Tunawezaje kupunguza gharama za ufugaji wa kuku ili kuongeza faida

Alejandroz

JF-Expert Member
Feb 14, 2017
327
376
Naomba kujifunza yafuatayo kabla sijaingia kwenye ufugaji;

Nafikiria kufuga kuku chotara (Sasso au Kroiler) kisha niwauze baada ya miezi 3 kwa bei isiyopungua 10,000/=

Lakin nimekaa nakupiga hesabu kulingana na ulishaji elekezi kwa kila wiki nikaona nikifuga kuku 100 kwa mwezi wa kwanza nitatumia mifuko 1¼ ya starter, mwezi wa 2 mifuko 2½ na mwezi wa 3 mifuko 3½

Kwa ninavyosikia mfuko mmoja wa kilo 50 bei yake ni 70,000/= hadi 80,000/= hivyo kwa ulishaji nilioutaja hapo juu kwa miezi mitatu nitatumia si chini ya laki 6 na bei yakuku (vifaranga) ni laki 2 hivyo napata jumla ya laki 8 hapo sijahesabu chanjo na madawa mengine

Nikiuza kuku wote (na-assume vifo havijatokea )
100 × 10,000/= nitapata 1000,000/= nikitoa laki 8 napata laki mbili nikitoa madawa na huduma zingine napata faida chini ya laki moja

Kwakupitia hesabu hizi hebu tupeane elimu na uzoefu,, maana naamini wengi wanachukia ufugaji kwasababu ya kukosa taarifa sahihi kama ilivyo kwangu,, kwakweli nimeona sipati faida au niwapi nakosea?

Au bei ya hio mifuko ya vyakula si sahihi?

Au kuchanganya chakula mwenyewe badala yakununua kunapunguza hizo gharama?

Je vipi nikichanganya mwenyewe nitapata matokeo mazuri?

Karibuni tuelimishane namna nzuri yakupunguza gharama za ufugaji wa kuku ili kupata faida nzuri
 
Umepiga hesabu vizuri kwa sababu chakula cha kuku kinapanda kutokana na uhitaji mkubwa kutoka kwa wafugaji wengine, pia hali ya hewa isiyotabirika.

Achana na hizi hadithi za kwamba azola, hydroponic sijui lucina inapunguza 80% wengine 50% ya gharama ya chakula. Ukiangalia nutrition content ya hayo malisho ni sorce ya vitamin coz mengi hapo ni majani. Feeding formula ukicheki kuku anahitaji protein na wanga sana..madini kiasi na hizo vitamins kiasi.

Uchawi upo hapa, kama unaweza kuzalisha chakula chako mwenyewe umetoboa..siyo kununua materials na kuchanganya...namanisha ulime mwenyewe nafaka. Uzalishe funza mwenyewe na uwe na hizo azola sijui hydroponic.
 
Kufuga kibiashara kunategemea bei ya chakula. Kupunguza bei ya chakula inategemea uko mkoa gani na ni vyakula aina gani unapata kwa urahisi.

Gharama ni kubwa kuwalisha kuku haraka ili kuwaweka sokoni.

Kama unafanya hiyo kitu hapa mjini usipunguze gharama za chakula ziongeze, kwa maana ya kupata bidhaa bora. Halafu mauzo yalenge siku yenye uhitaji mfano Dec kuanzia christmass mpaka mwaka mpya.

Au iangukie sikukuu za waislamu. Halafu panga bei ya maana.
 
Kuku chotara wa nyama cha lazima zaidi ni starter. Wakiwa na mwezi mmoja anza kuchanganya chakula chako. Nunua kimoja kimoja (mf. Pumba, mashudu, madini, lukina etc) kwenye sources zilizo cheap zaidi changanya mwenyewe kwa uwiano unaokuwa recommended. Mchanganyo huu kwa eneo nilipo ni kama Sh. 450 kwa kilo ya chakula tofauti na mifuko ya kunununua ambayo ni Sh 1,400 mpaka 1,600 kwa kilo ya chakula.

Wakifika miezi 2.5 mpaka 3 wanakuwa na uzito wa soko.

Ukitaka faida nzuri zaidi fuga chotara kuanzia 150 mpaka 200 kwa kila batch. Usiagize vifaranga vingi sana kwa mkupuo kwani usimamizi unakua hafifu (naongea kutokana na experience).

