Kuhusu Muungano, Makamo wa Kwanza wa Zanzibar, Adai ni Zanzibar Pekee iliyopoteza Sovereignty, Je Yuko Sahihi?

Umewahi sikia mahali kuna ubalozi wa Scotland, Wales, Northern Ireland, Catalonia, California, Texas, Kerala n.k.? Tangu lini umesikia barabara za Zanzibar zimeingia kwenye bajeti ya Tanganyika? Kama mnataka kuwa na balozi zenu vunjeni Muungano. Badala ya kuzunguka mbuyu mwambieni Rais wa JMT kuwa hamtaki Muungano, sio kujificha kwenye kile mnachoita kero. Pitisheni muswaada kwenye Baraza lenu la kusema kuwa hamtaki Muungano. Chama chake cha ACT Wazalendo kiweke kwenye ilani yake kuwa hakitaki Muungano. Shida kwani iko wapi? Fanyeni hivyo halafu muuone watanganyika wangapi watawabembeleza. Na mnaweza kukuta ndugu zenu wenyewe watawageuka.

Amandla...
acha povu., tumesema Tanganyika wamechukua mamlaka ya Nchi ya Zanzibar juzi kwenye kero za muungano selemani jaffo amesema wametoa kibali cha zanzibar kuruhusiwa kujenga barabara za chake chake mkoani, Wazanzibar wanahoji kwanini vibali vya maendeleo ya Zanzibar vinatoka tanganyika?

Wanaoutaka muungano na kuubembeleza zaidi sio wazanzibari ni Watanganyika maana ndio wanaonufaika nao wamekuwa wakiinyonya zanzibar miaka nenda miaka rudi sasa ccm wa zanzibar hawawezi inua mdomo kusema chochote., Ofisi za TRA zimejazana Zanzibar zinakusanya kodi kutoka kwa wazanzibari zikiwanufaisha watanganyika kulipana mishahara, posho na chakula chao cha kila siku.

Kama nchi 2 huru zimeungana kwanini mamlaka ya kuteuwa mabalozi kuwakilisha tanzania wanatoka bara pekee? Wazanzibar wamekuwa wakiukataa muungano miaka yote lakini ni kwa sababu zanzibar imepokwa soverenity yake toka enzi za mchonga meno., kwanini Karume aliuwawa?? lete majibu
 
Pitia uongo wake mwingine huu




Wanabodi,

Wale wenye access na Plus TV, watch now kipindi cha Uso kwa Uso, Makamo wa Kwanza wa Zanzibar, Mhe. Othman Masoud Othman asema uongo wa wazi wa mchana kweupe kuhusu muungano wetu.

Mhe. Masoud anadanganya u kuwa Tanganyika na Zanzibar tulipoungana, ile 1964, ni nchi moja tuu ya Jamhuri ya Watu wa Zanzibar, ndio pekee iliyopoteza sovereignity yake na kuikabidhi kwa Jamhuri ya Tanganyika, lakini Tanganyika haikupoteza sovereignity yake, bali Tanganyika ilibadili tuu jina kutoka Tanganyika kugeuka Tanzania with its sovereignity, kitu ambacho sii kweli!.

Kiukweli kabisa Tanzania bado tunahitaji sana civic éducation kuhusu huu muungano wetu, hata kwa baadhi ya Viongozi wetu, hawaujui vizuri huu muungano wetu hivyo wanapotosha bure watu wao na umma kwa ujumla.

Msingi mkuu wa muungano wetu ni dhima, kuwa sisi Watanzania ni ndugu moja, sisi ni wamoja, hivyo muungano ni kurudisha tuu asili yetu iliyotenganishwa na wakoloni. Dhima hiyo ndio ikatumiwa na Nyerere na Karume kuasisi huu muungano uliopo hadi leo. Hivyo anapoibuka kiongozi yeyote kutaka kuipotosha hii Dhima, Wazalendo tuliopo tunaoujua ukweli huu hatuwezi kunyamaza !.

Ukweli ni kuwa, tulipoungana ile 1964, nchi zote mbili, Jamhuri ya Tanganyika na Jamhuri ya Watu wa Zanzibar, nchi zote mbili zilipoteza sovereignity zake, kwa Zanzibar kupoteza sovereignity yake na kuikabidhi kwa Tanzania, la Tanganyika pia sio tuu ikapoteza sovereignity yake, bali hadi jina lake la Tanganyika na kuikabidhi kwa Tanzania. Tukaunda taifa moja jipya la Tanzania lenye nchi mbili ndani yake na zote hazina sovereignity zake. Nchi iliyokuwa Jamhuri ya Watu wa Zanzibar ikawa haipo tena na nchi ya Jamhuri ya Tanganyika pia ikawa haipo, kilichopo ni nchi moja mpya ya JMT, ambayo ina sehemu mbili, Tanzania Bara iliyokuwa Tanganyika na Tanzania Visiwani, au Tanzania Zanzibar iliyokuwa Jamhuri ya Watu wa Zanzibar.

