Kuhusu Morogoro a.k.a mji kasoro bahari

Kuhusu Morogoro a.k.a mji kasoro bahari

Huu mji ni wa kihistoria. Kipindi hicho cha uhuru ulikuwa ni moja ya miji mizuri sana tatizo haukuendelea kupiga hatua baada ya hapo ndiyo maana unaweza kusema kwa usahihi kabisa kuwa kuna manispaa ni nzuri kuliko Moro. Kwa mfano kama huu mji ungeendelea kukua kwa kasi ya kuridhisha ni wazi ungeweza kufanywa jiji kabla ya Mwanza lakini ndiyo hivyo tena.

Hii "Mji kasoro bahari" ni enzi hizo mkuu sio leo.
 
Niliwahi kuleta uzi hapa kuhusu taswira mbovu ya mji wa Morogoro especially nyumba duni saana,nikasema uchafu uliopo Moro,stend ya daladala Morogoro kule town wamejaa Mama ntilie(ndani ya stend) na majiko yao ya mkaa wanauza vyakula....

Yaaani mji nikichefuchefu hatari...

Moro haikui...kuliko kuishi Moro mjini,ni bora ukaishi zako Tanga mjini........
.
 
Umeme kuna baadhi ya sehemu haujafika tn pale pale Moro mjn
 
Uswahili, ujuaji uwongo ni mwingi sana kwenye huo mji,

Usiseme round about yao ni kubwa kupita zote Tanzania, watakufukuza, wenzako wanasema ni kubwa Afrika Mashariki na kati, wakati akiongea hayo nzi wamejaa kwenye kiatu hajakifua tangu akinunue, utajiuliza hiyo comparison alifanya akiwa wapi.

Baadhi ya vituo vya daladala vipo 100 metres apart, mfano: kuelekea Bigwa - toka rombo unakwenda mita 100 Lyasembe, mita 50 toka hapo ni Yehova, mita 75 toka hapo ni mwanzo wa makaburi, mita 50 toka hapo ni mti mkubwa, mita 70 toka hapo Ikweta.....mnaojua jazieni vinavyofuata nimesahau

Usipo ugua typhoid na UTI hukuwa mji kasoro bahari labda ulikuwa kwingine

Usafi wa round about hauakisi usafi wa ndani ya mji na vyoo vya public, ushahidi nenda kwenye vyoo vya migahawa, vituo vya mafuta, maofisi ya serikali na taasisi zake, vyuo vya ualimu veta nk utajionea kulivyo hovyoooo wakati viongozi wa hizo taasisi wapo kwenye suti day n night

Vitu fake vilivyoshindikana kuuzika Dar kama vipodozi, madawa ya binadamu na mifugo nk vimejaa kila kona ya mji

Ndoa za watu kudukuliwa ni kama kupokezana sigara kwa wavutaji, nilichoka niliposikia driver wa bus anasimulia kuwa mfanyakazi mwenzake hajapata unyumba miezi sita hivyo hajafika kazini kaenda baraza la usuluhishi, hayo ni baadhi ya niliyoyakuta hukooo kusiko na bahari pamoja na kuwa na kila kitu according to them

Umepanic kwenye issue ya vituo hapo, pia unageneralize mno mkuu
 
Niliwahi kuleta uzi hapa kuhusu taswira mbovu ya mji wa Morogoro especially nyumba duni saana,nikasema uchafu uliopo Moro,stend ya daladala Morogoro kule town wamejaa Mama ntilie(ndani ya stend) na majiko yao ya mkaa wanauza vyakula....

Yaaani mji nikichefuchefu hatari...

Moro haikui...kuliko kuishi Moro mjini,ni bora ukaishi zako Tanga mjini........
.

tanga ni majini na ushoga heri nibaki moro
 
Ukipita mitaa ya kuzunguka soko kuu mjini mvua ikinyesha utaipenda harufu yake, mitaro ilivyomibovu na sehemu kama soko la kikundi pamoja na ule mto kikundi miundo mbinu yake hovyo hadi raha kuitazama
 
Kuhusu shida ya maji...morogoro mjini hili ni tatizo sugu, tena linakera saaaaaaanaaa. Ukizingatia moro ipo jirani na MTO RUVU, MTO WAMI, MTO RUAHA, MTO KILOMBERO. Ila kuhusu mzunguko wa pesa ukitoa miji ya dar, arusha, mwanza, unaofuata ni Moro. Kwahyo kuna ugumu wa upatikanaji wa maji, na pia hili suala lipo mikoa yote ya mashariki.....linatutesa saaanaa tatizo la maji.
 
Ni mji mmojawapo ambao unaweza kusoma kuanzia chekechea hadi elimu ya Chuo Kikuu...na pia hata kuajiriwa pasipo kutoka kuenda wilaya nyingine za morogoro au hata bila kuenda mikoa iliyo nje ya morogoro
 
Umepanic kwenye issue ya vituo hapo, pia unageneralize mno mkuu
Hapana Mkuu, jamaa yuko sahihi! Ingawa labda ile ya kutaja mita, lakini ukweli vituo viko karibu karibu sana. Hebu angalia hivi vya Mjini-Mazimbu: Masika, Fire, duka la dawa, Njiapanda, Iringa road, butcher, double M, Ipoipo, Kona kubwa, Shubira, Kabla. ya reli, Mauki, Tumaini, Barakuda, Freedom, n.k!!
 
....

....The Nyumbani na ile vibe iko powa sana landscape nzuri sana Moro... tatizo lenu moro magamba yame wakalia vichwani
 
Je unataka kuoga kwenye bomba la mvua muda wowote utakao? Je unataka kuoga hata ndoo 20 za maji kila siku?, ni rahisi sana, hamia mwanza city, mwanza raha sana
 
Je unataka kuoga kwenye bomba la mvua muda wowote utakao? Je unataka kuoga hata ndoo 20 za maji kila siku?, ni rahisi sana, hamia mwanza city, mwanza raha sana


Bila shaka utakua mwenyeji wangu hapo Mwanza mwezi saba mkuu
 
Je unataka kuoga kwenye bomba la mvua muda wowote utakao? Je unataka kuoga hata ndoo 20 za maji kila siku?, ni rahisi sana, hamia mwanza city, mwanza raha sana
Hongereni sana mwanza, huku dar na moro ni kuna shida ya maji ile mbaya....may be wakubwa wanafanya biashara hii ya maji. Ila ni kero mno kuhusu maji katika miji hii....
 
Minipo moro na mtumishi wa manispaa moro pakidwanzi sana viongozi wa manispaa ya moro hasa afya wanakula pesa za watumishi kiufupi adminstration poor DMO na katibu wamegeuza ofisi ni mali yao wanakera sana hawa jamaa wamejaa rushwa mno
 
Wana mesenger ambae ndo anafanya kazi km DMO na kama katibu inshort watumishi wa moro municipal uozo sijajua km mh Nondo na mkurugenzi km wanajua hilo
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom