Kukemea ufisadi kwamponza Sumaye

Hawawezi kumuita muda umeisha na Kawawa hayupo.....Tingatinga wamelibwaga....Nyerere hayupo...so Kolimbanization is not possible
 
hongera Mh. Sumaye wakikuita kataa waambie uko busy, wakikusumbua amia Chadema

Nimeipenda hiyo.Hata Mwl.Nyerer alikwisha sema chama(CCM) SI MAMA YAKE nashangaa wengine wanaziba midomo wakati wanaumia
 
Hawa CCM watu wa ajabu sana. Ina maana wao wanakiri kwamba ni mafisadi na hawataki kukemewa? Nilishangaa gazeti lao moja (Mtanzania) limeanza kumuandama Sumaye baada ya kutoa msimamo huo. Hawa ni watu hatari wanaopaswa kutiwa adabu Oktoba 31. Shame on you CCM crooks.
 

Kukemea ufisadi kwamponza Sumaye

Na Tumaini Makene


Kauli ya tahadhari kuwataka Watanzania wawe makini katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 31 mwaka huu, wasichague watoa rushwa na mafisadi, iliyotolewa na Waziri Mkuu mstaafu Bw Frederick sumaye inaelekea kumgharimu baada ya kuwepo taarifa kwamba imekera baadhi ya vigogo wa Chama cha Mapinduzi (CCM) na sasa wanapanga kumchukulia hatua.

Vyanzo vyetu vya uhakika ndani ya CCM vimeliambiua Majira kuwa baadhi ya vigogo hao wanalalamika na kutaka Sumaye aitwe na kuhojiwa na vikao vya juu vya chama hicho kwa madai kuwa matamshi yake yamekidhalilisha chama hicho.

Hivi karibuni Sumaye, ambaye alikuwa Waziri Mkuu kwa miaka kumi mfululizo chini ya serikali ya Awamu ya Tatu iliyoongozwa na Rais Benjamin Mkapa, alinukuliwa na vyombo vya habari akitoa angalizo kuwataka wananchi kuwa makini wasichague viongozi wanaotoa rushwa ili washinde uchaguzi kwaniu hawataweza kujali matatizo yao wakishaingia madarakani.


……..Chanzo chetu kimedokeza kuwa kauli hiyo ya Sumaye imewakera baadhi vigogo wa CCM huku wengine wakidai kuwa kwa nafasi yake ndani ya chama, Sumaye hakupaswa kjukemea jambo hilo hadharani ambalo CCM imekuwa ikiandamwa nalo..….


Habari zaidi ktk Majira ya leo.
Wakati huo huo eti kuna watu wanashabikia hicho chama. Hivi ukiambiwa simba huyo, anakula watu utaendelea kumchezea? Nawaonea huruma wale wanaoshabikia ccm wakati wao ni wanyonge!
 
Jamani hivi hata kukemea rushwa ni kosa,basi hiki chama kimekufa kabisa na hata hakijui kinaelekea wapi!!!!
 
Sumaye ni moja ya viongozi wachache waliojitahidi kuiongoza Tanzania kwa uadilifu mkubwa, kwa mujibu wa Askofu Malasusa.I also agree with him.Hata enzi za Yesu alipowambia mafarisayo kuhusu udhaifu na uovu wao, waliishia kumchukia.Mungu ambariki na kumlinda Sumaye kwa kusimama kwenye ukweli.Siku zote Mungu wa Ibrahi, Isaka na Jakobo amekuwa ni mwenye nguvu, na hakuna anayeweza kuzuia jambo alitakalo Muumba wetu.May God bless Tanzania
 
Hivi hawa ccm walizaliwa kututawala milele? Hata soni hawaoni, mtu anakemea ufisadi na kuwashauri mema watz, wao kwao ni SOOO.....
Nyerere alisema "ccm siyo mama yangu", Sumaye fanya kweli.........:A S 103::A S 103:
 
Sijaona mahali ambapo Sumaye kataja sisiemu jamani. Kumwita ni kumuonea!
 

Kukemea ufisadi kwamponza Sumaye

Na Tumaini Makene


Kauli ya tahadhari kuwataka Watanzania wawe makini katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 31 mwaka huu, wasichague watoa rushwa na mafisadi, iliyotolewa na Waziri Mkuu mstaafu Bw Frederick sumaye inaelekea kumgharimu baada ya kuwepo taarifa kwamba imekera baadhi ya vigogo wa Chama cha Mapinduzi (CCM) na sasa wanapanga kumchukulia hatua.

Vyanzo vyetu vya uhakika ndani ya CCM vimeliambiua Majira kuwa baadhi ya vigogo hao wanalalamika na kutaka Sumaye aitwe na kuhojiwa na vikao vya juu vya chama hicho kwa madai kuwa matamshi yake yamekidhalilisha chama hicho.

Hivi karibuni Sumaye, ambaye alikuwa Waziri Mkuu kwa miaka kumi mfululizo chini ya serikali ya Awamu ya Tatu iliyoongozwa na Rais Benjamin Mkapa, alinukuliwa na vyombo vya habari akitoa angalizo kuwataka wananchi kuwa makini wasichague viongozi wanaotoa rushwa ili washinde uchaguzi kwaniu hawataweza kujali matatizo yao wakishaingia madarakani.


……..Chanzo chetu kimedokeza kuwa kauli hiyo ya Sumaye imewakera baadhi vigogo wa CCM huku wengine wakidai kuwa kwa nafasi yake ndani ya chama, Sumaye hakupaswa kjukemea jambo hilo hadharani ambalo CCM imekuwa ikiandamwa nalo..….


Habari zaidi ktk Majira ya leo.

Sumaye ni majeruhi wa kisiasa, kauli zake hazina uzito anatapatapa kuponya vidonda na makovu ya kushindwa Urais na Kikwete 2005 alikuwa wapi kutuambia hayo siku zote? Vidonda vya wenye kisukari haviponi haraka, kwa maelezo zaidi akamwone daktari wa tiba ya ugonjwa wa kisiasa
 
Jamani Wana JF,

CCM hawawezi kumwita Sumayi mbona its very simple si wange muanzia Hosea na PCCB yake na wanao miliki Runinga hapa Nchini si twayaona matangazo yao huko ivi huyo atake mwita Sumayi ni mbumbu kabisa na mjinga.

Mwalimu aliwaambia ingawa hivi vyama vya siasa bado vichanga ila mjifunze jinsi ya kutawala nchi katika mfumo wa vyama vingi na sasa hivyo vyama mwalimu alivyovisema 1995 ni vimekuwa sasa tena vyatisha kabisa. Ivi mpaka sasa hawa viongozi wa CCM hawakulijua hilo?kubweteka kwenye madaraka ni kubaya sana, kweli usemi wa Kolimba CCM imekosa DIRA ndio sasa unajidhihilisha bila ubishi

Na tukimaliza tu uchaguzi natoa angalizo kwa viongozi wote wa CCM katika mikutano ijayo mtapukutika kama mpunga unavyo kobolewa esp mafisadi au wale wote walioka karibu na hao mafisadi kwani najua UVCCM wamejipanga haswa kwani wameisha gundua CCM ikifa basi kuirudisha ita kuwa ni kazi sana na haitachukua miaka michache kurudi ni miaka zaidi hata 10 sasa tizama itakavyo gharimu kwahiyo wale wote waliokuwa wakikiongoza CCM kwa malengo yao waanze kukaaa mkao wa kuondoka kwani UVCCM wanakuja kukisafisha chama within two years mtaniambia
 
Sumaye naye bwana............. nilidhani yupo kama hayupo kumbe yupo lakini hayupo. Kuna tetesi alikwenda kuongeza elimu ya chuo kikuu marekani ili agombee Urais 2015. pole pole anajisafishia njia kwa mbinu mbadala.
 
