nyie muongee tu majukwaani lakini mwanamme haswaa hawezi kubaliana na feminism theory, mke ana nafasi yake ya pili na mme ana nafasi ya kwanza, wala haihitaji elimu kubwa kwani ELIMU YA ASILI IPO WAZI, ila tu ubishi na elimu zenu za vidato mnazitumia vibaya sana. Umetangulia kusema mwanamke akisalitiwa na mmewe eti achepuke ili kuitafuta furaha huko nje, hiyo elimu unaitoa wapi wewe kama sio mfumo jike huo yaani unasahau kuwa nyumba ya ndoa inashikwa na mwanamke, mwanaume hata akiwa kiruka njia ila mke akisimama imara familia itaendelea tu lakini sio mwanamke kuwa kicheche hapo hakuna uwezekano mkubwa wa familia kuendelea kusimama.
Kwanza mwenyewe umeprove ulichosema ni uongo. Mwanaume ni wa kwanza kwenye Nini? Ujinga?
Imani, culture, malezi, elimu na utashi wa mtu ndo hum Shape mtu. Unajua mwenyewe ni vipi umekuja kushikilia huo UNANILIU wa mwanaume nafasi ya kwanza.
And I won't take that away from you.
Wala si wanaume wote wana mawazo kama yako, there are billions of men what makes you think wote wako kama wewe??? Si ningekuwa sista!
Jiongelee mwenyewe bro na waafrika wenzio labda.
Sijui unamaanisha Nini unaposema Feminism, watu wana mawazo hasi kupitiliza, kama huyo aliyesema feminism ni kukosea watu heshima, ambayo sijajua anamaanisha Nini.
Na haujajishtukia jinsi ulivyo MTU wa HOVYO? Kwanini hujaandika kupinga wanaume MALAYA?
nimeongelea furaha ya mwanamke umedismiss like nothing!! Kumbe furaha ya mwanamke si kitu?
HUO NDO MFUME DUME.
Ndo unakotaka kuturudisha huko, huko ambako wanawake ni wanyonge??
Huko ndo tunatoka ndomana ndoa kibao CHALI kwasababu ya wanaume WABINAFSI, WASIOJIHESHIMU wala KUJALI FAMILIA zao.
Familia imara ndo inatengenezwa na mwanaume MALAYA na mwanamke asiyefurahia maisha hayo?
Embu nielezee mwanamke anayechepuka anaharibuje familia na mwanaume MALAYA anajengaje?
Kwanza kwenye vitabu vya dini msingi wa talaka ni UZINZI.
na huwa mnashauri waume za wanawake wachepukaji wapige goti kusali na kuvumilia ili familia iwe imara?? AU NDO MUENDELEZO WS MFUMO DUME?
Familia itasimama tu kwani wangapi wanaishi hayo maisha Leo hii huku huku nje tunajua ni wana ndoa?
Mbona wanaume Malaya wa zamani walivumiliwa watu wakaishi tu? .
MBONA NYIE WANAUME HAMTAKI KUPRACTICE SIFA HII YA KIMUNGU YA UVUMILIVU?
Tusidanganyane na UIMARA!! huo uimara unapimwaje? Kama MTU yuko comfortable na umalaya wa mwenzako so be it, lakini sio kuwalazimisha wenzenu/kuwapa guilt conscience waishi hayo maisha kwa kuwadanganya watakuwa na familia imara. kwanza ndo itatuzalishia watoto Malaya kama baba zao.
Overall sikia brother, times have changed. It's all about mutual respect, individual rights, and happiness now. Anything against that is SIN.
Kila MTU atafute tu mwenzi mwenye viwango sawa na mtazamo sawa wa maisha ili mifarakano ipungue.
Mimi kwamfano nisingeweza kuolewa na muafrika, nisingekuwa na furaha KAMWE wala uwezo wa kumfurahisha MTU asiyeelimika kama wewe sina.