Mimi sitatizwi na uongo wowote wa kawaida ambao hauna madhara, lakini uongo mkubwa kama huu, kuhusu muungano wetu adhimu, na kutoka kwa mtu mwenye cheo kikubwa kama hiki, aliyekuwa mwanasheria Mkuu wa Zanzibar, huu ni uongo wenye madhara makubwa kwa mustakabali mwema wa muungano wetu. Uongo kama huu una kitu kinachoitwa "ill motives" kwenye "the reasons or motivés behind" Jee lengo la uongo huu ni nini?.

Wakati wa Bunge la Katiba, niliwahi kutoa angalizo hili kuhusu mtu huyu
na kweli Dr. Shein alimshughulikia.

Muungano wetu ni muungano wa nchi mbili zenye hadhi sawa sawa, hakuna mkubwa wala mdogo, ndani ya muungano Tanganyika na Zanzibar ziko sawa sawa na zote mbili zilipoteza sovereignity zake na kuikabidhi kwa serikali ya JMT.

Muungano wetu ni aina ya muungano very unique duniani, kimataifa muungano wetu ni union wa nchi mbili zimeungana na kuunda nchi moja ya Tanzania. Hivyo Tanzania kimataifa ni nchi moja ya JMT, ni taifa moja, ni dola moja yenye rais mmoja, rais wa JMT ambaye ni Samia. Pia tuna Amiri Jeshi Mkuu mmoja tuu. Kimataifa Zanzibar sio nchi, Zanzibar ni sehemu ya JMT yenye utawala wake wa ndani.

Muungano wetu ndani ya muungano, muungano wetu ni muungano wa nchi mbili, yaani federation, hivyo ndani ya muungano, Zanzibar ni nchi, yenye rais wake, serikali yake, ina katiba yake, ambayo mabadiliko yaliyofanywa 2010 kuunda SUK, hayatambuliwi na katiba ya JMT. Kwa vile ndani ya muungano Zanzibar ina mamlaka yake huru bila kuingiliwa na serikali ya JMT, la katiba hiyo ni kwa ajili ya mambo yake ya ndani, japo katiba hiyo iko kinyume cha katiba ya JMT, lakini kwa vile ni ya ndani ya Zanzibar,

Kwa upande wa GNU au SUK,
ni serikali ya coalition. Kwenye coalition zote kuna the majority na a minority. A minority ndani ya coalition anatekeleza sera za à majority. Hivyo Viongozi wa ACT ndani ya serikali ya SUK ya Zanzibar, wanatekeza sera CCM.

Hivyo Viongozi wote wa ACT Wazalendo waliomo ndani ya Serikali ya Umoja wa Kitaifa ya Zanzibar wanapaswa kuhubiri na kutekeleza sera za CCM, hivyo hata wanapoalikwa popote kwenye public, watatanguliza maslahi ya Zanzibar kwa mujibu wa sera za chama tawala.

Sasa mtu huyu ndio yuko ndani ya nyumba, yuko jikoni kabisa, asipothibitiwa, amini usiamini, amini nawaambieni akija tokea kufika kule juu kileleni, very soon, tutagawana fito!.

Paskali
 
Mh, Pasco kama kuna mgongano wa katiba zetu hizi, ya JMT na SMZ na tukiingia ktk ufafanuzi unasema inayotakiwa ionekane batili ni ya Zanzibar unafikiri kuna siku wa Zanzibar watakubali yakwao isahihishwe? Kama si kukubali tufanyee hii ya JMT kuitambua Zanzibar kama nchi ili kunusuru muungano wetu
Kwa vile katiba ya Zanzibar inatumika Zanzibar only na huku Tanzania haitumiki, huo ubatili wa katiba ya Zanzibar dhidi ya katiba ya muungano, hauna madhara yoyote kwa muungano wetu, hivyo JMT, haina sababu kuingilia, inaihesabu ni mambo ya ndani ya Zanzibar, hivyo yasiingiliwe.

Tena kwa maoni yangu, for the sake of harmony, nashauri katiba ya JMT ifanyiwe marekebisho na kuingiza vipengele vya mabadiliko chanya ya katiba ya Zanzibar ambavyo havileti ubatilifu kwenye katiba ya JMT, kama suala la GNU, halafu hayo mambo ya Zanzibar kujiita nchi, tuwaachie Wenyewe Wazanzibari na katiba yao, lakini ukweli halisi wa Zanzibar sio nchi bali ni sehemu ya JMT, unabaki ndani ya katiba ya JMT, huku muungano tukiulinda kwa gharama yoyote.