Muhimu zaidi kuliko vyote usianze kwa kuwa na vifaranga wengi kwa mara ya kwanza. Anza kidogo kidogo huku unapata uzoefu mwenyewe, na sio zile habari za kuambiwa. Mara nyingi watu hua wanasahau kushauri kwenye hili
 
Kuku chotara wa nyama cha lazima zaidi ni starter. Wakiwa na mwezi mmoja anza kuchanganya chakula chako. Nunua kimoja kimoja (mf. Pumba, mashudu, madini, lukina etc) kwenye sources zilizo cheap zaidi changanya mwenyewe kwa uwiano unaokuwa recommended. Mchanganyo huu kwa eneo nilipo ni kama Sh. 450 kwa kilo ya chakula tofauti na mifuko ya kunununua ambayo ni Sh 1,400 mpaka 1,600 kwa kilo ya chakula.

Wakifika miezi 2.5 mpaka 3 wanakuwa na uzito wa soko.

Ukitaka faida nzuri zaidi fuga chotara kuanzia 150 mpaka 200 kwa kila batch. Usiagize vifaranga vingi sana kwa mkupuo kwani usimamizi unakua hafifu (naongea kutokana na experience).

Muhimu zaidi kuliko vyote usianze kwa kuwa na vifaranga wengi kwa mara ya kwanza. Anza kidogo kidogo huku unapata uzoefu mwenyewe, na sio zile habari za kuambiwa. Mara nyingi watu hua wanasahau kushauri kwenye hili
Mkuu, tufungue thread yetu ya wafugaji kuku, tuulizane maswali na ku share experience kusaidia wengi, unaonaje..?
 
Kuku chotara wa nyama cha lazima zaidi ni starter. Wakiwa na mwezi mmoja anza kuchanganya chakula chako. Nunua kimoja kimoja (mf. Pumba, mashudu, madini, lukina etc) kwenye sources zilizo cheap zaidi changanya mwenyewe kwa uwiano unaokuwa recommended. Mchanganyo huu kwa eneo nilipo ni kama Sh. 450 kwa kilo ya chakula tofauti na mifuko ya kunununua ambayo ni Sh 1,400 mpaka 1,600 kwa kilo ya chakula.

Wakifika miezi 2.5 mpaka 3 wanakuwa na uzito wa soko.

Ukitaka faida nzuri zaidi fuga chotara kuanzia 150 mpaka 200 kwa kila batch. Usiagize vifaranga vingi sana kwa mkupuo kwani usimamizi unakua hafifu (naongea kutokana na experience).

Muhimu zaidi kuliko vyote usianze kwa kuwa na vifaranga wengi kwa mara ya kwanza. Anza kidogo kidogo huku unapata uzoefu mwenyewe, na sio zile habari za kuambiwa. Mara nyingi watu hua wanasahau kushauri kwenye hili
Naomba machimbo ya kununua vichanganyio kwa bei ya jumla.
 
Kuku chotara wa nyama cha lazima zaidi ni starter. Wakiwa na mwezi mmoja anza kuchanganya chakula chako. Nunua kimoja kimoja (mf. Pumba, mashudu, madini, lukina etc) kwenye sources zilizo cheap zaidi changanya mwenyewe kwa uwiano unaokuwa recommended. Mchanganyo huu kwa eneo nilipo ni kama Sh. 450 kwa kilo ya chakula tofauti na mifuko ya kunununua ambayo ni Sh 1,400 mpaka 1,600 kwa kilo ya chakula.

Wakifika miezi 2.5 mpaka 3 wanakuwa na uzito wa soko.

Ukitaka faida nzuri zaidi fuga chotara kuanzia 150 mpaka 200 kwa kila batch. Usiagize vifaranga vingi sana kwa mkupuo kwani usimamizi unakua hafifu (naongea kutokana na experience).

Muhimu zaidi kuliko vyote usianze kwa kuwa na vifaranga wengi kwa mara ya kwanza. Anza kidogo kidogo huku unapata uzoefu mwenyewe, na sio zile habari za kuambiwa. Mara nyingi watu hua wanasahau kushauri kwenye hili
Asante kwa ushauri.Nimenunua juzi vifaranga20kama shamba darasa.Nahisi kuputia hawa ntajifunza mengi.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom