Kimeo ni kiungo muhimu kwenye mwili wa binadamu. Kukikata ni sawa na ukeketaji!
Utajiona unatibu kitu unachokidhania wewe lakini ukatengeneza tatizo lingine baya zaidi.
Naomba kujua kitaalam kama kukata kimeo kwa watoto wanaokohoa kama ni tiba au ni imani tu za watu.
Tanzania bado tupo katika kipindi cha mpito cha kutumia tiba za kudhani kuelekea tiba za kisasa ambazo zimefanyiwa utafiti wa kisayansi. Mtakumbuka miaka michache iliyopita watoto wenye homa walikuwa wanango'lewa meno ya plastik! na wapo waliodai wamepona homa, halafu watoto wenye degedege walikuwa wanatiwa kwenye ungo wanapepetwa na wakati mwingine kuwakojolea ati ndio dawa, na wapo wanaodai kuwa inaponesha degedege! wopo waliokuwa wanaumwa na kichwa halafu kichwa kinachanjwa ati wanatoa damu chafu (huku hawajui chanzo) pia wapo wanaodai inaponesha! Na sasa tuna tiba ya Loliondo ambayo nayo tunaambiwa inaponesha. Hiyo ni mifano tu.
Kama kukata kimeo kungekuwa kunaponesha basi tiba hiyo ingepatikana hata hospitalini. Maana itakuwaje waweze kupasua kichwa, moyo, macho, mapafu nk. washindwe kukata kimeo? Kifupi kwa mazingira ya kawaida kukata kimeo hakuponeshi na tena kuna madhara.
Mimi nilisumbuliwa sana kifua baada ya kukata kimeo,kifua kimeacha afya imerudi na hakuna madhara yoyote yaliyonikuta. Ingekuwa haisadii usingeona iyo huduma inatolewa miaka nenda rud japo kuwa kitaalam hairuhusiwi. Na uthibitisho ya watu km 3 imewasaidia.
Nb: apply mbayuwayu skills.
Dr. Ole ambaye ni mtaalam wa ENT pale Magomeni ambaye alikuwa Daktari Bingwa (sijui kama bado yupo) Muhimbili anakata Kimeo!!! Sijui anatumia utaalam au ni nini? Hebu wataalam wa ENT watupe elimu kwa hili.
HII NI IMANI,MAZOEA ,UKOSFU WA ELIMU ,DESTURI ZA WATU/MAHALI FULANI.UKWELI NI KWAMBA KIMEO HUREFUKA KULINGANA NA KILA MTU ALIVYOUMBWA.HAIWEZEKANI KIKAZIDI UREFU WA KAWAIDA LABDA KAMA KUNA TATIZO LA UGONJWA AU KUGONWA (INFECTION/IMFLAMMATION/INJURY) AU UMBILE POTOFU(HEREDITARY ABDOMARLITY).KAZI KUU YA KIMEO NI KUSAIDIANA NA KINYWABUCAL CAVITY),MFUPA WA ULIMI(HYOID BONE) NA KIUNGO KINGINE(LARNX)ILI KUWEZESHA CHAKULA KUMEZWA BILA KUINGIA KWENYE KOO LA HEWA NA SAUTI.KWAHIYO KUKATA KIMEO UNAHARIBU MFUMO WOTE HUO WA UMEZAJI CHAKULA.PILI HUWEZI KULETA UGONJWA (INFECTION),USAHA AMBAO UKIMEZWA NAO NI TATIZO JINGINE NA KWA KUWA KIUNGO HICHO PIA NI KIHUSISHI KATI JICHO,PUA NA KOO MADHARA YANAWEZA KUWA MAKUBWA ZAIDI.NA KUBWA ZAIDI VIFAA VINAVYOTUMIKA VISIWE SAFI(STERILE)HIVYI KUPATA MAGONJWA AMBUKIZI MFANO UKIMWI NK.TUACHANE NA MILA POTOFU ,ELIMU ITOLEWE ZAIDI NA VYOMBO VYA HABARI Anatomy and functionThe epiglottis guards the entrance of the glottis, the opening between the vocal folds. It is normally pointed upward while one is breathing with its underside functioning as part of the pharynx, but while one is swallowing, elevation of the hyoid bone draws the larynx upward; as a result, the epiglottis folds down to a more horizontal position, with its superior side functioning as part of the pharynx. In this manner it prevents food from going into the trachea and instead directs it to the esophagus, which is posterior.
The epiglottis is one of nine cartilaginous structures that make up the larynx (voice box). While one is breathing, it lies completely within the pharynx. When one is swallowing it serves as part of the anterior of the larynx.Mucosa
The entire lingual surface and the apical portion of the laryngeal surface (since it is vulnerable to abrasion due to its relation to the digestive tract) are covered by a stratified squamous non-keratinized epithelium. The rest of the laryngeal surface on the other hand, which is in relation to the respiratory system, has respiratory epithelium: pseudostratified, ciliated columnar cells and mucus secreting Goblet cells.Infection of the epiglottis
In children, the epiglottis will occasionally become infected with Haemophilus influenzae and Streptococci in the trachea, causing massive inflammation, called "Epiglottitis". This condition has become rare in countries where vaccination against Haemophilus influenzae (Hib) is administered
Mkuu pamoja na maelezo yako mazuri umechanganya mambo mno. Alichouliza ni ukataji wa kimeo ambao kwa kiingereza huitwa uvula, sio Epiglottis ambayo kwa kiswahili huitwa kidaka tonge. epiglottis na uvula ni viungo tofauti kabisa kwa maana vilipo na kazi zinazofanywa
unachokiona kwenye hiyo picha ambacho kimepewa na 3 ndio kimeo ambacho hukatwa na waganga wa kienyeji. Na hiyo picha hapo chini imekuonesha epiglottis au kidaka tonge.!!
Kuna ndugu yangu mmoja mwanae alikuwa anasumbuliwa nacho sana na kikohozi kiasi cha kushindwa hata kula,kapelekwa kwa mtaalam mitaa ya Temeke sasa mzima.Ni imani tu za watu wala si dawa.
Dr. Ole ambaye ni mtaalam wa ENT pale Magomeni ambaye alikuwa Daktari Bingwa (sijui kama bado yupo) Muhimbili anakata Kimeo!!! Sijui anatumia utaalam au ni nini? Hebu wataalam wa ENT watupe elimu kwa hili.
Ni imani lakini inasaidia, NB: Wataalam wa kukata kimeo kwa miaka hii inaweza kuwa ni hakuna. Zaidi sana watakata mpaka nyama then utamfanya mtoto apate kansa.
Jamani Mi Naushahidi wa kutosha kuhusu ukataji wa vimeo kuwa unaondoa kabisa la kukohoa haswa kwa watoto. Wadogo zangu wengi wamekatwa vimeo na kweli wamepona kabisa. Tatizo Letu tunaponda sana Traditional Medecine Wakati hatujapatwa na matatizo kama haya lakini kama kweli upo na mtoto ambaye anatatizo kama hili yaani we mwenyewe utalia kuona jinsi gani mtoto anapoteseka kwa kikohozi mpaka mbavu zinabana. Na hao wanaobisha na kuona kuwa ni mambo ya kiswahili waende kwa Nassoro Mkata Vimeo Wakaone Idadi ya watu wanaokuepo hapo na status zao ili wajue.