Kama kule nyuma tumeulinda muungano kwa gharama kubwa ikiwemo mtu kutoka Zanzibar kuitwa Dodoma, akaenda na ving'ora na kutoka bila ving'ora, then hatuwezi kushindwa kunyamazisha chokochoko zozote za kuuchokoa muungano. Naendelea kuwashauri hawa wenzetu Wazanzibari humu, hizi chokochoko, wamchokoe pweza, muungano hawatauweza.
P
 
acha povu., tumesema Tanganyika wamechukua mamlaka ya Nchi ya Zanzibar juzi kwenye kero za muungano selemani jaffo amesema wametoa kibali cha zanzibar kuruhusiwa kujenga barabara za chake chake mkoani, Wazanzibar wanahoji kwanini vibali vya maendeleo ya Zanzibar vinatoka tanganyika?

Wanaoutaka muungano na kuubembeleza zaidi sio wazanzibari ni Watanganyika maana ndio wanaonufaika nao wamekuwa wakiinyonya zanzibar miaka nenda miaka rudi sasa ccm wa zanzibar hawawezi inua mdomo kusema chochote., Ofisi za TRA zimejazana Zanzibar zinakusanya kodi kutoka kwa wazanzibari zikiwanufaisha watanganyika kulipana mishahara, posho na chakula chao cha kila siku.

Kama nchi 2 huru zimeungana kwanini mamlaka ya kuteuwa mabalozi kuwakilisha tanzania wanatoka bara pekee? Wazanzibar wamekuwa wakiukataa muungano miaka yote lakini ni kwa sababu zanzibar imepokwa soverenity yake toka enzi za mchonga meno., kwanini Karume aliuwawa?? lete majibu
Chuki kweli inapofusha! Luteni Humud Mohammed Humud ndie aliyempiga risasi Karume. Baba yake Luteni Humud, Mohammed Humud alimuua Sheikh Ahmed el Mugheiry mwaka 1955. Wote hawa walikuwa waarabu. Karume alimtoa gerezani Mohammed Humud mara baada ya mapinduzi ya mwaka 1964. October mwaka huo huo alitiwa ndani na Karume. Baadae mtoto wake aliambiwa na wafungwa walioachiwa kuwa baba yake aliteswa na kuuliwa. Hii ndio iliyomsukuma kumuua Karume. Hata hivyo wengi walihusisha mauaji yale na juhudi za chama cha Umma kutaka kuipundua serikali ya Afro Shirazi. Wakina Babu waliisha kwaruzana na Karume kwa vile waliaminikuwa hakuwa mjamaa vya kutosha. Salama ya Babu ilikuwa ni kuwekwa ndani Tanzania Bara na baadae kuachiwa.

Historia ya Zanziba imejaa chuki, mauaji na visasi. Karume asingeweza kuvunja Muungano kwa sababu alikuwa hana imani na waarabu pamoja na vijana wakijamaa wa kiarabu wa chama cha Umma. Kusema kuwa Muungano ni kama koti ni maneno tu ya kiasa kwa sababu alijua asingeweza kudumu nje ya Muungano.

Anayeteua mabalozi ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambae mara mbili sasa ametokea Zanzibar. Au ulitaka Rais wa Zanzibar awe anateua mabalozi wake?

Wizara ya Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi chini ya Waziri Rahma Kassim Ali ndio inasimamia ujenzi wa barabara Zanzibar. Kama Jaffo alizungumza itakuwa ni kwa sababu SMZ kuomba msaada JMT ili waweze kuijenga. Barabara ya Ole Kengeja ilitengewa bilioni 6 na SMZ lakini zilizotolewa ni bilioni 1.4 tu. Bila shaka barabara aliyoizungumzia Jaffo nayo ilikuwa katika hali hiyo hiyo na Machogo bila hiana wameamua kuwasaidia kumalizia. Lakini kwa roho yako ya korosho huwezi kuona hilo.

Amandla...
 
Chuki kweli inapofusha! Luteni Humud Mohammed Humud ndie aliyempiga risasi Karume. Baba yake Luteni Humud, Mohammed Humud alimuua Sheikh Ahmed el Mugheiry mwaka 1955. Wote hawa walikuwa waarabu. Karume alimtoa gerezani Mohammed Humud mara baada ya mapinduzi ya mwaka 1964. October mwaka huo huo alitiwa ndani na Karume. Baadae mtoto wake aliambiwa na wafungwa walioachiwa kuwa baba yake aliteswa na kuuliwa. Hii ndio iliyomsukuma kumuua Karume. Hata hivyo wengi walihusisha mauaji yale na juhudi za chama cha Umma kutaka kuipundua s

Wanaona basi, wao ndio hutunyonya sisi sasa tumeshtuka
 
Kwa vile katiba ya Zanzibar inatumika Zanzibar only na huku Tanzania haitumiki, huo ubatili wa katiba ya Zanzibar dhidi ya katiba ya muungano, hauna madhara yoyote kwa muungano wetu, hivyo JMT, haina sababu kuingilia, inaihesabu ni mambo ya ndani ya Zanzibar, hivyo yasiingiliwe.