Nchi yetu chini ya CCM ukikemea maovu unaitwa msaliti wa chama.
Ama kweli tulipofika sasa hakuna demokrasia.

Najua wataanza kumuandama zaidi ya alivyostaafu.
Kuna watu wana visasi we acha tu
 
Sijaona mahali ambapo Sumaye kataja sisiemu jamani. Kumwita ni kumuonea!

ndugu hukusoma hesabu za mafumbo, Sumaye katumia lugha ya mafumbo wakati anajua kwa ukweli kwamba maneno aliyotumia katika mafumbo yake ndiyo yaliyokipa misukosuko chama chake kwa takribani miaka 3.
 
Sumaye anajua anachofanya.... tofauti na viongozi wengi, yeye baada ya kuongoza alipata nafasi ya kufanya post-moterm ya tenure yake...

Kwa hili, BIG UP sana Sumaye

Wewe si zero tena
 
ndugu hukusoma hesabu za mafumbo, Sumaye katumia lugha ya mafumbo wakati anajua kwa ukweli kwamba maneno aliyotumia katika mafumbo yake ndiyo yaliyokipa misukosuko chama chake kwa takribani miaka 3.

And you continue supporting CCM.
Wana JF! mnahitaji jingine jipi kujua wanaoisuport ccm Ni mafisadi.
Huyu ni supporter wa CCM No.1 humu ndani. Someni majibu yake na muweke tafakari.
Asante Mungu kwa kuendelea kutufunulia mengi.
 
CCM wanajua kwamba wako kwa ajili yao binafsi na ndio maana wanajaribu kila njia kustick pamoja, maana as individual hawawezi kusimama.

Ndugu Sumaye tuko na wewe, wamejuaje unawasema kama sio kwamba ni wanafanya maovu uliyayataja? Nakushukuru kwa ujasiri wako kutamka na kukemea maovu, kwani kuna viongozi wengi ambao wamemaliza uongozi wanashindwa kusema yaliyo kweli mfano: Salim, Mkapa, Msuya, Mwinyi. Wote wanaona maovu CCM inayoyatenda kuwaangamiza wananchi lakini wameamua kuweka pamba masikioni na kuvaa miwani za mbao. Wanasahau kwamba siku ya mwisho watahukumiwa na mola na pia wananchi waTazania bado tunawalipia nyumba na gharama zao kwa jasho letu sisi as tax payers.

Tumeona kwenye chaguzi za nchi nyingine viongozi wastaafu wanasimama na mgombea ambao wanaona anafaa kuiongoza nchi na sio ni wa chama gani, wakijua kwamba huyo mgombea yuko kwa maslahi ya wananchi na nchi. Na mara nyingine ni wa chama ambacho ni kipinzani, lakini kwakuwa ni bora yeye anampa support.

Viongozi wetu wa zamani should feel ashamed......they have put morals and ethics on the side. Ni wakati wabadilike.
 
Nashangazwa mnno na watanzania wanao muunga mkon Sumaye kwa kukemea rushuwa .Kwani alipokuwa Waziri Mkuu ndani ya serkali ya Mkapa ndipo kipindi pekee cha kihistoria kwa nchi yetu kuwa na wimbi kubwa la ulaji wa rushwa kuliko kipindi kingine chochote kilichowahi kutokea. KUanzia Bossz wake mwenyewe had kufiki ngazi ya muhudumu wa offisi wote walikula rushwa sasa kama yeye achukia rushwa mbona wakati ule hakukemea hiyo rushwa?. Boss wake(Mkapa) aliuza kila rasilimali ya Watanzania katika mazingira ya kirushuwa-rushuwa.Nayeye mwenyewe kujiuzia mgodi kwa mali kauli na kujiwekea vitegauchumi huko Afrika ya Kusini. Je yote hayo yeye Sumaye hakuyajua?. Mimi ninaamini kama sumaye angelikuwemo katika kinyang'anyiro cha kugombea uongozi asingeyasema hayo.
 
Sumaye,you want to be a really hero?...then stand on what you believe
 
Back
Top Bottom