muda mrefu wakati wahusika hawafurahii, mnafurahia nyie watazamaji!
Ndoa ina side effect kubwa kuliko ya arvDah! Hadi sumu? Kuna mtu aliwahi kuniambia kuna wanandoa wanaombeana hadi vifo ili wawe huru .
Ubarikiwe mkuuUliyoyasema yote ni kweli. Mi nadhani tatizo kubwa watu wanakimbilia ndoa labda kwasababu wanaona wenzao wameoa/kuolewa au wamehimizwa na familia au kupenda sifa tu hasa kwa wadada au pia kuona umri umeenda. Nimesoma vitabu vichache vya ndoa na kufahamu kua sababu pekee ya kumfanya mtu aingie kwenye ndoa ni utayari wa kuingia kwenye ndoa na si vinginevyo.
Hamna ndoa iliyokosa changamoto, ata kama hao watu walipendana kiasi gani... Uvumilivu ndo unafanya ndoa nyingi zidumu.
Pia upendo usiwe kigezo pekee cha kuingia kwenye ndoa. Upendo huzaliwa, hukua na pia hufa. Wengi pale upendo unapoyumba ndo wanagundua mapungufu yao. Mtu anatakiwa aoe/aolewe na mtu anayeendana na mipango yako ya maisha, sio mmoja ana mpango wa kwenda kuishi mbeya na mwingine anataka abaki Dar... Yote haya ni ya kuyasuluhisha ndani ya uchumba.
Ishu ya feminism pia inawaharibu wanawake wengi sana. Wanawake tusijidanganye, hatuwezi kua sawa na wanaume. Ndio una elimu yako na kazi yako ata kama unaingiza kipato zaidi ya mwanaume inabidi umpe heshima yake mume wako. Mwache mwanaume awe kichwa... Usimlinganishe na wanaume wengine na husimfanye akajiona hana thamani. Kama tunavyopenda kusifiwa, wanaume nao wanapenda hivyo. Ukimaliza tendo na mwenza wako msifie kwa kazi aliyofanya ata kama unajua siku hiyo kachemsha... Kesho yake ataongeza juhudi.
Kwa wanaume walio kwenye ndoa,,, ukimshindwa huyo ulienaye una uhakika gani huyo unaetaka kumchukua atakua tofauti?
Ndoa ina side effect kubwa kuliko ya arv

Sababu kuu ndoa za siku hizi ni maigizo unakuta shoga au rafiki ana kauli ndani ya ndoa ya wenzake na kuifanya atakavyo. Pia mashemegi na wakwe nao hawana furaha na ndoa zao huanza fitna kwa ndoa za watoto wao. Bila ya kusahu wadada wengi hutamani mapenzi kama za kwenye tamsilia wakisahau hayo mapenzi ni ya mchezo tu na yameshapangwa.Nini sababu nyingine zinachangia? Karibu mtoe maoni tuwaandae vijana kabla hawajaingia kwenye ndoa takatifu.