Tena kwa maoni yangu, for the sake of harmony, nashauri katiba ya JMT ifanyiwe marekebisho na kuingiza vipengele vya mabadiliko chanya ya katiba ya Zanzibar ambavyo havileti ubatilifu kwenye katiba ya JMT, kama suala la GNU, halafu hayo mambo ya Zanzibar kujiita nchi, tuwaachie Wenyewe Wazanzibari na katiba yao, lakini ukweli halisi wa Zanzibar sio nchi bali ni sehemu ya JMT, unabaki ndani ya katiba ya JMT, huku muungano tukiulinda kwa gharama yoyote.

Kama kule nyuma tumeulinda muungano kwa gharama kubwa ikiwemo mtu kutoka Zanzibar kuitwa Dodoma, akaenda na ving'ora na kutoka bila ving'ora, then hatuwezi kushindwa kunyamazisha chokochoko zozote za kuuchokoa muungano. Naendelea kuwashauri hawa wenzetu Wazanzibari humu, hizi chokochoko, wamchokoe pweza, muungano hawatauweza.
P
Sisi tuakuchokoa weye paskali mwanzo na wenzako halfu ndio pweza ww ni kuwadi wa siasa ya ccm tunakujua kuwa una chuki na Zabnzibar na Wazanzibari Unafikiri Zanzibar kama nchi ya mama ako utaikoma na huo muungano iko siku utavunjika mwandishi mjinga asiejua alama za wakati tuko ktk ulimwengu wa DOT COM .
 
Chuki kweli inapofusha! Luteni Humud Mohammed Humud ndie aliyempiga risasi Karume. Baba yake Luteni Humud, Mohammed Humud alimuua Sheikh Ahmed el Mugheiry mwaka 1955. Wote hawa walikuwa waarabu. Karume alimtoa gerezani Mohammed Humud mara baada ya mapinduzi ya mwaka 1964. October mwaka huo huo alitiwa ndani na Karume. Baadae mtoto wake aliambiwa na wafungwa walioachiwa kuwa baba yake aliteswa na kuuliwa. Hii ndio iliyomsukuma kumuua Karume.
Mkuu Fundi Mchundo, asante kwa kisa hiki ambacho lei ndio mara yangu ya kwanza kukisikia na nimekisikia kwako. Kiukweli kuna mengi ya huko kwa wenzetu Zanzibar, hayasemwi. Nashauri yale mabaya maovu yoliyotokea Zanzibar baada ya yale Mapinduzi Matukufu ya 1964, tusiyakumbushie, yasije tonesha makovu yakaleta machungu.
Zanzibar tunaipenda, Wanzibari, tunawapenda, muungano utadumu milele as long as na CCM itaendelea kutawala milele.
P
 
Mkuu Fundi Mchundo, asante kwa kisa hiki ambacho lei ndio mara yangu ya kwanza kukisikia na nimekisikia kwako. Kiukweli kuna mengi ya huko kwa wenzetu Zanzibar, hayasemwi. Nashauri yale mabaya maovu yoliyotokea Zanzibar baada ya yale Mapinduzi Matukufu ya 1964, tusiyakumbushie, yasije tonesha makovu yakaleta machungu.
Zanzibar tunaipenda, Wanzibari, tunawapenda, muungano utadumu milele as long as na CCM itaendelea kutawala milele.
P

Siku CCM ikianguka upande wowote ule na Muungano unafia hapo au wakiruhusu kura ya wazi juu ya muungano unafia hapo hapo
 
Sisi tuakuchokoa weye paskali mwanzo na wenzako halfu ndio pweza ww ni kuwadi wa siasa ya ccm tunakujua kuwa una chuki na Zabnzibar na Wazanzibari Unafikiri Zanzibar kama nchi ya mama ako utaikoma na huo muungano iko siku utavunjika mwandishi mjinga asiejua alama za wakati tuko ktk ulimwengu wa DOT COM .
Mkuu Resurrection , chuki ya Zanzibar itoke wapi and for what?. Tena ujue kiukweli baadhi yetu huku bara, tunawapenda sana Wanzanzibari waki Zanzibari kuliko Wabara wakibara!. Kama unasubiria muungano uvunjike, then utasubiri sana, kama fisi anavyomfuata binadamu kwa nyuma, akiangalia jinsi anavyotingisha mikono, fisi anamfuata huku ana,ezea mate akiamini hiyo mikono imeregea karibu itaanguka. Utasuburi sana!.
P
 
Kwanza rekebisha. Jee in makamo was kwanza au wa Pili. Kwenye mada.
Mtoa mada wewe ni mkereketwa ulie na chuki zilizojificha dhidi ya Zanzibar.

