Prof. Lipumba: Mbowe, Seif walikuwa wanawasiliana peke yao kuhakikisha Lowassa anakuwa mgombea UKAWA

The Phylosopher

JF-Expert Member
Mar 11, 2015
1,495
2,042
Ni aliyekuwa mwenyekiti wa CUF Profesa Ibrahim Haruna Lipumba kesho anatarajiwa kuzungumzia mgogoro unaoendelea ndani ya CUF kupitia kituo cha Clouds fm ktk kipindi kinachoruka asubuhi.

---------------------------

Updates Sept. 08, 2016
- Sikuwa na barua ya kusimamishwa uanachama mpaka waliposikia nitakuwa Clouds ndipo wakaniletea barua ya kunisimamisha. Barua ilikuwa ya tarehe 30 Agosti, 2016 na niliipata jana tarehe 7 Septemba.

- Mbunge wa Kaliua Mh. Sakaya bado ni mwanachama na Mbunge, kikao kilichofanyika kumsimamisha uanachama hakina uhalali, Mh. Sakaya ilibidi awe kwenye Kikao hicho kama Naibu katibu Mkuu Bara ambaye ni msaidizi wa Katibu mkuu ndio alikuwa anahusika kuandaa kikao lakini hakuwa na taarifa mpaka siku moja kabla ya kikao ndio akajulishwa.

- Vikao vya CUF vina utaratibu, hiki hakikufuata utaratibu maana cha kimafia.

- Vyama vinavyounda UKAWA vilikubaliana kumsimamisha Mgombea mmoja kati ya Dr. Slaa, Prof. Lipumba na Dr. Kahangwa wa NCCR Mageuzi.

- Nilikaa kikao na Dr. Slaa na Dr. Kahangwa nyumbani kwangu na tukakubaliana kwakuwa wenzetu CHADEMA wamejiandaa na wana uwezo mkubwa basi wamsimamishe Mgombea wa Urais (Dr. Slaa), CUF hatukuwa na uwezo.

- Wakati tunapanga kumbe Mbowe na Seif walikuwa wanamshawishi Lowassa ahamie CHADEMA na awe mgombea Urais.Mh Mbowe na Maalim walikuwa wanawasiliana peke yao katika kuhakikisha EL anakuwa mgombea kwa bendera ya UKAWA bila kushirikisha kamati tendaji za vyama vyao.

- Tulikuwa tumekubaliana kutosimamisha mgombea wa makapi, tulitaka mgombea aliyetoka ukawa aliyekuwa anaunga mkono rasimu ya katiba ya Jaji Warioba, Lowassa hakuwa anaunga katiba ya Jaji Warioba.

- Nilimshawishi Warioba agombee Urais kupitia UKAWA, Alikataa na kusema yeye bado ni mwanaCCM.

Lipumba: Seif anaiuza CUF bara kwa bei poa

Kufukuzwa kwa Wabunge ni kujenga misingi ya kuimaliza CUF Bara kuifanya isiwe na nguvu na hapa Maalim Sef anaiuza CUF Bara kwa bei poa. Haya sio maneno yangu, ni maneno ya Professa Lipumba wakati akiongea na Clouds FM katika kipindi cha Power Breakfast.

Kuhusu uwepo wa Lowassa ndani ya UKAWA Professa anasema, “Sababu za msingi za kutomkubali Mh. Edward Lowassa kuingia UKAWA, ni kwamba ukiwa katika siasa unahitaji uongozwe na misingi na 'principals' na hoja kwamba mnagombea kitu gani, na sisi tulianzisha UKAWA kwa kusema kwamba tutafute nchi, serikali na dola inayowajibika ambayo inatengeneza mambo vizuri, inatumia rasilimali vizuri itapambana na ufisadi na itajenga demokrasia ya kweli katika nchi yetu,

Ukiwa na misingi hiyo kwamba utataka kiongozi ambaye anaunga mkono misingi hiyo na tulikuwa wote kwenye bunge la katiba na Mh. Edward Lowassa alikuwepo kwenye bunge hilo hakuwa mmoja ya wabunge aliyeunga mkono rasimu ya Katiba" Ibrahim Lipumba

"Kwahiyo ilikuwa ni kinyume kabisa na ile misingi iliyotuunganisha kwamba utataka kiongozi ambaye anaunga mkono misingi hiyo na ukumbuke Mh. Edward Lowassa alikuwepo katika bunge la katiba ya rasimu ya Jaji Warioba na hakuunga mkono rasimu hiyo kwahiyo ilikuwa ni kinyume kabisa na ile misingi iliyotuunganisha na kuanzisha UKAWA kuja kumchukua Edward Lowassa ndiye awe mgombea urais wa watu wanaounga mkono rasimu ya Jaji Warioba" Ibrahim Lipumba
 
Ameunguruma Azam TV, muungurumo wake haukudondosha hata jani!!

