Kukata kimeo

Hawa hawajui chochote.huu sio ushirikina ni matibabu tosha .Sisi kwetu wote tumekatwa kimeo kwasababu tumerithi kuwa na vimeo virefu ambavyo huwa vinagusa sehemu za chini za koromeo nakusababisha kukohoa kavukavu wakati mwingine husababisha kutapika.na huwezi kupona kwa dawa ila operation.lla sio tiba ya kifua kikuu.serekali inawasiwasi na vifaa

Again, vitu vinafanywa kwa mazoea tu...babu, bibi, mjomba, shangazi, baba n.k walikatwa vimeo vyao virefu basi na sisi tunakata na kukata wanetu. Hivi unafikiri ni kwenu tu na hamna sehemu nyingine duniani wana vimeo virefu? na huko nako wanakata? Kukohoa kikohozi kikavu hadi kutapika ni ugonjwa ulikuwa common sana miaka ya nyuma ukiitwa Diphteria, na ndio ulipelekea chanjo yake ikajumuishwa kwenye chanjo ilikuwa ikiitwa DPT (Diphtheria Pertusis Tetanus) unachoma paja la kushoto..siku hizi wamengeza inaitwa DPT-HHib. Tangu watoto waanze kuchanjwa siku hizi huoni hili tatizo, na halikutokomezwa na wakata vimeo...bali DPT vaccine! Machapisho yapo, lete machapisho yako kuwa wakata vimeo wakichangia kutokomeza hilo tatizo.
 
We Mamndenyi wee...nani kakuambia hizi hadithi? Sijawahi kuona maandiko/chaposho yanayosema hivyo!
Kinachonishangaza ni kuwa kwa nini watu wanapona wanapokatwa kimeo?Kama si kitaalam ni nini?
 
Kinachonishangaza ni kuwa kwa nini watu wanapona wanapokatwa kimeo?Kama si kitaalam ni nini?

Una uhakika gani kwamba wanapona? Kuna chapisho zilizosema hivyo kama evidence? kama hakuna evidence haya mnayosema yametoka wapi? Au hata confession ya mtu mmoja tu basi ndio evidence kuwa kitu fulani kinawork?

Hivi unafikiri kama kweli kukata vimeo kunawork, mpaka sasa kungekuwa hakuna tuu scientific publications kuelezea success yake na jinsi ya kufanya hivyo safely! Badala ya inavyofanyika sasa na risk zote hizi za HIV, other bacterial infections, bleeding etc?!
 
HII NI IMANI,MAZOEA ,UKOSFU WA ELIMU ,DESTURI ZA WATU/MAHALI FULANI.UKWELI NI KWAMBA KIMEO HUREFUKA KULINGANA NA KILA MTU ALIVYOUMBWA.HAIWEZEKANI KIKAZIDI UREFU WA KAWAIDA LABDA KAMA KUNA TATIZO LA UGONJWA AU KUGONWA (INFECTION/IMFLAMMATION/INJURY) AU UMBILE POTOFU(HEREDITARY ABDOMARLITY).KAZI KUU YA KIMEO NI KUSAIDIANA NA KINYWABUCAL CAVITY),MFUPA WA ULIMI(HYOID BONE) NA KIUNGO KINGINE(LARNX)ILI KUWEZESHA CHAKULA KUMEZWA BILA KUINGIA KWENYE KOO LA HEWA NA SAUTI.KWAHIYO KUKATA KIMEO UNAHARIBU MFUMO WOTE HUO WA UMEZAJI CHAKULA.PILI HUWEZI KULETA UGONJWA (INFECTION),USAHA AMBAO UKIMEZWA NAO NI TATIZO JINGINE NA KWA KUWA KIUNGO HICHO PIA NI KIHUSISHI KATI JICHO,PUA NA KOO MADHARA YANAWEZA KUWA MAKUBWA ZAIDI.NA KUBWA ZAIDI VIFAA VINAVYOTUMIKA VISIWE SAFI(STERILE)HIVYI KUPATA MAGONJWA AMBUKIZI MFANO UKIMWI NK.TUACHANE NA MILA POTOFU ,ELIMU ITOLEWE ZAIDI NA VYOMBO VYA HABARI Anatomy and functionThe epiglottis guards the entrance of the glottis, the opening between the vocal folds. It is normally pointed upward while one is breathing with its underside functioning as part of the pharynx, but while one is swallowing, elevation of the hyoid bone draws the larynx upward; as a result, the epiglottis folds down to a more horizontal position, with its superior side functioning as part of the pharynx. In this manner it prevents food from going into the trachea and instead directs it to the esophagus, which is posterior.
The epiglottis is one of nine cartilaginous structures that make up the larynx (voice box). While one is breathing, it lies completely within the pharynx. When one is swallowing it serves as part of the anterior of the larynx.Mucosa
The entire lingual surface and the apical portion of the laryngeal surface (since it is vulnerable to abrasion due to its relation to the digestive tract) are covered by a stratified squamous non-keratinized epithelium. The rest of the laryngeal surface on the other hand, which is in relation to the respiratory system, has respiratory epithelium: pseudostratified, ciliated columnar cells and mucus secreting Goblet cells.Infection of the epiglottis
In children, the epiglottis will occasionally become infected with Haemophilus influenzae and Streptococci in the trachea, causing massive inflammation, called "Epiglottitis". This condition has become rare in countries where vaccination against Haemophilus influenzae (Hib) is administered