Kujificha nyuma ya kiini macho cha Tanzania wakati unajua fika by practice na reality kilichoondoka ni neno Tanganyika tu.

Hakuna Muungano huu. Wizara za Tanganyika kwa mambo ya Tanganyika zinaitwa za Tanzania.

Kibaya zaidi kumezaliwa matatizo kibao ya Muungano Leo zinaitwa kero. Lkna shida ni mfumo na muundo. Linapokuja suala LA haki za Zanzibar, wasomi wote wa Bara na wachambuzi wanakuwa wanafiki.

Nini kimejificha nyuma ya chuki hii?
Kuna wakati huwa nahisi Zenj wanajiliza-liza sana! Wana tabia ya kudeka sana! Ni kweli kuna matatizo ambayo ni ya msingi, lakini matatizo hayo yako pande zote mbili. Ubaya zaidi, ktk matatizo hayo, Zenj wanapewa upendeleo bila sababu tofauti na watu wa bara. Mfano. Mtu wa Zenj anapewa ajira bara kwenye wizara ambayo siyo hata ya muungano, lakini hakuna mtu wa bara anayeweza kupewa hata kiti ndani ya ofisi ya SMZ! Wanafunzi wa Zenj wanalipiwa na bodi ya mikopo wakati elimu siyo muungano.

Ndani ya Muungano kuna mambo Z'bar inayakosa na yanafanywa kwa utu jambo ambalo siyo zuri. Mfano, FIFA, Mikataba ya hali ya hewa, nk. Wakati huo huo wanafaidika mfano na WHO ingawa afya siyo muungano.
 
Watanganyika wametugaidi waZanzibar,haina shida karibuni tunagawana mbao ,halafu tusijuane ,enhee,kwani kuna ulazima ??

Nina uhakika wa asilimia miamoja na nusu ,ya kuwa ndio utakuwa mwisho wa CCM.
 
halafu saivi kama Zanzibar tiyari imeshajitenga kiaina naona ,haifuatilii sana mambo ya pale bungeni ,wanalwepa sababu zisizo na msingi kushirikiana na wadau wabaya.
 
Mkuu Fundi Mchundo, asante kwa kisa hiki ambacho lei ndio mara yangu ya kwanza kukisikia na nimekisikia kwako. Kiukweli kuna mengi ya huko kwa wenzetu Zanzibar, hayasemwi. Nashauri yale mabaya maovu yoliyotokea Zanzibar baada ya yale Mapinduzi Matukufu ya 1964, tusiyakumbushie, yasije tonesha makovu yakaleta machungu.
Zanzibar tunaipenda, Wanzibari, tunawapenda, muungano utadumu milele as long as na CCM itaendelea kutawala milele.
P
Mkuu, inabidi tuyakumbushe ili vidonda vipone. Tusipofanya hivyo wataendelea kufanya wanayofanya kila siku ya kuwarushia lawama zote machogo wakati wao ndio wenye chuki kubwa baina yao.

Tunasahau kuwa baada ya Mapinduzi ni Nyerere aliipa hifadhi meli ya Sultan Jamshid wakati ilikataliwa kupiga nanga Mombasa. Wanasahau kuwa ndugu zake huyo Sultan walikataa kumpokea Oman kwa miaka 50. Aliishi maisha ya ukiwa Uingereza, yeye na familia yake.

Wanasahau jinsi walivyokuwa wakiburuzwa chini ya utawala wa Karume na kuwafanya wengi wahamie kwa machogo ambako walipokewa bila hiana. Hawa hawataki kukiri kuwa ni chuki yao dhidi ya wapemba na waarabu ndio ilimfanye Salim Ahmed Salim asiwe Rais wa JMT.

Wazanzibari wanahitaji a Truth and Reconciliation Commission itakayopitia historia yao bila kificho na wale ambao hawakutendewa haki waombwe msamaha. Amani kamili haiwezi kupatikana wakati watu bado wametunza picha za mahandaki ambamo ndugu zao walizikwa.

Baada ya hapo ndio, kwa pamoja wafanye uamuzi kuhusu huu Muungano ambao kwa kiasi kikubwa umezuia watu kulipizana visasi. Uamuzi wowote watakaoufikia itabidi machogo tuukubali isipokuwa kama sisi tumesema hatutaki Muungano na wao wakasema hawautaki. Muungano uendelee tu kama pande zote wanautaka. Pande moja ikiukataa tuuvunje na tupigiane hesabu halafu kila mmoja aende njia yake. Na kukubali kwa masharti ni kuukataa.

