Kalamu Nzito
JF-Expert Member
- Aug 13, 2015
- 318
- 662
Wakuu nina degree ya sheria ambayo nimeipata kwa mbinde sana (mishale mingi bado kidogo ni-disco). Nimeenda law school nikasema ngoja nikaze walau nitoke first seat kusafisha maumivu ya degree, ila wapi. Nikakamatwa vimeo vitatu somo moja (pale law school tunaita “full suit”). Nimechomoa kimeo kimoja. Hivyo vingine viwili huu unaenda mwaka wa tatu sijafanikiwa kuchomoa.
Sina ajira mpaka sasa. Naishia kufanya tu internship bila malipo. Sijui naanzia wapi nifanikiwe na umri nao unasogea. Moyo unanisukuma kukata tamaa lakini katika hilo nimeshinda kwani bado ninalo tumaini kwamba nitafanikiwa tu.
Ombi langu kwenu;
1. Kama kuna sehemu wanashea nafasi za kazi/fursa yoyote naaomba nikumbukwe.
2. Kama unaweza binafsi kuniunga mahali nikafanya kazi basi nitashukuru sana.
Mwisho kabisa, wakuu hii maisha inatunyoosha wallah Mungu atusaidie sana.
Sina ajira mpaka sasa. Naishia kufanya tu internship bila malipo. Sijui naanzia wapi nifanikiwe na umri nao unasogea. Moyo unanisukuma kukata tamaa lakini katika hilo nimeshinda kwani bado ninalo tumaini kwamba nitafanikiwa tu.
Ombi langu kwenu;
1. Kama kuna sehemu wanashea nafasi za kazi/fursa yoyote naaomba nikumbukwe.
2. Kama unaweza binafsi kuniunga mahali nikafanya kazi basi nitashukuru sana.
Mwisho kabisa, wakuu hii maisha inatunyoosha wallah Mungu atusaidie sana.