Waweza kuwa na ujumbe mwanana ; lkini umekiuka sheria za uandishi ndg. kiasi kwamba inaumiza kuisoma kwa wengine kam sio kuchosha!

Tukirudi kwenye topic; nilishuhudia utotoni mwenzetu akikatwa kimeo na baaday alikuja kufariki wakati huo nina miaka 6! Nilizilaani tiba asilia (mtanisamehe) na baadaye ukubwani nikajiapiza sitatumbukia huko milele; Huwa nalikumbuka tuukio lile kama vile ni jana!
 
Una uhakika gani kwamba wanapona? Kuna chapisho zilizosema hivyo kama evidence? kama hakuna evidence haya mnayosema yametoka wapi? Au hata confession ya mtu mmoja tu basi ndio evidence kuwa kitu fulani kinawork?

Hivi unafikiri kama kweli kukata vimeo kunawork, mpaka sasa kungekuwa hakuna tuu scientific publications kuelezea success yake na jinsi ya kufanya hivyo safely! Badala ya inavyofanyika sasa na risk zote hizi za HIV, other bacterial infections, bleeding etc?!
Bado kichwa yangu inauma kwa hili jambo mkuu.
 
Mimi nilisumbuliwa sana kifua baada ya kukata kimeo,kifua kimeacha afya imerudi na hakuna madhara yoyote yaliyonikuta. Ingekuwa haisadii usingeona iyo huduma inatolewa miaka nenda rud japo kuwa kitaalam hairuhusiwi. Na uthibitisho ya watu km 3 imewasaidia.
Nb: apply mbayuwayu skills.[/QUOTsamahani naomba na mm kukuulizaa ulipona baada ya mda gani sababu ata mm nimekata nikiambiawa ntapona baada ya sikuu tatu lakini leo siku ya tatu bado kinaniuma yani sijaponaa sass naogopaa au amenikata vibaya au nivute subira uwenda nikaponaa
 
Jaman naomben msaada nilikata kimeo nna siku ya tatu sasa lakini sijapona nahisi maumivu ya sehemu niliyokata Na watu wengi waliniambia kuwa nitapona baada ya siku tatu lakini sioni mabadilikoo bado napata maumivu naomba mnishauri nifanyaje... Au amenikata vibaya??
 
Mimi nilisumbuliwa sana kifua baada ya kukata kimeo,kifua kimeacha afya imerudi na hakuna madhara yoyote yaliyonikuta. Ingekuwa haisadii usingeona iyo huduma inatolewa miaka nenda rud japo kuwa kitaalam hairuhusiwi. Na uthibitisho ya watu km 3 imewasaidia.
Nb: apply mbayuwayu skills.
Kabisa hata mm hiiii hali inanisumbua sana nimeangaliwa nimeambiwa nina kimeo nakweri kinaonekana kwakweri nimepima kira ugonjwa sina kifua sina lakini nakuua napataka maumivu kifuani nikaambiwa kimeo kinasababidha nikikikata kitaacha kuuuma kwa mana kimeo kimekua kirefuu kinaonekana
 
Nimermtoka kumkata mtoto wa 3yrs mwezi uliopita.
Kabla ya hapo alikua anakohoa sana na akila chakula anatapika. Ila baada ya kukata tu kawa mpya.
Hapo kwa mtaalam nimeenda nikakuta foleni ndefu ya watu wakisubiri huduma.
 
Back
Top Bottom