Amandla...
 
Chuki kweli inapofusha! Luteni Humud Mohammed Humud ndie aliyempiga risasi Karume. Baba yake Luteni Humud, Mohammed Humud alimuua Sheikh Ahmed el Mugheiry mwaka 1955. Wote hawa walikuwa waarabu. Karume alimtoa gerezani Mohammed Humud mara baada ya mapinduzi ya mwaka 1964. October mwaka huo huo alitiwa ndani na Karume. Baadae mtoto wake aliambiwa na wafungwa walioachiwa kuwa baba yake aliteswa na kuuliwa. Hii ndio iliyomsukuma kumuua Karume. Hata hivyo wengi walihusisha mauaji yale na juhudi za chama cha Umma kutaka kuipundua serikali ya Afro Shirazi. Wakina Babu waliisha kwaruzana na Karume kwa vile waliaminikuwa hakuwa mjamaa vya kutosha. Salama ya Babu ilikuwa ni kuwekwa ndani Tanzania Bara na baadae kuachiwa.

Historia ya Zanziba imejaa chuki, mauaji na visasi. Karume asingeweza kuvunja Muungano kwa sababu alikuwa hana imani na waarabu pamoja na vijana wakijamaa wa kiarabu wa chama cha Umma. Kusema kuwa Muungano ni kama koti ni maneno tu ya kiasa kwa sababu alijua asingeweza kudumu nje ya Muungano.

Anayeteua mabalozi ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambae mara mbili sasa ametokea Zanzibar. Au ulitaka Rais wa Zanzibar awe anateua mabalozi wake?

Wizara ya Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi chini ya Waziri Rahma Kassim Ali ndio inasimamia ujenzi wa barabara Zanzibar. Kama Jaffo alizungumza itakuwa ni kwa sababu SMZ kuomba msaada JMT ili waweze kuijenga. Barabara ya Ole Kengeja ilitengewa bilioni 6 na SMZ lakini zilizotolewa ni bilioni 1.4 tu. Bila shaka barabara aliyoizungumzia Jaffo nayo ilikuwa katika hali hiyo hiyo na Machogo bila hiana wameamua kuwasaidia kumalizia. Lakini kwa roho yako ya korosho huwezi kuona hilo.

Amandla...
Ndivyo ulivyolishwa maneno sasa umekuwa hardheaded, karume aliuwawa baada kuona sasa mchonga meno alitumia hadaa kumtawala kimabavu kwa kumwambia Zanzibar ni nchi changa mumepata uhuru juzi bora tuungane kukusaidia ulinzi lakini kila siku zilivyoyoyoma ndivyo mchonga meno alihodhi mamlaka ya zanzibar mpaka Karume alivyokuja kudai mambo ambayo hayakuwa kwenye mkataba wa muungano akakikiona alichokiona.,

kwa sababu zanzibar imefungwa miguu na mikono misaada yote kutoka kwa wahisani huombwa ni serikali ya Jamhuri ya Muungano na sasa utekelezaji wake kwa upande wa zanzibar ni lazima kibali kitoke Tanganyika., Sasa Zanzibar kutaka kufanya maendeleo yake ya ujenzi wa barabara na mambo mengine ionekane kama Tanganyika imewafanyia hisani ndivyo munavyoipelekesha Zanzibar. Rais wa Zanzibar hawezi ata kusafiri nje ya nchi bila kibali kutoka Tanganyika ndio maana Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar alimaanisha haya yote., Zanzibar imepokwa soverenity yake.,

Anayeteuwa mabalozi ni Rais wa Jamuhuri lakini jiulize mara ngapi Rais wa Jamuhuri amekuwa akitoka Mkoa wa Tanganyika? Samia amepata urais usiotegemewa baada mwendazake na kwa sababu za kikatiba otherwise sasa munampiga vita asigombee ata hiyo 2025.,
 
Pascal serikali ya Tanganyika ama mamlaka ya Tanganyika yako wapi? Nani Anayasimamia? Ukweli ni kwamba wakati Zanzibar ina mambo yake ambayo huyasimamia yasiyo ya Muungano, kwa Tanganyika hali ni tofauti. Mambo yote hayo hufanywa na serikali ya muungano. Hapa unakataaje kwamba serikali ya Tanganyika ndio serikali ya muungano? Na kinyume chake ni sawa pia.
Wanabodi,

Wale wenye access na Plus TV, watch now kipindi cha Uso kwa Uso, Makamo wa Kwanza wa Zanzibar, Mhe. Othman Masoud Othman asema uongo wa wazi wa mchana kweupe kuhusu muungano wetu.

