Kula kwa mamantilie ni risk

Mleta uzi inaonekana umezaliwa masaki, ukasomea upanga, kisha ukaenda nje ya nchi kuchukua digil yako, kazi unafanya bank kuu na unamaisha mazur! Ongela tuache cc tulioZoea maisha hayo.. Mushkru pia Mungu kwa hayo maisha
 
Sio kweli kabisaaaa na huo ugunduzi wako n feki,kingine sio wote tunaoweza kwenda kula chakula kwenye mahoteli makubwa,kwa hyo sisi kama sisi tutakula ww jipikilishe huko kwako,kingine ww una imani potofu ndo maana unakuja na maswala ya kulogwa hapa
 
Msiharibie akina mama food vendors biashara zao. Acha ubishoo akina mama hao wanasomesha watoto wao kwa biashara hizo. Cha muhimu ni usafi. Period.
 
Ishu za kulogwa zipo tuu hata usipokula. Na mabasi usipande maana asilimia kubwa yana mazindiko.

Ukicomplicate maisha utapata tabu sana, nimelelewa kwa biashara ya mama ntilie, nimesomeshwa nayo, na nimekula sana kwa mama ntilie mpaka sasa maisha yananiendea ahueni nimeweza kujitegemea na kusimama mwenyewe, though sasa hivi nimempumzisha mama na kumtafutia ishu nyingine ya kufanya. Big respect to wanawake wanaojishughulisha na kulea familia zao kupitia shughuli hizo.
 
Ah wapi zile zilikuwa story tu kama hizi za kuwekewa maji ya maiti kwenye msosi.

Kaka ile stori kweli mkuu Hebu waje waliozunguka watakwambia ukiwa 5star hotel huko ukinywa kahawa usipofunika Watu wanakujazia tu..mi nilishuhudia kwe Brazilian restaurant wenyewe wanakuwekea nyama hadi uonyeshe kibao kinaonesha upo full
 
[QU OTE=Annael;10642469]Nimejiproud wapi bro?[/QUOTE]
Mabrazamen mna shida.....uchawi kibongobongo upo Kila kona hadi kwe nyumba za Ibadan Hebu usiwachafue wamama wa watu
 
Mimi napenda kujipikia chakula changu kwangu, huwa sipendi kula kwa mama nitilie au sehemu wanapopika vyakula kiholela.

Hii ni baada ya kugundua asilimia kubwa ya mama nitilie wanatumia ushirikina kwenye biashara zao, na hatimaye kuweka uchafu kwenye vyakula. Yaani utakuta eti ndani ya ubwabwa wamechanganya maji ya maiti au kachanganya mkojo wake wa asubuhi!!! Hii inatia kinyaa sana lakini ndio hivyo.

Kunajamaa yangu wa karibu kanunua maandazi baada yakuanza kula akakutana na nywele kibao ndani ya andazi.

Utakuta mara nyingine anachanganya choo cha mtoto ndani ya chakula ili apate wateja wengi. Hii inatia kinyaa sana.

Baada ya kugundua hivyo niliamua kupika mwenyewe kwangu.

Ni hayo tu.
Annael kama unahasira na mama ntilie alikuibia bwanako mwendee umshambulie moja kwa moja yeye mwenyewe lakini siyo kuwaharibia wanawake wanaopambana na maisha haya magumu, kuwa muungwana.
 
Sijasema wote. Kwanini bro nisiseme kitu ambacho kinatendeka? Pawepo utaratibu maalumu ili watu wasiingize issue za ushirikina.

hembu toa maoni ya huo "utaratibu maalum" unataka uweje?
 
Dah umenikumbusha mbalii...nliangaliaga ile movie ya 3idiots mpaka leo sili chapat za kununua baada ya kuona yule mama akimkunia mmewe yale mapele kile kifimbo cha kusukumia chapati..kula magengen yahitaj moyo

Siyo magengeni tu bali hata ukichunguza hali ya usafi kwenye migahawa mingine utaacha kabisa kula huko!

Kwa mfano jikoni mtu anasonga ugali ama anapika wali kifua wazi, majasho yanadondoka hadi kwenye sufuria la ugali au wali......!!!
 
Mimi napenda kujipikia chakula changu kwangu, huwa sipendi kula kwa mama nitilie au sehemu wanapopika vyakula kiholela.

Hii ni baada ya kugundua asilimia kubwa ya mama nitilie wanatumia ushirikina kwenye biashara zao, na hatimaye kuweka uchafu kwenye vyakula. Yaani utakuta eti ndani ya ubwabwa wamechanganya maji ya maiti au kachanganya mkojo wake wa asubuhi!!! Hii inatia kinyaa sana lakini ndio hivyo.

Kunajamaa yangu wa karibu kanunua maandazi baada yakuanza kula akakutana na nywele kibao ndani ya andazi.

Utakuta mara nyingine anachanganya choo cha mtoto ndani ya chakula ili apate wateja wengi. Hii inatia kinyaa sana.

Baada ya kugundua hivyo niliamua kupika mwenyewe kwangu.

Ni hayo tu.

acha mawazo mgando ndugu sasa kuna uhusiano gani kukuta nywele kwenye chakula na kuvuta wateja au ndo nyie washirikina?.
 
Uzushi mkubwa wakati mamantilie wengi wana chumba kimoja tu cha biashara wanapikia umo na kuuzia umo.tunawaona wanaanza kupika mpaka wanapakua hadharani hayo mavi yanawekwa SAA ngap?
 
Hata kama wanaweka uharo tutakula hivyo hivyo na hapa nipo kwa mama ntilie nakula nikimkuta nzi namfyonza namtupa usiulize udogoni nimeishije.
 
Na tutakula sana...Dunia hii wapi utapata wali wa nazi jumlisha nyama rosti, maharage nazi, chachandu, chainiz vikiwa vya moto vinaipuliwa kwa buku mbili tu.

buku mbili kwenu huko...kwetu uswazi buku tu!!!
 
Back
Top Bottom