Ni wasomi lakini nadhani hawajui madhara ya kugombana mbele ya watoto. Laiti wangejua na wangekuwa wanawajali hao watoto wasingefanya hivyo.
.
Kuna ndugu yangu ndoa ina miaka 15. Lakini kutwa analalamika mume wake anavyomnyanyasa (kupigwa na kutukanwa).
Yeye furaha yake ni kuwa kakaa kwenye ndoa miaka mingi...ni role model wetu..... Hahaha.
Kuna siku waligombana na mumewe nikiwepo. Ile scenario mpaka leo nikiikumbuka huwa siamini na hunipa hofu sana.
Mdada akaniambia hapo ilikuwa kawaida tu. Inakuwaga timbwili kweli kweli, mpaka watoto hujificha...mh
Ila haya mambo naona hutegemea na mtu pia. Kuna watu wastahimilivu sana.
(SAMAHANI kwa gazeti ,maneno hayaniishi)
Nothing else is more important than peace of mind.
Watu wanaoishi kupigana wana amani gani? Kwanza unalalaje na MTU aliyekupiga, huogopi atakukaba usiku!
Haya yanafanywa na MASOKWE huko porini sio jamii iliyostaarabika.
kweli kuwitness gumi za watu wazima can be traumatic, tena watoto!!
Watu aggressive nafikiri bado "umwitu" uko active ndani yao. They might as well just leave our societies wakaishi na masokwe wenzao porini huko.
Niijua ni vibabu vya leo ndo vilikuwa vinapiga wake zao, na wanywa gongo uswahilini huko.
Kusikia kuna vijana Leo wanaishi kwa vipigo, tena walioenda shule, tena hadi kufa, inashangaza mno.
Watu wanaovumilia haya wana Nini vichwani?
Ndo Hawa hawa wanaopelekeshwa na jamii.
Wanadanganyika na sifa za uongo kama "mke imara" na "mke mwema". Eti ndo watengeneza familia bora. Wanaogopa JINAMIZI linaoitwa " kuachika" " u single mother"
Baadae atasimulia kwa sifa UVUMILIVU wake, thawabu aliyopata ni kusifiwa na jamii. Manake hata mwanao Kama sio kilaza hawezi Ku appreciate wewe kukaa matesoni wakati uwezo wa kuondoka unao.
Watu wenyewe wanaokusifia ndo hawa wasiostaarabika, wasioelimika, wasiojiheshimu, wasiojali wenzao, wasioheshimu wanawake, wanaume malaya, wasio na UTU wala HURUMA, wenye akili EMPTY na wenye undugu wa karibu na MASOKWE.
HII HAIWAHUSU WASIO NA UWEZO WA KUJITEGEMEA manake inawezekana wangeweza wangejiondokea.
Kweli the greatest battle is the battle of the mind.
************************
I just came across this