Mhe. Masoud anadanganya u kuwa Tanganyika na Zanzibar tulipoungana, ile 1964, ni nchi moja tuu ya Jamhuri ya Watu wa Zanzibar, ndio pekee iliyopoteza sovereignity yake na kuikabidhi kwa Jamhuri ya Tanganyika, lakini Tanganyika haikupoteza sovereignity yake, bali Tanganyika ilibadili tuu jina kutoka Tanganyika kugeuka Tanzania with its sovereignity, kitu ambacho sii kweli!.

Kiukweli kabisa Tanzania bado tunahitaji sana civic éducation kuhusu huu muungano wetu, hata kwa baadhi ya Viongozi wetu, hawaujui vizuri huu muungano wetu hivyo wanapotosha bure watu wao na umma kwa ujumla.

Msingi mkuu wa muungano wetu ni dhima, kuwa sisi Watanzania ni ndugu moja, sisi ni wamoja, hivyo muungano ni kurudisha tuu asili yetu iliyotenganishwa na wakoloni. Dhima hiyo ndio ikatumiwa na Nyerere na Karume kuasisi huu muungano uliopo hadi leo. Hivyo anapoibuka kiongozi yeyote kutaka kuipotosha hii Dhima, Wazalendo tuliopo tunaoujua ukweli huu hatuwezi kunyamaza !.

Ukweli ni kuwa, tulipoungana ile 1964, nchi zote mbili, Jamhuri ya Tanganyika na Jamhuri ya Watu wa Zanzibar, nchi zote mbili zilipoteza sovereignity zake, kwa Zanzibar kupoteza sovereignity yake na kuikabidhi kwa Tanzania, la Tanganyika pia sio tuu ikapoteza sovereignity yake, bali hadi jina lake la Tanganyika na kuikabidhi kwa Tanzania. Tukaunda taifa moja jipya la Tanzania lenye nchi mbili ndani yake na zote hazina sovereignity zake. Nchi iliyokuwa Jamhuri ya Watu wa Zanzibar ikawa haipo tena na nchi ya Jamhuri ya Tanganyika pia ikawa haipo, kilichopo ni nchi moja mpya ya JMT, ambayo ina sehemu mbili, Tanzania Bara iliyokuwa Tanganyika na Tanzania Visiwani, au Tanzania Zanzibar iliyokuwa Jamhuri ya Watu wa Zanzibar.

Mimi sitatizwi na uongo wowote wa kawaida ambao hauna madhara, lakini uongo mkubwa kama huu, kuhusu muungano wetu adhimu, na kutoka kwa mtu mwenye cheo kikubwa kama hiki, aliyekuwa mwanasheria Mkuu wa Zanzibar, huu ni uongo wenye madhara makubwa kwa mustakabali mwema wa muungano wetu. Uongo kama huu una kitu kinachoitwa "ill motives" kwenye "the reasons or motivés behind" Jee lengo la uongo huu ni nini?.

Wakati wa Bunge la Katiba, niliwahi kutoa angalizo hili kuhusu mtu huyu
na kweli Dr. Shein alimshughulikia.

Muungano wetu ni muungano wa nchi mbili zenye hadhi sawa sawa, hakuna mkubwa wala mdogo, ndani ya muungano Tanganyika na Zanzibar ziko sawa sawa na zote mbili zilipoteza sovereignity zake na kuikabidhi kwa serikali ya JMT.

Muungano wetu ni aina ya muungano very unique duniani, kimataifa muungano wetu ni union wa nchi mbili zimeungana na kuunda nchi moja ya Tanzania. Hivyo Tanzania kimataifa ni nchi moja ya JMT, ni taifa moja, ni dola moja yenye rais mmoja, rais wa JMT ambaye ni Samia. Pia tuna Amiri Jeshi Mkuu mmoja tuu. Kimataifa Zanzibar sio nchi, Zanzibar ni sehemu ya JMT yenye utawala wake wa ndani.

Muungano wetu ndani ya muungano, muungano wetu ni muungano wa nchi mbili, yaani federation, hivyo ndani ya muungano, Zanzibar ni nchi, yenye rais wake, serikali yake, ina katiba yake, ambayo mabadiliko yaliyofanywa 2010 kuunda SUK, hayatambuliwi na katiba ya JMT. Kwa vile ndani ya muungano Zanzibar ina mamlaka yake huru bila kuingiliwa na serikali ya JMT, la katiba hiyo ni kwa ajili ya mambo yake ya ndani, japo katiba hiyo iko kinyume cha katiba ya JMT, lakini kwa vile ni ya ndani ya Zanzibar,

Kwa upande wa GNU au SUK,
ni serikali ya coalition. Kwenye coalition zote kuna the majority na a minority. A minority ndani ya coalition anatekeleza sera za à majority. Hivyo Viongozi wa ACT ndani ya serikali ya SUK ya Zanzibar, wanatekeza sera CCM.

