Kulikoni ndoa za siku hizi?

Kulikoni ndoa za siku hizi?

Mie ni victim wa hvyo vitu!daah!acha tu!

Nilipenda,niliheshimu,ndugu walinipenda nilijishusha nilipambana!

Nilikua nampa kila anachokitaka kwa muda muafaka!!

Mwisho akaniambia hanihitaji akiulizwa sababu anasema basi tu nimemchoka!hana hata ubaya Ila mie sasa hivi sitaki mke!

Mungu ananiona simsingizii hata angekuepo hapa!

Mwisho nakuja Dar kuuguza narudi nakuta replacement ndani!

Nikageuza kwetu sijarudi tena nmna niliacha kila kitu!

Naanza upyaaa maisha moja kabisa!

Ndoa kwa sasa hapana kwa kweli badoooo!!!

Wacha waoane!
Acha waoane kwakwel mi pia nilichokwa mwenzio... hivi kwan mtu hawez.ishi mwenyewe bila upuuzi huu? Bora pekeangu kwakwel nakua na free zaid
 
Mie ni victim wa hvyo vitu!daah!acha tu!

Nilipenda,niliheshimu,ndugu walinipenda nilijishusha nilipambana!

Nilikua nampa kila anachokitaka kwa muda muafaka!!

Mwisho akaniambia hanihitaji akiulizwa sababu anasema basi tu nimemchoka!hana hata ubaya Ila mie sasa hivi sitaki mke!

Mungu ananiona simsingizii hata angekuepo hapa!

Mwisho nakuja Dar kuuguza narudi nakuta replacement ndani!

Nikageuza kwetu sijarudi tena nmna niliacha kila kitu!

Naanza upyaaa maisha moja kabisa!

Ndoa kwa sasa hapana kwa kweli badoooo!!!

Wacha waoane!
Duh! Stori yako imenisikitisha pole sana
 
Ndoa ni nzuri cha muhimu ni heshima na maelewano pande zote ,hakuna ndoa iliyo na furaha kila siku lazima kutofautiana na kusonga mbele.mimi nina mwaka wa 9 na sijafikiria kuachana kamwe.
ameen na hongera pia!

Mungu awaongoze hvyo hvyo awape hekima na busara!
 
Mimi nimegundua asilimia kubwa ya ndoa za siku hizi ni fasheni. Mtu hajakaa na mwanaume wala mwanamke muda mrefu wakajuana au sio kujuana tu kufahamiana na kukomaa akili zao wanazukia ndoa. Na ukikaa muda mrefu hasa kama ni binti hujaolewa utaonekana una mkosi au nung'aembe. Kitu ambacho si kweli. Upendo pekee hautakufanya ukae na ndoa yako milele. Ni Upendo, Ufahamu na Ukomavu wa akili ndio vitakusaidia.
Vijana wenzangu mkiomba Mungu akawasaidia mkayapata hayo mtanusurika. Na wewe ambae hujaoa/hujaolewa tuliza kichwa na moyo usije kujuta bureee halafu uje useme wanawake au wanaume wote wabaya. Kumbe hukuwa mtu sahihi na mahala sahihi.
Mfano huu ni mzuri, siku moja nilikuwa katika pita pita zangu mjini nikaona kiatu kizuri nikaangalia namba nikaona inanitosha haraka haraka nikakichukua kile kiatu (sikujali kuangalia mambo mengine kuhusu kiatu hicho kama ngozi yake ...nk). Nilipofika nyumbani kesho yake nikakitinga, kumbe mguu unaingia vizuri hadi chini ila juu kuna urembo ambao ulibana mguu wangu na kutengeneza msuguano fulani kila nilipotembea na hatimae kunitengenezea lenge lenge. Nilitembea kwa shida siku nzima na maumivu juu. Niliporudi niligawa kiatu kile wala sikukitamani tena wakati nilikipenda sana. Nililazimisha kukimiliki kwa sababu tu ni kizuri. Huu mfano una akisi maisha ya watu kuelekea kwenye ndoa.
Nawatakia wiki njema.
 
Niseme tu wengi wanaotaman kuingia kwenye ndoa ... hawajui ndoa ni nini. wengi walioko nje huwa hawatafakar changamoto za ndoa.. ila wanatafakar raha za ndoa.. huku wakisahau misukosuko inayoweza kutokea kwenye ndoa na jinsi gani kukabiliana nayo.
Na pia baadhi ya vijana wengi wa kizazi hiki.. hawajitambui.. ni wachache sana.. wanaojitambua.
Uvumilivu umepungua kutokana na kila mtu kujiona bora kuliko mwingine... dharau.. na tamaa za kijinga.
 
