Riwa
Platinum Member
- Oct 11, 2007
- 2,607
- 3,065
Hawa hawajui chochote.huu sio ushirikina ni matibabu tosha .Sisi kwetu wote tumekatwa kimeo kwasababu tumerithi kuwa na vimeo virefu ambavyo huwa vinagusa sehemu za chini za koromeo nakusababisha kukohoa kavukavu wakati mwingine husababisha kutapika.na huwezi kupona kwa dawa ila operation.lla sio tiba ya kifua kikuu.serekali inawasiwasi na vifaa
Again, vitu vinafanywa kwa mazoea tu...babu, bibi, mjomba, shangazi, baba n.k walikatwa vimeo vyao virefu basi na sisi tunakata na kukata wanetu. Hivi unafikiri ni kwenu tu na hamna sehemu nyingine duniani wana vimeo virefu? na huko nako wanakata? Kukohoa kikohozi kikavu hadi kutapika ni ugonjwa ulikuwa common sana miaka ya nyuma ukiitwa Diphteria, na ndio ulipelekea chanjo yake ikajumuishwa kwenye chanjo ilikuwa ikiitwa DPT (Diphtheria Pertusis Tetanus) unachoma paja la kushoto..siku hizi wamengeza inaitwa DPT-HHib. Tangu watoto waanze kuchanjwa siku hizi huoni hili tatizo, na halikutokomezwa na wakata vimeo...bali DPT vaccine! Machapisho yapo, lete machapisho yako kuwa wakata vimeo wakichangia kutokomeza hilo tatizo.