Hivyo Viongozi wote wa ACT Wazalendo waliomo ndani ya Serikali ya Umoja wa Kitaifa ya Zanzibar wanapaswa kuhubiri na kutekeleza sera za CCM, hivyo hata wanapoalikwa popote kwenye public, watatanguliza maslahi ya Zanzibar kwa mujibu wa sera za chama tawala.

Sasa mtu huyu ndio yuko ndani ya nyumba, yuko jikoni kabisa, asipothibitiwa, amini usiamini, amini nawaambieni akija tokea kufika kule juu kileleni, very soon, tutagawana fito!.

Paskali
 
Ndivyo ulivyolishwa maneno sasa umekuwa hardheaded, karume aliuwawa baada kuona sasa mchonga meno alitumia hadaa kumtawala kimabavu kwa kumwambia Zanzibar ni nchi changa mumepata uhuru juzi bora tuungane kukusaidia ulinzi lakini kila siku zilivyoyoyoma ndivyo mchonga meno alihodhi mamlaka ya zanzibar mpaka Karume alivyokuja kudai mambo ambayo hayakuwa kwenye mkataba wa muungano akakikiona alichokiona.,

kwa sababu zanzibar imefungwa miguu na mikono misaada yote kutoka kwa wahisani huombwa ni serikali ya Jamhuri ya Muungano na sasa utekelezaji wake kwa upande wa zanzibar ni lazima kibali kitoke Tanganyika., Sasa Zanzibar kutaka kufanya maendeleo yake ya ujenzi wa barabara na mambo mengine ionekane kama Tanganyika imewafanyia hisani ndivyo munavyoipelekesha Zanzibar. Rais wa Zanzibar hawezi ata kusafiri nje ya nchi bila kibali kutoka Tanganyika ndio maana Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar alimaanisha haya yote., Zanzibar imepokwa soverenity yake.,

Anayeteuwa mabalozi ni Rais wa Jamuhuri lakini jiulize mara ngapi Rais wa Jamuhuri amekuwa akitoka Mkoa wa Tanganyika? Samia amepata urais usiotegemewa baada mwendazake na kwa sababu za kikatiba otherwise sasa munampiga vita asigombee ata hiyo 2025.,
Karume aliutaka Muungano kuliko Nyerere. Alikuwa anawahofia waarabu wa nje na ndani ya nchi. Aidha, hakuwa na imani na vijana wenye itikadi ya kikomunisti waliokuwa wanachama wa chama cha Umma ndio maana aliwanyonga wakina Mdungi Ussi, Kassim Hanga, wakina Bharwani na wengine wengi. Kama kweli Karume alitaka kuvunja Muungano ni kwa sababu aliona Nyerere anamuwekea breki kwenye vitendo vyake vya kikatili. Waulize ndugu zako walioishi chini ya utawala wake wakueleze hali ilivyokuwa.

Hamna nchi yenye marais wawili. Kwa sababu hiyo Rais wa Zanzibar siku zote atawajibika kwa Rais wa JMT. Ndivyo ilivyo. Msipotaka awajibike vunjeni Muungano. Semeni wazi kupitia Baraza lenu la Mapinduzi, Serikali yenu na wabunge wenu kuwa hamuutaki Muungano. Acheni unafik wa kujifanya mnataka serikali tatu ( lazima Rais wa JMT atakuwa bosi wa Rais wa Tanganyika na Rais wa Zanzibar) au ya mkataba ( mfano wa E.U hauna mantik kwa sababu E.U sio nchi). Tangazeni kuwa mnataka kuwa nchi kamili iliyo huru. Mnaogopa nini?

Amandla...
 
Wazanzibari wengi wanajuta kumfukuza Sultan na kuungana na Tanganyika. Tena wanaona yale mapinduzi ni kama yalipangwa na watu ambao si Wazanzibari. Sultan wa Oman angekuwa bado anatawala Zanzibar ingekuwa kama Muscat siku hizi. Utajiri wote wa mafuta ya Oman, Wazanzibari wameukosa. Wamebaki na umasikini na kuburuzwa na serikali ya JMT.
Jemshed alikataliwa na ndugu zake wa Oman mpaka alipokaribia kufariki. Mnajidanganya kama mnadhani kuwa wa Oman wangewagia mafuta yao. Kule wanawapokea katika nafasi za kitwana lakini sio za utawala. Jemshed aliruhusiwa kurudi Oman kwa sharti kuwa yeye ni sehemu tu ya ukoo wa kisultani lakini sio mrithi wa usultani.

Mnapenda mno dezo. Mngekuwa kama Comoro sio Oman au Singapore.

Amandla...
 
Back
Top Bottom