Ndoa ni tendo la kiimani hivyo wanandoa inawapasa kumtanguliza Mungu mbele ili aweze kuilinda ndoa yao. Vijana wa siku hizi wakimaliza kuoana hawamuhusishi tena Mungu wao,, Hawaendi Misikitini wala Makanisani. Hawasali pamaoja! Sala ndio nguzo pekee ya ndoa! Muwekeni Mungu wenu mbele nanyi mtaishi miaka mingi kwa raha daima!

Pia vijana waache kuhusisha maisha ya ndoa na mambo ya social networks.. Social networks ndio chanzo kikubwa cha kuvuruga ndoa nyingi! Wana ndoa wanapotaka kuiga mambo ya watu wengine wanayoyaona kwenye social network ndio tatizo linapoanzia hapo. Mdada anaona mwenzake kila siku katolewa outing na mumewe naye anataka mumewe amfanyie vivyo hivyo bila kujali mpangilio wao wa kimaisha yeye na mwenza wake!
Umemaliza, Ni Mungu pekee ndie solution kwenye migogoro na furaha uwapo ndoani
 
tatizo kubwa ubinafsi na kukosekana kwa upendo, fake nyingi before marriage, kukosa mawasiliano mazuri ndani ya ndoa...mtazamo wa ndoa kabla ya ndoa ndiyo inamaliza mengi tunategemea makubwa ndani humo na hatujipangi namna ya sisi kuchangia katika hayo makubwa
 
Mkuu kinachofanya ndoa ziwe ngumu siku hizi ni watu kuingia kwenye ndoa bila kuelewa wanakuwa humo kwa sababu gani? Sasa hivi ukisema uulize mtu kwanini amefunga ndoa ni wachache sana watakaokupa majibu ya kuridhisha nilichokiona kwa muda niliokaa kwenye ndoa ni yafuatayo
1. Wanandoa wanajua ni furaha siku zote hakuna nyakati za huzuni, hasira na maumivu
2. Wanafuata mapenzi kwenye ndoa na sio kujenga familia nzuri
3. Hawaelewi kuwa mtu unaeenda kuishi naye ana mapungufu na anaweza kukosea na unapaswa kusamehe over and over bila kuweka kinyongo
4. Watu wanategeana kufanya majukumu yao mfano kuhudumia familia, na kuheshimiana
5. Watu wanakata tamaa mapema sana linapotokea tatizo hawakai kusolve au kufight ndoa iendelee kuwepo
Hayo ndo niliyoyaona na nimeyafanyia kazi kwa kiasi kikubwa nyumba ina amani na ninaimani nitazeeka na mzee tukiwa pamoja in one piece.
kujiinua na kujiona kila mtu hana shida na mwenzie
 
Wanandoa hasa wanawake hawataki kujikubali wanapenda maonyesho anataka awe juu zaidi ya wanawake wote vitu ambavyo havimsaidii moja kwa moja social netwek ndo inawaharibu imefikia mahali me nimepiga marufuku insta na fb ili kunusuru ndoa maana ilishakuwa ICU imekata kauli kauli.ndoa ya miaka 9 nilikuwa naivunja ndani ya siku moja!
Mwanamke anakwambia ona kina fulani wanavyoishi vizuri sijui mara hivi,huwezi kujua ndoa za watu ndani wanaishi vipi ni sisi wa nje ndo tunafurahia maisha ya ndoa ya watu wengine ila wao hawana raha ndani inafikia wanataka kuwekeana hata sumu
mkuu umesema vyema hilo nalo tatizo kubwa kujilinganisha
 
Yaani hizi ndoa! Tatizo ni kutokujielewa tu na kutambua kwanini unaingia kwenye ndoa. Kikubwa zaidi hofu ya Mungu hakuna.

Kuna boya mmoja anataka kumuacha mke wake eti kisa hajasoma, sasa nikajiuliza wakati anaoa huyo mke alikuwa kasoma ila sasa ndio hana elimu!!
bora hata ya mimi nafuta pesa na kumiliki vikubwa ..akiamua kugonga vibinti huko watajiju sababu nitabana mpaka penat wataambulia duduu tu
 
Ni bora kujiishia pekeako tu huu ujinga hata mie nauona unamnyenyekea mke mke anakuona bwege unamkuta anatongozana.na vitoto vya chuo tena vya field... sijazaa wala nn bora.achape lapa bora pekeangu
ha haha si ishu ya kucheka ila mkeo duh
 
Back
Top Bottom