Kuishi Mjini vs kuishi kwenye Vijiji vilivyochangamka

mwanyaluke

JF-Expert Member
Jan 22, 2015
473
1,448
Kazi unazofanya ni miongoni mwa vitu ambavyo vinakuchagulia mahala pa kuishi. Nimeishi sehemu nyingi za mjini na kijijini, nilichokiona mimi maisha ya mjini ni mazuri ukiwa na pesa nyingi na maisha ya kuishi kwenye kijiji kilichochangamka ni mazuri zaidi hata ukiwa na pesa kiasi.

Nimechukua location ya shamba langu moja lilipo na mara nyingi huwa nikitoka mjini huwa napumzika hapo na kulala, nimejikuta napenda sana haya mazingira, pana maji, umeme, barabara ipo ya uhakika, soko dogo na sehemu za starehe zipo, network ipo, ni sehemu ambayo nikiwa hapo shamba napata utulivu sana wa akili, sisumbuliwi na mtu.

Hii ipo tofauti na kwangu mjini mara umelala unasikia geti linagongwa unatoka mtu anakwambia nilikuwa nauza icecream au nasajili line, mara usikie mke na mume wanagombana, ukitoka unyoshe miguu mara umekoswa na bodaboda, mara huyu kakusimamisha akupige mizinga nk full kero.

Kwa upande wako ni sehemu gani nzuri kuishi katikati ya mji au pembeni kidogo ya mji.
 
Huwezi kulinganisha maisha ya mjini na kijijini, labda mjini kama unaishi Mbagala Manzese, na maeneo ya slums kama hayo, hamna kijiji kiliochagmka kuzidi town labda unasemea utulivu sio mambo mengine, hata Mutume wa Allah alishauri sana ufuasi wake waishi mijini kuna barakah tere za kupata riziki kuliko vijijini, kama huna pesa ya kulipia utilities mjini panakua pachungu kwa kweli.
 
Mkuu kama una shamba na kazi inakuruhusu kukaa kijiji kilichochangamka ni jambo jema
 
Huwezi kulinganisha maisha ya mjini na kijijini, labda mjini kama unaishi Mbagala Manzese, na maeneo ya slums kama hayo.......hamna kijiji kiliochagmka kuzidi town labda unasemea utulivu sio mambo mengine, hata Mutume wa Allah alishauri sana ufuasi wake waishi mijini kuna barakah tere za kupata riziki kuliko vijijini, kama huna pesa ya kulipia utilities mjini panakua pachungu kwa kweli.
Nilishi dar kimara, manzese, mwenge dah yale maisha yalikuwa ya uwongo sana , joto ,nyumba zimebanana nilichemka aisee
 
Huwezi kulinganisha maisha ya mjini na kijijini, labda mjini kama unaishi Mbagala Manzese, na maeneo ya slums kama hayo.......hamna kijiji kiliochagmka kuzidi town labda unasemea utulivu sio mambo mengine, hata Mutume wa Allah alishauri sana ufuasi wake waishi mijini kuna barakah tere za kupata riziki kuliko vijijini, kama huna pesa ya kulipia utilities mjini panakua pachungu kwa kweli.
Sasa watu wengi mjini si ndiyo wanaishi maeneo kama hayo, Tandale, Manzese, Mwananyamala et al
 
Napenda sana kuishi maeneo kama hayo, na nilishajaribu changamoto nikakumbana na uchawi mwingi, usalama mdogo na asilimia kubwa ya watu maeneo Yale ilikuwa jamii moja
 
Napenda sana kuishi maeneo kama hayo, na nilishajaribu changamoto nikakumbana na uchawi mwingi, usalama mdogo na asilimia kubwa ya watu maeneo Yale ilikuwa jamii moja
Kwa ujinga wa kuamini uchawi hutapenda kuishi mahali popote.
 
Kwa ujinga wa kuamini uchawi hutapenda kuishi mahali popote.
Ujinga umekujaje? Huoni kwamba wewe ndio mjinga zaidi? Toa maoni Yako bila kukashivu ya mwenzako huo ndio uelevu ila hapa kama Mimi nitakuwa mjinga basi wewe utakuwa mpumbavu kiwango Cha mwisho
 
Maeneo ya wilayani siku hizi yanabamba kuliko kwenye majiji...uwe na mpunga kiasi tu wa bia mbili tatu
Kuna jamaa mmoja mweusi ana lafudhi kama ya Uingereza anazunguka Tanzania na kupiga picha kwenye miji mikubwa na midogo, analinganisha, hali ya hewa, bei ya vyakula, usafi etc.

Anasema Tukuyu ukiwa na buku tu unapata chakula kingi sana

Alinivutia sana.

 
Ujinga umekujaje? Huoni kwamba wewe ndio mjinga zaidi? Toa maoni Yako bila kukashivu ya mwenzako huo ndio uelevu ila hapa kama Mimi nitakuwa mjinga basi wewe utakuwa mpumbavu kiwango Cha mwisho
Kuamini kuwa kuna wachawi wanaweza kukudhuru ni ujinga sana
 
Mjini ni kuzuri sana ila mjini kama ni ungaunga mwana au mishahara hii ya laki nane ndugu kuzifikia ndoto zako ni kazi sana.

Ila kuna vijiji fursa nje nje na pia uhakika wa mzunguko wa hela kiasi kwamba ukituliza akili itabaki ni story.

Speaking from exprience niko bush sana namtumikia mmama wa kizenji japo weekend niko mjini kubadilisha akili.

Shida ya vijijini ni umbea na kufuatiliana sana kiasi kama huna moyo utapakimbia ila ukiwapuuza basi umemaliza.
 
Maeneo ya wilayani siku hizi yanabamba kuliko kwenye majiji...uwe na mpunga kiasi tu wa bia mbili tatu
Tukuyu nilipita tu ila kuna greenish ya ukweli sana..ila zipo sehemu nyingi tu kama hizo bongo
 
Back
Top Bottom