VUTA-NKUVUTE
JF-Expert Member
- Nov 25, 2010
- 6,140
- 18,006
Nashauri tu watani zangu wa UKAWA. Nawashauri kuwakata wawili wanaotajwatajwa kuwa wana mvutano usio na mfano na kusababisha mkwamo. Saa 11 za jana zilishindwa kumaliza VUTA-NKUVUTE hiyo. Wanapaswa kukatwa au wao wenyewe wajitoe kugombea Urais kwa bendera ya UKAWA. Hata CCM yetu ilipoona Lowassa na Membe wamepania,wakakatwa. Wote walipoondolewa kwa kukatwa,mambo yakatulia.
UKAWA wanapaswa kuwakata wawili hawa. Ni mafahari katika vyama vyao na hivyo hawawezi kuishi kwenye zizi moja. Hakuna atakayekubali kushindwa hivihivi tu. Patachimbika na UKAWA kusambaratika. Maneno ya Mbatia ya jana kuwa mambo yanakwnda sawia na mgombea ameshapatikana hayana tofauti na yale ya Nape Nnauye baada ya kikao cha CC. Baadaye wakaibuka akina Nchimbi. Maneno ya Mbatia ni ya kisiasa na kidiplomasia.
Nawashauri UKAWA mambo mawili. La kwanza,kuwakata Prof. Ibrahim Haruna Lipumba na Dr. Wibrod Peter Slaa katika orodha ya wanaotaka ugombea. La pili, wamsimamishe Tundu Antipas Mughwai Lissu kupeperusha bendera UKAWA. Dr. John Pombe Magufuli,mgombea mteule wa CCM, ni heavyweight. Wa level yake ni Lissu tu wakishakatwa hao wawili. Nanyamaza nitazame na kusikia mlivyonielewa.
Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam
UKAWA wanapaswa kuwakata wawili hawa. Ni mafahari katika vyama vyao na hivyo hawawezi kuishi kwenye zizi moja. Hakuna atakayekubali kushindwa hivihivi tu. Patachimbika na UKAWA kusambaratika. Maneno ya Mbatia ya jana kuwa mambo yanakwnda sawia na mgombea ameshapatikana hayana tofauti na yale ya Nape Nnauye baada ya kikao cha CC. Baadaye wakaibuka akina Nchimbi. Maneno ya Mbatia ni ya kisiasa na kidiplomasia.
Nawashauri UKAWA mambo mawili. La kwanza,kuwakata Prof. Ibrahim Haruna Lipumba na Dr. Wibrod Peter Slaa katika orodha ya wanaotaka ugombea. La pili, wamsimamishe Tundu Antipas Mughwai Lissu kupeperusha bendera UKAWA. Dr. John Pombe Magufuli,mgombea mteule wa CCM, ni heavyweight. Wa level yake ni Lissu tu wakishakatwa hao wawili. Nanyamaza nitazame na kusikia mlivyonielewa.
Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam