Intern unapangiwa sehemu mbalimbali, na mkataba wa intern kikawaida ni mwaka mmoja. So sehemu ambayo unafanyia intern wakikupenda wanakuchukua moja kwa moja ndio mana unaweza sema wamepata intern toka TaESA.
Kumbuka hawatoi ajira permanent, hiyo kazi ni ya Utumishi. Ila CV yako itakuwa inabustiwa kupitia wao. Kuna jamaa zangu kadhaa waliingia intern shirika flani TaESA akiwa ndo kawaweka. Utendaji wao wa kazi ulipelekea mmoja kupewa mkataba wa kudumu.
Intern hizo unapangiwa sehemu yoyote tu ile yenye uhitaji ila sio pale kwao. Mfano unaweza pelekwa TRA, TANESCO, NGOs mbalimbali. Mfano kuna mwaka flani nilienda omba intern Red Cross nkaambiwa wao wanachukua watu kutoka TaESA, so nkajisajili kwanza kule.