Kuiponya UKAWA, hawa lazima wakatwe

Kuiponya UKAWA, hawa lazima wakatwe

Sure! ts about time waamue kufanya maamuzi kwa ajili ya wananchi wanaowawakikilisha na sio kuleta uvyama hasa kwa chadema, wakishikilia kua wao ndio wenye nguvu na lazima mgombea atoke kwao huu umoja haufiki kokote na vyama kama NLD huko they have nothing to loose kwa mvunjiko huo ila Chadema itakua kana kwamba wanauthibitishia umma kua lengo lao ni chadema kuingilia ikulu na sio kuleta mabadiliko ambayo watanzania wanayataka na wanategemea kupata kutoka umoja huo..

Lazima tuwe na ufaham mpana zaidi ya kuhua lengi la chama chochote cha siasa ni kushika dola. Haukuna lengo lingine. Hivyo katika muungani huu wa ukawa (ambao sio chama) ni lazi.a yawepo makubaliano chanya kwa washirika wote juu ya kupata wagombea katka nafasi za uongozi basipo kukifuta chama kingine, ndio maana maafikiano yanachukua muda mrefu kwa kuzingatia hayo hapo juu.

Huwezi eti ukamuweka Mbatia au Makaidi kugombea nafasi ya urais kisa tu eti kunetralize migongano kati ya cuf na chadema! Tambua pia kuwa kunaugum kwa katiba hii.

Mfano, iwapo watamsimamisha Prof. Lipumba lazima Makamu atoke zanziba kwa maana either awe mwanachama wa chedema, nccr au Nld. Swali ni je kunapresidential figure kutoka makundi hayo kwa zanziba?

Na hata ikisemekana agombee Dr. Slaa lazima makamu atoke Zanziba lets say Juma Duni haji. Huyu atalazimishwa kikatiba achukue kadi ya chadema!

Haya mambo ni magumu ndio maana watu wenye akilo zao wamejifungia ndani mpaka sasa kupata muafaka wa jambo hili.

Na sio kulaumu tu kuwa eti Dr. Slaa anang'ng'ania au Prof. Lipumba analazimisha awe mgombea kwa mwamvuli wa ukawa. Tujifunze kuona jambo kwa lenzi ya tatu sio kusukumwa na matamanio ya nafsi zetu.
 
Nakubaliana na VUTA-NIKUVUTE kwamba UKAWA au CHADEMA wamsimamishe Tundu Lissu badala ya Dr Slaa.
Hizi ni sababu ninazoziona zinaweza mfanya Dr Slaa ashindwe vibaya dhidi ya Dr Magufuli:
1) Kura za Waislamu-Huu ndio udhaifu mkubwa wa Dr Slaa, Waislamu watakuwa radhi wakampe kura Dr Magufuli badala ya Dr Slaa.Historia ya nyuma ya Dr Slaa ndio kikwazo kikubwa cha yeye kukubalika na wapi kura wa imani hii.
2) Kura za wanawake-Wanawake wamekuwa tegemeo kubwa la CCM kama wapiga kura wao.
3) Kura za Wakristu-Kuna uwezekano mkubwa wa Dr Slaa kupata kura chache za Wakristu tofauti na uchaguzi wa 2010,anaweza kugawana za Wakrisru na Dr Magufuli.

Kwanini Mwanasheria Tundu Antipasi Mughwai Lissu ni chaguo bora?hizi ndio sababu:
1) Kura za Waislamu-Anaweza kupambana vikali na Dr Magufuli Kwenye kundi hili la wapiga kura.Ni vigumu kumnasibisha Lissu na udini.
2) Kura za vijana-Kumchagua Lissu kama mgombea wa urais kutawasisimua vijana wengi kwenda upande wake,Kifupi Lissu anauzika vizuri kwa wapiga kura vijana.
3) Kura za Wanawake-Anaweza kupambana vikali na Dr Magufuli ktk kundi hili la wapiga kura.
4) Kura za Wakristu-Anaweza pia kupambana na Dr Magufuli ktk kupata kura za Wakristu
5) Kura za wasomi-Hili ni eneo lingine ambalo linaweza kumpatia Lissu kura za kutosha.

Hoja ya katiba mpya inaweza kuwa silaha ya maangamizi ya Tundu Lissu dhidi ya CCM wakati wa kampeni.Nawasilisha.
 
Tatizo mashabiki wa Chadema wengi mawazo yao ni mgando, wao wanajua anayefaa kugombea urais ni Dr. Wilbroad Slaa tu kumbe hawajui kuna vichwa vingine vingi ambavyo vinaweza kupeperusha bendera vizuri kabisa.

Je nanyie mashabiki wa maziwa ya chai mawazo yenu ni yepikuhusu mgombea uraisi anayefaa kuliko huyu unayesema hafai
 
Lumumba jipangeni upya kutoa ushauri potofu.

1. Kura za Lipumba 2010 zilimsaidia dhaifu na hazikutosha. Mkapindua kura za Dr Slaa kama mlivyopindua za Dr Asha Rose mkatuletea pombe kana kwamba sisi wote ni walevi. Leo mnajipinda hawa wakatwe.

Upuuzi mtupu sijui kwa nini mnahaha wakati refa ni wenu UWT ni yenu wafungaji wa goli la mkono.

Tulieni kilio na kicheko zote ni kelele. Msiba na harusi zote ni sherehe. Subirini kelele za sherehe
 
Back
Top Bottom