Huko PB ya akina Masoud Kipanya na Barbara Hassan anakuja na muungurumo gani vile?

Kwa nini profesa asimwige mwenzake Dr Slaa? Alisema anaachana na siasa na kweli, aliacha.

Japo Dr Slaa naye alikimbia mapambano wakati aliokuwa anahitajika sana CHADEMA, however binafsi namkubali huyo Dokta kwa kuwa ni mtu mwenye msimamo thabiti na anasimama ktk principles zake, hayuko easily twisted.

Lol...! Lakini huyu Profesa wa kinyamwezi sijui karogwa na nani tu hata kutaka kuharibu legacy yake ndogo aliyokuwa ameibakisha ktk harakati za siasa za vyama vya upinzani Tanzania!!

Yaani yeye haoni kabisa kuwa CCM wanamtumia kama taulo la guest house tu na mwisho wa siku litaanikwa nje likauke kisha aje achukue/apewe mwingine
kujifutia?
 
Ni aliyekua mwenyekiti wa CUF Profesa Ibrahim Haruna Lipumba kesho anatarajiwa kuzungumzia mgogoro unaoendelea ndani ya CUF kupitia kituo cha Clouds fm ktk kipindi kinachoruka asubuhi.

Je mjadala huo unamnufaisha nani?
mgogoro anao yeye tu., CUF kama chama kipo salama na shuuli zinaenda kama kawaida, asubiri kufukuzwa kabisa kabisa uwanachama soon
 
Ni aliyekua mwenyekiti wa CUF Profesa Ibrahim Haruna Lipumba kesho anatarajiwa kuzungumzia mgogoro unaoendelea ndani ya CUF kupitia kituo cha Clouds fm ktk kipindi kinachoruka asubuhi.

Je mjadala huo unamnufaisha nani?
Atazunguka kwenye media kutafuta hisani kama kina Mtela nyakati zile mwishoooooooni ataishia kuvaa nguo yetu ya chama tawala maana atakuwa amechoka tayari. Karibu ccm Lipumba
 
Lipumba naye ameshachoka sana kifikra. Alijiuzulu mwenyewe na kuitosa CUF. Sasa anachotaka nini huyu mchumi. Si aende tu kisarawe akalime tikiti na mihogo maisha yaendelee?
 
Anahojiwa na Kipanya,
Anaeweza kutiririka live updates aendelee i'm little bit busy
 
Inawezekana kuwa kweli mie nakumbuka uchaguzi wa mwaka jana ulijaa sarakasi za kila aina
Nimpongeze tu mzee wangu Warioba kwa kukataa kuitosa CCM licha ya tofauti za kimtazamo alizokuwa nazo wakati ule kati yake na wanaccm Wenzie
Huo ndo ukomavu wa kisiasa
 
Viongozi wa aina hii hawafai. Dr Slaa na Prof Lipumba, hawajui mchezo wa siasa. Mnakosana na wenzako wewe unaanza kumwaga mtama, hii ni kuharibia vyama siku zijazo. Ni ujinga wa kiwango chake kama hatumiki.
 
barafu....BP ni BP ya clouds fm...na 360 ni 360 ya clouds tv

Siyo "BP" mkubwa bali usahihi ni "PB" ikiwa ni kifupi cha maneno "Power Breakfast!"

NOTE: Kwa manufaa ya wasio familiar na kipindi, kwamba, hiki ni kipindi kinachoruka "live" kupitia Radio Mawingu (Clouds FM Radio) kila siku za jumatatu - Ijumaa kuanzia saa 12: 00 - 4:00 asubuhi

Huhusisha live talks, music, local ad international sports news & etertainments

unajua dk mihogo analipiwa na nani kuishi Canada?

Sijui. Na nani vile?

Na ndo kusema naye ni suala la muda tu, kwamba, atarudi kuja kudai nafasi yake ya party GS?
 
Back
Top Bottom