CHASHA FARMING
JF-Expert Member
- Jun 4, 2011
- 7,789
- 8,914
Wakuu kwa mara nyingine nimefanikiwa kuagiza hawa vifaranga wa Kuroiler. Hawa ni kuku kutoka India na wanaweza fugwa free range na hawa like Dorep wanakuwa wakubwa sana. So by mwezi wa 12 nitaanza kutoa supply ya kwanza ya hawa kuku.
=============================================
=============================================
KUROILER :
Asili ya kuku hawa wa kuroiler wametokea nchini _INDIA_
Hawa ni kuku wa kibiashara yaani ni kama broiler wa kienyeji. Wana kuwa kwa haraka sana miezi *3--4* anakuwa yupo tayari kuingia sokoni kama akipewa matunzo mazuri. Wana taga vizur
Kuku hawa kwa mwaka unaweza vuna Mara Tatu kwa makadrio ya miezi 4.
"Kwa mfano mwezi wa 1 ukiingiza Vifaranga bandani hadi mwezi 4 utawauza, mwezi wa 5 ukiingiza Vifaranga bandani hadi mwezi wa 8 utawauza , mwezi wa 9 ukiingiza Vifaranga bandani hadi mwezi wa 12 utawauza."
Kwahiyo ni mizunguuko 3 kwa mwaka mmoja.
kila Batch ukiuza kuku 1,000 kwa mwaka utakua umeuza kuku 3,000
Huku kuku wa kienyeji pure mizunguuko 1-2 kwa mwaka.
*Sifa Za Kuku Aina Ya Kuroiler*
•Wanakua haraka.
•Wanakadiriwa kuwa na uzito kati ya kilo 3 mpaka 3 na nusu wakiwa na umri wa miezi 4
•Wanavumilia magonjwa.
•Wanafugika aina zote za ufugaji ndani, nusu huria na huria kabisa.
*Muhimu* kuroiler wanafanua vizuri zaidi katika upande uzalishaji mayai na kwa ukuaji wa haraka...
Tanga Poultry Farm