Nimefuatilia sana mijadala mingi inaoendelea kuhusiana na tamko la Serikali juu ya mabus ya Usafiri Mikoani na matumizi ya Stendi ya Magufuli.
Ni hivi, miji yote mikubwa duniani ina Kituo kikuu cha Usafiri wa mabus au treni (Central Station) ambapo mabus yote hufikia pale kisha kuna usafiri wa ndani ambao kwa mji wetu wa Dar kuna usafiri wa Dart, taxi, Uber, Daladala na kadhalika ambao kazi yao huunganisha safari za abiria kule waondako.
Hii ni mipango miji inayolenga uboreshaji wa huduma, kupunguza msongamano wa magari mijini na usalama wa wananchi barabarani. Msafiri wa bus hawezi kuwa na haki zote barabarani pasipo kuzingatia watu wengine katika biashara zao.
Sii kila mfanya biashara ya Usafiri ana mabus ya kwenda Mikoani wengine shughuli zao huishia mjini na ndio riziki zao zinavyopatikana na mzunguko wa fedha unavyotakiwa. Hatuwezi kuondoa Umaskini nchini kwa huruma na sadaka za uongo wakati hawa ni wafanya biashara sio NGOs.
Ikiwa Stendi ya Magufuli ina mapungufu basi ni vema yakajadiliwa hayo mapungufu yakaboreshwa kuliko kuweka madai mengine ya uongo kama kwamba wananchi ni wajinga sana.
Isitoshe tunajua, hakuna bus linalotoza nauli moja kwa wasafiri wote, tiketi hutolewa kulingana na msafiri anaposhukia. Ukisema Pugu utatozwa gharama yake tofauti na yule anayekwenda Kariakoo au Mbezi.
Kisha hawa hawa wenye mabus ndio wana wapiga debe! Bei ya tiketi huongezwa kwa faida zaidi halafu unaambiwa ati wanasaidia maskini wasioweza kupanda Dart au Daladala.
Inawezekanaje bus linatoka Kigoma na samaki wamefungiwa kwenye buti la bus halafu anapelekwa Mpaka Kariakoo sokoni, waseme ati msafiri anasaidiwa! Samaki kwenye buti la mizigo na masanduku ya nguo za watu unasema unamsaidia nani?
Kisha Hakuna mzigo unaosafirishwa bure hata ukituma kikasha cha ubuyu utatozwa gharama ya usafiri.
Ifike pahala Watanzania tuache mazoea, tujifunze kuishi kwa Sheria na taratibu zilowekwa ndio Ustaarabu. Kutetea wenye mabus ambao wanadai hupeleka wateja wao Kariakoo, Chanika au Mbagala BURE wakati tunajua ndiko wao hulaza magari yao ni kutufanya wananchi wote wapumbavu kutetea Upumbavu - Haikubaliki.
Ni hivi, miji yote mikubwa duniani ina Kituo kikuu cha Usafiri wa mabus au treni (Central Station) ambapo mabus yote hufikia pale kisha kuna usafiri wa ndani ambao kwa mji wetu wa Dar kuna usafiri wa Dart, taxi, Uber, Daladala na kadhalika ambao kazi yao huunganisha safari za abiria kule waondako.
Hii ni mipango miji inayolenga uboreshaji wa huduma, kupunguza msongamano wa magari mijini na usalama wa wananchi barabarani. Msafiri wa bus hawezi kuwa na haki zote barabarani pasipo kuzingatia watu wengine katika biashara zao.
Sii kila mfanya biashara ya Usafiri ana mabus ya kwenda Mikoani wengine shughuli zao huishia mjini na ndio riziki zao zinavyopatikana na mzunguko wa fedha unavyotakiwa. Hatuwezi kuondoa Umaskini nchini kwa huruma na sadaka za uongo wakati hawa ni wafanya biashara sio NGOs.
Ikiwa Stendi ya Magufuli ina mapungufu basi ni vema yakajadiliwa hayo mapungufu yakaboreshwa kuliko kuweka madai mengine ya uongo kama kwamba wananchi ni wajinga sana.
Isitoshe tunajua, hakuna bus linalotoza nauli moja kwa wasafiri wote, tiketi hutolewa kulingana na msafiri anaposhukia. Ukisema Pugu utatozwa gharama yake tofauti na yule anayekwenda Kariakoo au Mbezi.
Kisha hawa hawa wenye mabus ndio wana wapiga debe! Bei ya tiketi huongezwa kwa faida zaidi halafu unaambiwa ati wanasaidia maskini wasioweza kupanda Dart au Daladala.
Inawezekanaje bus linatoka Kigoma na samaki wamefungiwa kwenye buti la bus halafu anapelekwa Mpaka Kariakoo sokoni, waseme ati msafiri anasaidiwa! Samaki kwenye buti la mizigo na masanduku ya nguo za watu unasema unamsaidia nani?
Kisha Hakuna mzigo unaosafirishwa bure hata ukituma kikasha cha ubuyu utatozwa gharama ya usafiri.
Ifike pahala Watanzania tuache mazoea, tujifunze kuishi kwa Sheria na taratibu zilowekwa ndio Ustaarabu. Kutetea wenye mabus ambao wanadai hupeleka wateja wao Kariakoo, Chanika au Mbagala BURE wakati tunajua ndiko wao hulaza magari yao ni kutufanya wananchi wote wapumbavu kutetea Upumbavu - Haikubaliki.
